Andiko lako linaonyesha fikra za kibinafsi na mlengo wa kidini.
Rais Kikwete kama angetaka kufanya jambo lolote la maendeleo kama ujenzi wa barabara na umeme kwenye sehemu aliyozaliwa asingeshindwa. Nadhani aliamua kutokuwa mbinafsi na kwa maana hiyo, maisha ya wananchi wengi wa maeneo aliyozaliwa yanaakisi maisha ya Watanzania wengi.
Hata Mwl. Nyerere alipong'atuka, Butiama ilikuwa haina huduma bora za kijamii achilia mbali Musoma pamoja na kwamba alikuwa Rais Mkrisitu.
Inashangaza sana kusoma thread za aina hii katika karne ya 21!
ok thread hii sasa yaonesha udini hapa ila mmesahau kijana aliyesimama na kusema rais hatatoka kaskazin na bado wenye mamlaka wakakaa kimya kumbken haya mnavyoandka pia