Wote tulilaumu ufisadi
Kodi zilikuwa hazilipwi?
Rais aliitwa dhaifu kwa kutokuwa mkali!
Wana ccm wakabadili gia Dodoma na kuhama!
Rais alikuwa anasafiri karibu kila mwezi
Lakini barabara zilijengwa, Vyuo vikuu na shule nchi nzima.
Majengo ya kisasa na upanuzi mkubwa wa miji wenye majengo ya kisasa kabisa!
Watumishi wa umma na wafanyabiashara walineemeka!
Na Rais wetu alikuwa full kutabasamu, urais kwake ilikuwa kitu kidogo kama ukiranja wa zamu tu!
Leo sasa!
Kila kitu kimerekebishwa, na rais hacheki cheki!
Lakini Mambo yamezidi kuwa magumu, na hata mwenyewe amesikika akisema anajutia uamuzi wake wa kukitaka kikombe hiki!
Je, ni wakati wa kurejea kupata semina elekezi toka kwa "mkwere"?
Au Mkuu apitie tu kisirisiri hadidu za rejea za serikali ya "mkwere" ili mambo yasiende mrama!