Kikwete alitumia uchawi gani?

Kikwete alitumia uchawi gani?

Uliza deni la taifa lilifikia sh. ngapi?

Uliza mikataba iliyo sainiwa (juu ya malia asili) leo bado inakunufaisha?

ILIKUWA FUNIKA KOMBE MWANAHARAMU APITE. JE TUENDELEE NA STYLE KAMA HIYO?
Mkuu deni hata lingekuwa dola 500bn kama maisha ni easy hapo mbona raha sn, kuliko kuwa na deni kiduchu na bado ya wananchi ni ya kutokujua kesho itafikaje
 
mkuu usipoteze muda tafuta definition ya Leader,,,,,,,,
Then tafuta definition ya Supervisor,,,,,,,,,,,,,,,
Alafu ndo uludi hapa!!!!!
 
Loooooh!mtamkumbuka mkwere the great thinker


Kwa kweli uongozi ni kipaji sio wala elimu, Unaweza ukawa na elimu tosha ila huna sifa ya uongozi...
Kiongozi anatakiwa kuwa mvumilivu, kiongozi ukishasema wewe unajutia uongozi wako je unaowaongoza wawe ktk hali gani?
Kiongozi anatakiwa akubali kuwa yeye ni jalala (kama ilivyo usemi wa wahenga 'Mkubwa jalala') unatakiwa usipanic panic na kuwa na hasira hasira zisizo na mipaka.
Rais ni sawa na Baba na familia yake...sisi ndio watoto wake yeye ni baba.

Mkwere alikuwa anasifa za uvumilivu..Sifa ya uongozi...Japo kuna sifa nyingine hakuwa nazo km za kiufanisi lakini zilitegemea wale wanaomshauri ndio wawe nazo.
 
Ukweli usemwe Mkwere alitupeleka pabaya.
Pamoja na promo kibao za NSSF, NPF, makongamano, masemina elekezi na masherehe matanuzi. Nchi ilizidi kudidimia kiuchumi wakubwa wakizidi kwenda kubembea Dubai Brazili na kwinginepo!!
Ina maana hamukuona wizi na ufisadi uliokuwa unaendelea??
Sioni sababu ya kumsifia mtu aliyedidimiza uchumi wa nchi eti ni kichwa!!
Madawa ya kulevya TZ ikageuka safe heaven ya madealers!!
Lugha za wizi zikazaliwa eti Mchongo , uchakachuaji, maujanja!!
Yote yamezaliwa na watu wa kuliibia taifa letu!!
Mhs Rais awabane warudishe hata fedha walizo ficha huko Ulaya!!
Mtu katawala nchi bila kujali uadilifu bora liende!!

Semina elekezi ni semina zenye maana sana kwa anayeelewa la sivyo ndio utaishilia kukurupuka ktk kazi bila semina elekezi.
NSSF pia kunamazuri yake yaliyofanyika, japo kuna mabaya yake kiasi...Na NSSF huwezi mlaumu JK walaumu viongozi wa NSSF.

Sasa nikuambie Unavyowaongoza Raia ni sawa na Mwalimu na wanafunzi...wewe ukibana huku atatafuta mwanya huu wa kutokea. Hivyo usilaumu saaana Rais, pia jilaumu wewe...Hivi wewe ulishaifanyia nini Serikali yako?
Naamini wewe wewe unayelaumu unaweza pita barabarani ukaona teja kabeba mfuniko ule wa kuzuia maji taka barabarani lkn ukamuacha badala ya kumchukulia hatua,
Wewe wewe unapita unaona mtu anafanya uhalifu Kumuibia mtu, au Kutumia vifaa vya serikali yako hovyo lakini wewe wewe ukamuangalia tuu na kupita kuacha halafu unakaa ukilaumu Rais. Rais hawezi mulika kote, uhalifu wote...Unatakiwa na wewe umsaidie kumulika mwizi.

ACHENI LAWAMA, PIA NYIE MNAPASWA KUJILAUMU NA KUJIULIZA UMEFANYIA NINI NCHI YAKO? ULISHAMCHUKULIA SHERIA NANI KWA UHALIFU TUU JAPO MDOGO MITAANI ILI USAIDIE SERIKALI YAKO KATIKA KUPAMBANA NA UHALIFU?
 
Amekutuma? Atakupa tsh ngap unadhan? We ndo wale mlikuwa mnaingizwa vyuon hamna sifa.maana inawezekana kabisa ulifaidika
Naye. Unaacha kujadili mambo ya msing unaleta hoja za kipuuzi kabisa.


Wote tulilaumu ufisadi

Kodi zilikuwa hazilipwi?

Rais aliitwa dhaifu kwa kutokuwa mkali!

Wana ccm wakabadili gia Dodoma na kuhama!

Rais alikuwa anasafiri karibu kila mwezi

Lakini barabara zilijengwa, Vyuo vikuu na shule nchi nzima.

Majengo ya kisasa na upanuzi mkubwa wa miji wenye majengo ya kisasa kabisa!

Watumishi wa umma na wafanyabiashara walineemeka!

Na Rais wetu alikuwa full kutabasamu, urais kwake ilikuwa kitu kidogo kama ukiranja wa zamu tu!

Leo sasa!

Kila kitu kimerekebishwa, na rais hacheki cheki!

Lakini Mambo yamezidi kuwa magumu, na hata mwenyewe amesikika akisema anajutia uamuzi wake wa kukitaka kikombe hiki!

Je, ni wakati wa kurejea kupata semina elekezi toka kwa "mkwere"?

Au Mkuu apitie tu kisirisiri hadidu za rejea za serikali ya "mkwere" ili mambo yasiende mrama!
 
Uliza deni la taifa lilifikia sh. ngapi?

Uliza mikataba iliyo sainiwa (juu ya malia asili) leo bado inakunufaisha?

ILIKUWA FUNIKA KOMBE MWANAHARAMU APITE. JE TUENDELEE NA STYLE KAMA HIYO?
kuna mtu alikufuata kwako ulipe hilo deni la taifa?,

hata sasa unadhani deni la taifa linazidi ama linapungua?.
Nishasema hapa,hakuna rais atakayevunja rekodi za jk,
mda ndo utaproof right ama wrong,meanwhile imebaki miaka 4 na miezi 4 kufikia uchaguzi mkuu,minyoosho na iendelee
 
Bajeti ya Mwaka huu serikali inakopa trilioni saba...bado kwenye ujenzi wa reli....wachina wakitukopesha trilioni 16,kwa mwaka mmoja serikali inakuwa imekopa trilioni 23.....hebu rudia ...umesema kipindi cha jk deni lilipanda toka ngapi kwenda ngapi?
umesahau zile bilioni karibu 900 alizotoa mmarekani juzi,bado euro nao wametoa,sasa baada ya miaka miwili,deni laweza kuwa mara mbili ya sasa au hata mara tatu,hizo trlion 7 tu kwa mpigo kuzilipa ni ishu kwelikweli
 
umesahau zile bilioni karibu 900 alizotoa mmarekani juzi,bado euro nao wametoa,sasa baada ya miaka miwili,deni laweza kuwa mara mbili ya sasa au hata mara tatu,hizo trlion 7 tu kwa mpigo kuzilipa ni ishu kwelikweli

hapo sasa hakutakuwa na namna itabadi tu tuwaachie gas yao kumaliza deni, lakin nasikia mchina kashailipia cash! au tutawapa hii iliyogunduliwa majuzi.
 
Wote tulilaumu ufisadi

Kodi zilikuwa hazilipwi?

Rais aliitwa dhaifu kwa kutokuwa mkali!

Wana ccm wakabadili gia Dodoma na kuhama!

Rais alikuwa anasafiri karibu kila mwezi

Lakini barabara zilijengwa, Vyuo vikuu na shule nchi nzima.

Majengo ya kisasa na upanuzi mkubwa wa miji wenye majengo ya kisasa kabisa!

Watumishi wa umma na wafanyabiashara walineemeka!

Na Rais wetu alikuwa full kutabasamu, urais kwake ilikuwa kitu kidogo kama ukiranja wa zamu tu!

Leo sasa!

Kila kitu kimerekebishwa, na rais hacheki cheki!

Lakini Mambo yamezidi kuwa magumu, na hata mwenyewe amesikika akisema anajutia uamuzi wake wa kukitaka kikombe hiki!

Je, ni wakati wa kurejea kupata semina elekezi toka kwa "mkwere"?

Au Mkuu apitie tu kisirisiri hadidu za rejea za serikali ya "mkwere" ili mambo yasiende mrama!
Chini ya Kikwete deni la taifa lilifika trl 40. Mambo uliyotaja yalifanywa kwa mikopo badala ya mapato ya ndani na kwa kua uthibiti ulikua mdaifu mikopo mingine iliishia mifukoni mwa watu. Ndio maana Tanzania inaitwa shamba la bibi kwa kuwa wajanja wachache walitafuna fedha ya ndani kwa kutolipa kodi.
 
Kwa kweli uongozi ni kipaji sio wala elimu, Unaweza ukawa na elimu tosha ila huna sifa ya uongozi...
Kiongozi anatakiwa kuwa mvumilivu, kiongozi ukishasema wewe unajutia uongozi wako je unaowaongoza wawe ktk hali gani?
Kiongozi anatakiwa akubali kuwa yeye ni jalala (kama ilivyo usemi wa wahenga 'Mkubwa jalala') unatakiwa usipanic panic na kuwa na hasira hasira zisizo na mipaka.
Rais ni sawa na Baba na familia yake...sisi ndio watoto wake yeye ni baba.

Mkwere alikuwa anasifa za uvumilivu..Sifa ya uongozi...Japo kuna sifa nyingine hakuwa nazo km za kiufanisi lakini zilitegemea wale wanaomshauri ndio wawe nazo.
Huo unafiki wenu wabongo hautaisha aliyepondwa jana leo anasifiwa...anayesifiwa leo huenda kesho akapondwa.
Na hayo yanafanywa kwa sababu jana hakugusa maslahi yake, leo ameyagusa.
Magufuli anaongoza nchi kwa maslahi mapana ya umma na sikufurahisha na kuneemesha kikundi cha watu na wazalendo wa kweli wanayaona mazuri aliyoyafanya kwa muda mfupi aliokaa madarakani na wapi anatupeleka kama Taifa.
Lakini kikubwa tufanyeni kazi, riziki zitapatikana katika kufanya kazi na si kwa kuchonga deal kama tulivyokuwa tumezoea.
 
Uliza deni la taifa lilifikia sh. ngapi?

Uliza mikataba iliyo sainiwa (juu ya malia asili) leo bado inakunufaisha?

ILIKUWA FUNIKA KOMBE MWANAHARAMU APITE. JE TUENDELEE NA STYLE KAMA HIYO?
ULIZA DENI MWAKA HUU TU WA KWANZA LINAONGEZEKA KIASI GANI; 8 TRILLION
 
Ukweli usemwe Mkwere alitupeleka pabaya.
Pamoja na promo kibao za NSSF, NPF, makongamano, masemina elekezi na masherehe matanuzi. Nchi ilizidi kudidimia kiuchumi wakubwa wakizidi kwenda kubembea Dubai Brazili na kwinginepo!!
Ina maana hamukuona wizi na ufisadi uliokuwa unaendelea??
Sioni sababu ya kumsifia mtu aliyedidimiza uchumi wa nchi eti ni kichwa!!
Madawa ya kulevya TZ ikageuka safe heaven ya madealers!!
Lugha za wizi zikazaliwa eti Mchongo , uchakachuaji, maujanja!!
Yote yamezaliwa na watu wa kuliibia taifa letu!!
Mhs Rais awabane warudishe hata fedha walizo ficha huko Ulaya!!
Mtu katawala nchi bila kujali uadilifu bora liende!!

, IDADI YA SHULE ZA SEKONDARI ZILIZOJENGWA KIPINDI CHA JK NI KUBWA KULIKO JUMALA YA SHULE ZA NYERERE MWINYI NA MKAPA KWA PAMOJA! JUMLA YA KILOMETER ZA BARABARA ZILIZOJENGWA KIPINDI CHA JK NI KUBWA KULIKO JUMLA YA KILOMETA ZA BARABARA ALIZOJENGA NYERERE MWINYI NA MKAPA! WAFANYAKAZI TULIKUWA TUNAONGEZEWA MISHAHARA KILA MWAKA JK ANAINGIA MADARAKANI NALIPWA LAKI NNE; AMEONDOKA NALIPWA MIL NNE FOR THE SAME WORK!KILA MWAKA AJIRA RASIMI ZAIDI YA ELFU HAMSINI SERIKALINI; UJENZ WA RELI YA KATI KWA STANDARD GAUGE NI MATUNDA YA JK WALA SIO JPM, SEMA TU UJENZI NDO UNAANZA WAKATI WAKE JPM; LAKINI JPM HAJAWAHI KUKANYAGA MGUU WAKE CHINA KWENDA KUNEGOTIATE
 
Wote tulilaumu ufisadi

Kodi zilikuwa hazilipwi?

Rais aliitwa dhaifu kwa kutokuwa mkali!

Wana ccm wakabadili gia Dodoma na kuhama!

Rais alikuwa anasafiri karibu kila mwezi

Lakini barabara zilijengwa, Vyuo vikuu na shule nchi nzima.

Majengo ya kisasa na upanuzi mkubwa wa miji wenye majengo ya kisasa kabisa!

Watumishi wa umma na wafanyabiashara walineemeka!

Na Rais wetu alikuwa full kutabasamu, urais kwake ilikuwa kitu kidogo kama ukiranja wa zamu tu!

Leo sasa!

Kila kitu kimerekebishwa, na rais hacheki cheki!

Lakini Mambo yamezidi kuwa magumu, na hata mwenyewe amesikika akisema anajutia uamuzi wake wa kukitaka kikombe hiki!

Je, ni wakati wa kurejea kupata semina elekezi toka kwa "mkwere"?

Au Mkuu apitie tu kisirisiri hadidu za rejea za serikali ya "mkwere" ili mambo yasiende mrama!

Kama una akili timamu jiulize japo hata kidogo....hivyo vyuo vilikuwa na ubora gani kielimu? Barabara zilikuwa zinajengwa baada ya wiki mbili kwisha zinaharibika kwa rasharasha ya manyunyu ya mvua na rais bado tu anachekelea makandarasi. Kaingia Magufuli na wataalam wake, makandarasi kibao wamefutiwa leseni kutokana na kugundulika kuwa fake. Majengo mengi ya ghorofa na ya kisasa kabisa yaliporomoshwa chini ya kiwango na rais bado tu alikuwa anacheka.

Vihiyo na wajinga wengi ndiyo walikuwa wafanyakazi katika idara nyeti serikalini na ufanisi wa kazi ulikuwa hakuna kutokana na watu kutokuwa na ujuzi wa kazi. Almashauri zilishindwa kufuatiliwa, bandari ndiyo usiseme. Jiji lilizidi kuwa chafu wakati rais anachekelea tu kuona uchafu umezagaa mjini. Ufisadi ulikithiri huku wanafunzi ambao ni taifa la kesho wakizidi kukaa chini ya minazi na miembe kusoma, rais anacheka tu na kudanganya wadanganyika kuwa hii nchi ni masikini sana huku yeye na genge lake wakizidi kuneemeka.

Mungu aliona mateso wapatayo watanzania na kuhamua kutuletea Magufuli. Kwa vyovyote vile, vihiyo na wabangaizaji wengi watalia na kulalama juu ya hili. Mwenye akili hawezi kamwe kumlaumu Magufuli kwani afanyayo yeye si mageni duniani ila hapa Bongo tunaona mageni na unyanyasaji kwa sababu watu walizoea kubangaiza na kutopenda kufanya kazi.
 
Kama una akili timamu jiulize japo hata kidogo....hivyo vyuo vilikuwa na ubora gani kielimu? Barabara zilikuwa zinajengwa baada ya wiki mbili kwisha zinaharibika kwa rasharasha ya manyunyu ya mvua na rais bado tu anachekelea makandarasi. Kaingia Magufuli na wataalam wake, makandarasi kibao wamefutiwa leseni kutokana na kugundulika kuwa fake. Majengo mengi ya ghorofa na ya kisasa kabisa yaliporomoshwa chini ya kiwango na rais bado tu alikuwa anacheka. Vihiyo na wajinga wengi ndiyo walikuwa wafanya kazi katika idara nyeti serikalini na ufanisi wa kazi ulikuwa hakuna kutokana na watu kutokuwa na ujuzi wa kazi. Almashauri zilishindwa kufuatiliwa, bandari ndiyo usiseme. Jiji lilizidi kuwa chafu wakati rais anachekelea tu kuona uchafu umezagaa mjini. Ufisadi ulikithiri huku wanafunzi ambao ni taifa la kesho wakizidi kukaa chini ya minazi na miembe kusoma, rais anacheka tu na kudanganya wadanganyika kuwa hii nchi ni masikini sana huku yeye na genge lake wakizidi kuneemeka. Mungu aliona mateso wapatayo watanzania na kuhamua kutuletea Magufuli. Kwa vyovyote vile, vihiyo na wabangaizaji wengi watalia na kulalama juu ya hili. Mwenye akili hawezi kamwe kumlaumu Magufuli kwani afanyayo yeye si mageni duniani ila hapa Bongo tunaona mageni na unyanyasaji kwa sababu watu walizoea kubangaiza na kutopenda kufanya kazi.

Unataka kutwambia JPM hakuifanya kazi yake vizuri?, maana yeye ndo alikuwa bosi na msimamizi mkuu wa hayo mabarabara
 
Wote tulilaumu ufisadi

Kodi zilikuwa hazilipwi?

Rais aliitwa dhaifu kwa kutokuwa mkali!

Wana ccm wakabadili gia Dodoma na kuhama!

Rais alikuwa anasafiri karibu kila mwezi

Lakini barabara zilijengwa, Vyuo vikuu na shule nchi nzima.

Majengo ya kisasa na upanuzi mkubwa wa miji wenye majengo ya kisasa kabisa!

Watumishi wa umma na wafanyabiashara walineemeka!

Na Rais wetu alikuwa full kutabasamu, urais kwake ilikuwa kitu kidogo kama ukiranja wa zamu tu!

Leo sasa!

Kila kitu kimerekebishwa, na rais hacheki cheki!

Lakini Mambo yamezidi kuwa magumu, na hata mwenyewe amesikika akisema anajutia uamuzi wake wa kukitaka kikombe hiki!

Je, ni wakati wa kurejea kupata semina elekezi toka kwa "mkwere"?

Au Mkuu apitie tu kisirisiri hadidu za rejea za serikali ya "mkwere" ili mambo yasiende mrama!
Huyu Rais yupo fiti shida yake ni kuisigina demokrasia na utawala wa sheria. Kiuchumi anatupeleka vizuri sana kwa kubana matumizi yasiyo ya lazima. Na kupunguza ajira ambazo hazina msingi
 
Back
Top Bottom