gollocko
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 2,945
- 2,281
Ni malighafi muhimu kwa wachawi
Wazifanyia nini, maana kama kuzipata ni rahisi sana, hasa nywele ambazo huko saloon tunaziacha bila wasiwasi!
Ni malighafi muhimu kwa wachawi
Wazifanyia nini, maana kama kuzipata ni rahisi sana, hasa nywele ambazo huko saloon tunaziacha bila wasiwasi!
Za saluni hazijulikani ni za nani labda mtu akuotee....lakini zile za kunyoana nyumbani ni hatari mno kuzitupa hovyo
Za saluni mara nyingi hutumiwa na wamiliki wa saluni kwa masharti ya mganga kuwa akija mteja mwenye haiba fulani huyo nywele zake usizitupe
Mmiliki huzihifadhi vizuri na kumpelekea mganga kwa ajili ya kutengenezewa dawa ya mvuto
Haa! Mvuto? Inamaana anachukua mvuto wa huyo mwenye nywele au? Vipi na aliyechukuliwa hizo nywele zake hubaki katika hali gani! Halafu Mshana jr, nahisi kuna kitu unataka kufunguka kwenye hii nyuzi ila umeanzia mbali!
Vitu vingine ni upuuzi mtupu na kuliwa hela tu na waganga angalia visaluni vingi vya uswazi pale mlangoni kwa juu hapakosi bahasha, mle ndani ni madawa zikiwemo nywele za wateja
Haya mambo ya mvuto ukweli ni kidogo sana huduma bora mazingira masafi customer care ndio siri ya mchezo
Maofisini mitaani hata kwenye hizi social forums kama hii JF wachawi wapo. Si kuwa usiku wa napiga manyanga au wanenda kwa karumanzila kukuvunjia mayai visa njia panda laah, uchawi wao ni kukufatilia habari zako kujiweka karibu na wewe na kujifanya mtu mwema, akishapata atakacho anaenda kukisambaza huko utasema anasambaza UKIMWI halafu ukiwa shtukia wachawi wanatoaga macho utasema fundi saa anatafuta mshale wa seconds mfyuuuuu zao
Okey! Dunia ina mambo mengi sana, hivyo vibahasha vya saluni sijawahi kuvishtukia, ntaanza kuwa natupia macho kila niingiapo kwenye hizi saluni
Biashara nyingi za mitaani wana hayo mambo kwa sana tuu
Niliwahi kuweka mada haya ya nyamachoma kwenye mabar na mambo machafu yanayofanyika kule bahati mbaya sana ikawekwa kwenye kundi la invalid topic na kuchinjiwa baharini
Kasinde, hii umeshawahi kukutana nayo?
Na alama za nyayo, pale ulipokanyaga!
Zinafanyiwa mambo kuleta mvuto
Kama kuna kitu cha kuogopwa kuliko vyote duniani basi ni binadamu....binadamu ni kiumbe wa kushangaza sana anaweza kucheka nawe machoni lakini rohoni ana lake baya kabisa analokusudia kukufanyia....mara nyingi watu tunaowapenda na kuwasaidia sana nakuwajali kwa kila namna ndio watu ambao huja kutufanyia mambo machafu kabisa.
Kwahiyo inapotokea ukakutana na situation kama hii basi uwe makini na kujua kuwa hawa ndo binadamu walivyo. Kuna mengi ya kujilinda nayo ukiwa na watu unaowaamini sana kwakuwa kama wakidhamiria kukufanyia mabaya basi wataanza na vitu vitu vinavyokuhusu kama nguo za ndani, nywele ulizonyoa kucha , pedi zilizotumika nk nk
Vema vitu vya jinsi hii ukajitahidi kuvitunza na kuvihifadhi sehemu ambazo hakuna mwingine anayeweza kuvifikia.
Wengi wameumizwa kwa njia hii kwahiyo ni vema kuwa makini sana.