Kyawanjubu
JF-Expert Member
- May 13, 2017
- 2,437
- 2,158
we nae umezidi kama season za kihindi dk 5 unasubiri muendelezo wiki iyayoTUENDELEE,
BALAA LA KWANZA
katika mwambao wa Hilo ziwa hapa kijijini ikola Kuna bandari ndogo ambayo inapokea maboti yalioundwa kwa mbao kwaiyo yakifika hapa ikola yanapakia mizigo ya mazao yanapeleka Congo...Sasa kumbe Hawa watu wanaomiliki haya maboti wanarogana hakuna mfano..boti lako likionekana linafanya kazi Sana linazamishwa kichawi ziwani na upepo maarufu uitwao lukuga.
Sasa Kuna mwamba alipewa laki mbili akachote maji kwenye boti la mfanyabiashara mmoja ili hayo maji yapelekwe kwa mganga...mwamba akachukua dili Hilo huyooo mpaka kwenye boti akachota maji na kuyapeleka kwa aliemuagiza.
Basi baada ya siku mbili yule mwamba alietumwa kuchota maji kwenye boti akaanza kuota kidonda mkononi...baada ya wiki Hali ikawa mbaya...Kijiji hakina huduma ya afya zaidi ya maduka ya dawa tu...ikabidi apelekwe kwa mnganga kufika huko ikaonekana jamaa amerogwa kwa kuchota maji botini...ametibiwa na mnganga ikashindikana Hali yake ikazidi kuwa mbaya..ikabidi ndugu wamtafute mmiliki wa boti wamueze Hali halisi.
Mwenye boti akawaambia kuwa boti lake amelizindika kwa waganga zaidi ya ishirini kutoka kongo...kwaiyo hajui ni dawa za mnganga yupi zimempata ndugu yao..baada ya siku tatu mbele mgonjwa akakata Moto... ITAENDELEA
TUENDELEE
Kwanza niwatake radhi ndugu zangu, naandika kwenye notipad halafu ndo nahamishia hapa, sasa simu ilijizima kabla sijasevu, ninatumia kitecno kinasumbua kweli.
BALAA LA PILI
Baada ya jamaa kukata moto, ndugu walikaa kikao wakatoka na azimio moja, kwamba kwa yeyote atakayekuwa amehusika na hicho kifo basi hatabaki salama, yeye na ndugu zake hadi mifungo yote wanayomiliki na panya walioko kwenye nyumba zao.
Wakamzika ndugu yao maisha yakawa yanaendelea.
Sasa yule jamaa aliyesema ameenda kwa waganga 20 alikuwa na mke na mtoto mmoja, siku moja wakatoka ili waende kuzunguka mjini, akapita kule kwenye boti yake ili aangalie kama wametia nanga kiusahihi. Mara mtoto akamwambia baba yake kwamba anataka kupanda boti, baba akamwita na mke wake wakaingia ili wazunguke kidogo ziwani. Sasa wakati wamefika mbele akaibuka yule mwamba aliyefariki, akazima injini, yule baba akashtuka, mara mtumbwi ukapigwa ukageuka. Hao wakawa wa kwanza kwenye ile listi.
ITAENDELEA
we umemaliza?..nimekaa hiko kijiji mwaka jana mwezi wa 8 hd wa 9...
Kwanza siku niliyofika tu sikujua kama ndo nimefka..niliambiwa tu broo ndo tumefika ikola(nikachoka kbsa)
Pili,umeme ulikuwa ushafika ila bdo ulikuwa haujawashwa..duka pekee la vinywaji brd kwa kutumia solar lipo kwa jamaa mmoja anaitwa DIWANI..
Tatu,nilienda ziwani siku moja mida kama ya sa 3 hv asubuh...nikakuta wamama,wadada waliobalehe kbsa wanaogelea wakiwa wamevaa khanga tu na pembeni kuna wanaume wanaendelea na shughuli zao za kuandaa boti kwa ajili ya kuvua jion yake na wala hawana habari..
Nne,Kulikuwa na kombe la N'gombe ambalo lilijumuisha timu kutoka vijiji vyote vya jiran..uwanja unazungushiwa mifuko ya sandarusi then kiingilio 500..na watu wanajaa hatar
Tano,alikuja BROTHER K COMEDIAN..aisee uwanja ulijaa balaa mpk ikabd walinzi washindwe ku handle lile nyomi..na kiingilio kilikuwa 2000 tu..hapo ndo nilipojua kuwa wasanii wanapiga hela sana vijijini...huku mjini tunaona wa kawaida tu
Sita,Kwa mara ya kwanza nilionja supu ya dagaa...mjini kuna supu ya mbuzi,n'gombe na samaki..kule wana supu ya dagaa..ni tamu hatari
Saba,Kuna siku nilienda kijiji cha mbele kidogo ya ikola..aisee kile kijiji kjna sehemu ina muonekano mzuri ajabuu wa ziwa..nikamuuliza mwenyekiti kma naweza kupata kipande cha ardhi..nikaonywesha kipande kina zaidi ya nusu heka kwa laki 1 tu
Nane...Nilienda kutembelea bandari mpya ya KAREMA inapojengwa...aiseee..hii nchi ina miradi mikubwa sana
Tisa,Aisee kuna ndoa za ajabu sana niliziona..yani kule mzee wa miaka 45/50 kuoa mtoto mdogo wa miaka 15 and above ni jambo la kawaida sana..cha msingi awe na uwezo tu wa kuwahonga wazaz wa binti..na mabinti wengi wanazalishwa then mambo yakibadilika wanaume wanawakimbia wanabaki wanahaha tu mtaani..
Kuna siku nilimsaidia mmoja hela ya kula nashangaa kesho yake anakuja na wenzake wawili eti nao niwasaidie...na wote wana watoto!!
Unataka kutiwa mastoryJamani mimi hamu zimenizidi huku njoo endelea
Tatizo msimuliaji anatuweka roho juujuuUnataka kutiwa mastory
Utata gani wakati jamaa anachelewa kuendeleaMkuu hii kauli yako ni tata..
Aisee, SHIKATAATunaendelea,,BALAA LA TANO,,Hapa kileji pamoja kuwa ni sehemu ndogo lakini Kuna sehemu ama kijiwe Cha starehe kinaitwa SHILAWADU aisee eneo Hilo sio powa .hapo vurugu zote kwanzia ulevi madawa ya kulevya ndo sehemu yake. ..Hilo eneo bangi Haina thamani,,sigara zenu za embasi,,sijui spoti na esiemu zinachukuliwa Kama takataka ..hapa ikola sigara maarufu na ya kijanja unaitwa SHIKATAA ,,aisee sio vijana sio wazee sio wakina mama sio wasichana wote wanakwambia sigara ni SHIKATAA,,sigara hiyo inatokea kongo huko mzigo huo ni zaidi ya mundende na vumbi la kongo unaambiwa ni BALAA..,,Hilo eneo la SHILAWADU ni noma usishangae kukutana na shangazi yako toka mkoani huko Arusha ,,songea,ama mwanza anajiuza ,,hapo warembo kutoka mikoa yote utawapata na gesti zote Kijiji kizima wamezikodi wao ..Kuna jamaa alikutana na mama yake mdogo kumbe anajiuza huku kwa wavuvi wakati nyumbani huko singida ameaga amekuja kufunga mzigo wa samaki,,hapo SHILAWADU ndani ya ikola pamoja na watu kupiga vinywaji vikali na vya gharama lakini pombe maarufu unaitwa TEVERE. ,,kunywa madude yako yooote Ila Kama hujanywa tevele watu wanakuona unaigiza ....ITAENDELEA.....
Tunaendelea,,BALAA LA TANO,,Hapa kileji pamoja kuwa ni sehemu ndogo lakini Kuna sehemu ama kijiwe Cha starehe kinaitwa SHILAWADU aisee eneo Hilo sio powa .hapo vurugu zote kwanzia ulevi madawa ya kulevya ndo sehemu yake. ..Hilo eneo bangi Haina thamani,,sigara zenu za embasi,,sijui spoti na esiemu zinachukuliwa Kama takataka ..hapa ikola sigara maarufu na ya kijanja unaitwa SHIKATAA ,,aisee sio vijana sio wazee sio wakina mama sio wasichana wote wanakwambia sigara ni SHIKATAA,,sigara hiyo inatokea kongo huko mzigo huo ni zaidi ya mundende na vumbi la kongo unaambiwa ni BALAA..,,Hilo eneo la SHILAWADU ni noma usishangae kukutana na shangazi yako toka mkoani huko Arusha ,,songea,ama mwanza anajiuza ,,hapo warembo kutoka mikoa yote utawapata na gesti zote Kijiji kizima wamezikodi wao ..Kuna jamaa alikutana na mama yake mdogo kumbe anajiuza huku kwa wavuvi wakati nyumbani huko singida ameaga amekuja kufunga mzigo wa samaki,,hapo SHILAWADU ndani ya ikola pamoja na watu kupiga vinywaji vikali na vya gharama lakini pombe maarufu unaitwa TEVERE. ,,kunywa madude yako yooote Ila Kama hujanywa tevele watu wanakuona unaigiza ....ITAENDELEA.....
Ila mwana utakuwa kuku wa kizunguTatizo msimuliaji anatuweka roho juujuu
Hicho kijiji kipo mkuu yn nikijiji ila nazan kunahaja yakukipa hazi ya mji mdogo nisehemu imechangamka balaa mishe mishe zake pale sio zakibush bush nizamjini mjini hadi wadada wauzaji pale wapo kipindi chamavuno yampunga/ufuta au kipindi samak wanakufa sana bas nao wanatoka tabora,kigoma kuja kuuza ikolaEeh hicho kijiji mbona kama nchi ya kusadikika!
Hivi wewe dogo unaliwa na mboga gani?Ila mwana utakuwa kuku wa kizungu
ulikamata mkweso..pole SanaDa ikola.. Nimepamis sana nakumbuka nilimtembelea rafiki yangu twaha wakati wa mavuno ya ufuta nilikua naenda kuuza mwanza.. Ila starehe za huko nilijikuta nakula mtaji wote na vidosho.. Hali ikawa mbaya hapo ndo nilijifunza kupiga makasia nikapata nauli ya kurudi kwetu.. Ila ipo siku ntarudi tena
Twende kazi mkuubado haijaisha