Kijana usikubali kuletewa mke

Kijana usikubali kuletewa mke

co fm

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2016
Posts
1,569
Reaction score
2,584
I hope mko poa humu,jana katika harakati zangu huwa napenda kuongea sana na watu wapya.Basi, kuna sehemu nikawa nimekaaa na kijana mwenzangu tukawa tunapiga stori mbili tatu.

Katika mazungumzo yetu akagusia kwamba umeoa au,nikamwambia bado akaniuliza kwanini bado? nikamjibu muda ukifika na nikiona kwamba na uhitaji wa kuoa ntaoa.

Mimi pia nikamuuliza wewe vipi umeoa? Akacheka kidogo akanijibu,nimeoa kwa force ya wazazi na mke nimeletewa ila sina mapenzi nae niko nae siku ya nne ndani ila yaani simpendi.

Akaniambia labda nimshauri kutokana na hiyo kadhia, wazazi wake walimforce aoe ila akawaambia subiri kidogo au mnitafutie mwanamke huko nyumbani basi wazazi bila iyana wakamtafutia binti na picha wakamtumia sasa picha ile walikuwa wameizoom jamaa akaona fresh,siku anayoenda mbezi kumpokea jamaa alisema alinyong’onyeka sana hakuamini alichokiona binti ni mdogo sana,mfupi na mwili hana na yeye anapenda nyama nyama.

Baada ya kumpokea ndo leo siku ya nne wapo nae ndani yaani yupo yupo tu kuzimu hayupo dunianu hayupo yaani mwanamke hamvutiii kabisa,akiwaambia kwao anataka amrudishe wanamwambia mlishe mwili utakuja tu la si hivyo utatutia aibu.

Kiufupi jamaa anawakati mgumu. Ndo maana mimi hayo mambo ya kutafutiwa mke siyataki kabisa
 
Wanaume walivyo utashangaa anasema yupoyupo simpendi ila baada ya wiki kadhaa unaona bidadada anapata kichefuchefu

Jamaa kamwekea vijiti asizae nae
 
Wanaume walivyo utashangaa anasema yupoyupo simpendi ila baada ya wiki kadhaa unaona bidadada anapata kichefuchefu
Ndio uleewe tafsiri ya upendo kwa mwanaume sio sex. Tunaweza gonga ata tusio wapenda
 
Kichefu chefu anapata mtu hata kama hapendwi. Sababu ni simba na swala ama mbuzi na majani huwezi waweka pamoja.
Hii sio sawa kabisa...muwe mnafanya hivi kwa hawa maslay queen wa mjini sio hawa watoto decent waliotunzwa
 
Yeye aendelee nae tu kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo atakavyo jikuta anaanza kumkubali
 
Sikuhizi hata waliotafuta wenyewe wanahangaika nafikiri dunia Kuna mahali imebinuka sio kwa Mambo haya yanayotupata!
 
Kwahiyo jamaa kauziwa mbuzi kwenye gunia?

Ila duniani kuna watu wazembe sana. Huyo jamaa ni mmoja wao. Hapo hamna namna ampikie masotojo masaptasapta na marotarota manzi atavuta room tu.
 
Kumbe aendelee kuishi nae basi anaweza kuja kumpenda siku za mbeleni
Ndio hivyo same jamaa inaonekana ana haraka sana ila akiwa na subira anaweza baadae akajikuta yeye ndio anadata kabisaa
 
I hope mko poa humu,jana katika harakati zangu huwa napenda kuongea sana na watu wapya.Basi, kuna sehemu nikawa nimekaaa na kijana mwenzangu tukawa tunapiga stori mbili tatu.

Katika mazungumzo yetu akagusia kwamba umeoa au,nikamwambia bado akaniuliza kwanini bado? nikamjibu muda ukifika na nikiona kwamba na uhitaji wa kuoa ntaoa.

Mimi pia nikamuuliza wewe vipi umeoa? Akacheka kidogo akanijibu,nimeoa kwa force ya wazazi na mke nimeletewa ila sina mapenzi nae niko nae siku ya nne ndani ila yaani simpendi.

Akaniambia labda nimshauri kutokana na hiyo kadhia,wazazi wake walimforce aoe ila akawaambia subiri kidogo au mnitafutie mwanamke huko nyumbani basi wazazi bila iyana wakamtafutia binti na picha wakamtumia sasa picha ile walikuwa wameizoom jamaa akaona fresh,siku anayoenda mbezi kumpokea jamaa alisema alinyong’onyeka sana hakuamini alichokiona binti ni mdogo sana,mfupi na mwili hana na yeye anapenda nyama nyama.

Baada ya kumpokea ndo leo siku ya nne wapo nae ndani yaani yupo yupo tu kuzimu hayupo dunianu hayupo yaani mwanamke hamvutiii kabisa,akiwaambia kwao anataka amrudishe wanamwambia mlishe mwili utakuja tu la si hivyo utatutia aibu.

Kiufupi jamaa anawakati mgumu.Ndo maana mimi hayo mambo ya kutafutiwa mke siyataki kabisa
Unataka kusema jamaa haja tomb* hadi leo

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
 
Kama ana mkula kwa chumvi amlishe hamna namna atapata nyama nyama anazozipenda.
 
Back
Top Bottom