Kujitolea (Volunteer) imekuwa tabia kandamizi katika mfumo wa ajira nchini

nashukuru mzima

JF-Expert Member
Jul 11, 2017
1,014
1,896
Habari,

Kujitolea katika Serikalini au kwenye private kwa sasa imekuwa ni ugonjwa mkubwa sana nchini.

Baada ya Uhaba mkubwa wa ajira nchini, kumekuwa na wimbi la Hali ya mashirika,taasisi za umma na binafsi kuhitaji watu wa kujitolea kwenye sehemu za kazi.

Kiuhalisia kujitolea sio jambo baya kwa sababu ni jambo ambalo linaleta uzoefu mkubwa hasa kwa Fresh graduate na uzoefu kama ilivyokuwa ikifanyika miaka ya awali.

Ila kwa sasa suala la kujitolea limefanywa kama ni aina fulani ya ajira rasmi yenye lengo la kuwanyonya wanaojitolea.

Kwanza kabisa nafasi za kujitolea kwa sasa zinafuata utaratibu wote wa ajira kuanzia kutangaza, kuita watu kwa usaili, kupata watu katika nafasi zinazotakiwa na kuwaingiza kazini.

Ila Watu wengi wanaojitolea pindi wanapoingia makazini wanakutana na mambo kadhaa.

Kwanza Posho/Mshahara mdogo usiokuwa na hadhi hata kidogo ya thamani ya Elimu, yake ukubwa wa majukumu na muda anaotumia kazini unakuta mtu amesoma Account ilibidi alipwe million 1.2 labda ila kwenye kujitolea atalipwa laki 2 na hela inakuja kwa kuchelewa.

Pili Unyanyasaji mkubwa sana katika maeneo ya kazi baina ya wafanyakazi waliojiriwa tayari na wakuu wa Sehemu hizo za kazi wanawanyanyasa sana Wanaojitolea na kuwaona hawana thamani yoyote uonesha kwa vitendo na kwa kusema kabisa.

Tatu Wanaojitolea hawapewi Mikataba yenye kuonesha hali ya matibabu itakayofanyika pindi watakapoumwa, hela ya kujikimu, overtime, ruhusa wala likizo.

Waajiri wengi wanapowachukua Volunteer huwadanganya kwa kuwaambia mkijitolea kwa muda mrefu mtapata ajira ya kudumu suala ambalo utekelezaji wake mdogo.

Hitimisho: Serikali inatakiwa iweke jicho la Tatu kwenye hili suala
 
Ngoja nichangie tofauti taasisi ninayofanyia hawa madogo wanaojitolea especially wahasibu wana katabia kama kuna imprest hawashughulikii kwa haraka kama huwatoi, imekuja kasumba kama una imprest lazima uweke jina lake hii hatarii kwa upande mwingine. Ushauri taasisi hizi zingeangalia jinsi ya kuwalipa.
 
Naunga mkono hoja kuwa litazamwe upya.

Ila nakuulizeni ninyi vijana na akili zenu na usomi wenu hivi kweli ninyi wakufanyiwa hayo yote na elimu unayo, uthubutu unao kwanini kuvumilia ujinga ilihali unaweza kujitafuta kuliko kukaa sehemu unasubiri ajira ambazo hukuagana nazo?

Vijana jitafakirini sana .
 
Acha upotoshaji mshahara wa Mwasibu anaye anza kazi Serikalini ni milioni 1.2?. Kwa mjibu wa muongozo anaye jitolea analipwa 80% ya mshahara na taasisi husika kipitia OC.Mwasibu Serikalini anae anza hulipwa 680,000. Anayejitolea hulipwa 544,000; Ukitoa paye,TRA,Bima n.k atajikuta anapaya chini ya 400,000/.

Madakta wanaonza kazi Serikalini hulipwa milioni 1.2 na wanaojitilea hulipwa 980,000. Tatizo lipo sikuzote makato ni mengi mpaka kupata take home hela inapungua.
 
Acha upotoshaji mshahara wa Mwasibu anaye anza kazi Serikalini ni milioni 1.2?. Kwa mjibu wa muongozo anaye jitolea analipwa 80% ya mshahara na taasisi husika kipitia OC.Mwasibu Serikalini anae anza hulipwa 680,000. Anayejitolea hulipwa 544,000; Ukitoa paye,TRA,Bima n.k atajikuta anapaya chini ya 400,000/.

Madakta wanaonza kazi Serikalini hulipwa milioni 1.2 na wanaojitilea hulipwa 980,000. Tatizo lipo sikuzote makato ni mengi mpaka kupata take home hela inapungua.
Naomba nikutane kwanza wewe ni moumbavu.

Haya Turudi kwa mada.

Asilimia 80%wanaojitolea walipwe hivyo hii ilitoka wapi mkuu.

Watu wana lipwa laki 2 uko ulimwengu wa wapi wewe?

Kuna watu wanaitwa Taesa wanalipwa laki na nusu.

Kuna madaktari wanajitolea wanalipwa laki 4 hadi 5 wewe uko wapi wewe.
 
Naomba nikutane kwanza wewe ni moumbavu.

Haya Turudi kwa mada.

Asilimia 80%wanaojitolea walipwe hivyo hii ilitoka wapi mkuu.

Watu wana lipwa laki 2 uko ulimwengu wa wapi wewe?

Kuna watu wanaitwa Taesa wanalipwa laki na nusu.

Kuna madaktari wanajitolea wanalipwa laki 4 hadi 5 wewe uko wapi wewe.

Ametolea mfano tu
 
Acha upotoshaji mshahara wa Mwasibu anaye anza kazi Serikalini ni milioni 1.2?. Kwa mjibu wa muongozo anaye jitolea analipwa 80% ya mshahara na taasisi husika kipitia OC.Mwasibu Serikalini anae anza hulipwa 680,000. Anayejitolea hulipwa 544,000; Ukitoa paye,TRA,Bima n.k atajikuta anapaya chini ya 400,000/.

Madakta wanaonza kazi Serikalini hulipwa milioni 1.2 na wanaojitilea hulipwa 980,000. Tatizo lipo sikuzote makato ni mengi mpaka kupata take home hela inapungua.
Wewe ni mjinga ...

Samahani Sana kwa kukuambia hivo mkuu
 
Naunga mkono hoja kuwa litazamwe upya.

Ila nakuulizeni ninyi vijana na akili zenu na usomi wenu hivi kweli ninyi wakufanyiwa hayo yote na elimu unayo, uthubutu unao kwanini kuvumilia ujinga ilihali unaweza kujitafuta kuliko kukaa sehemu unasubiri ajira ambazo hukuagana nazo?

Vijana jitafakirini sana .
Mimi nilishaachana na hizo mambo za kujitolea.

Now nafanya biashara zangu za kuingiza hela.
 
Mimi nilishaachana na hizo mambo za kujitolea.

Now nafanya biashara zangu za kuingiza hela.
Hongera sana.
Najua ukoo na familia yako walikuona hamnazo sababu kibongo koo zinaamini kazi za ofisini ndiyo kazi hizi zingine ni kupoteza muda .

Hongera sana keep it up ukijitafuta yanawezekana sana .

Kijana usikubali kulipwa hela ya ngama eti kisa unajitolea na elimu unayo na mtaa unauona ila bado unaendelea kuemyeka kwa majina ya collar jobs kataa ujinga huu .

Dunia imebadirika sana
 
Mkuu hongera sana kwa uzi huu...

Umeniwahi tu.. nilitaka leta hoja hii.

Ni unyanyasaji mkubwa. Sasa hivi imefika mahala mpaka matangazo yanatoka mitandaoni watu waende mkoa fulani wakajitolee kufundisha.

Huu ni upumbavu na unyonyaji uliokithiri. Walimu wamejaa mitaani shule hazina walimu.
Lakini mbaya zaidi hata hao wanaojitolea ajira zinapotoka wanakosa.

Imefika mahali walimu wahitimu wamekata tamaa kabisa na taaluma yao. Hili ni la kupaza sauti.
 
Nmecheka kwa hasira sana huu uzi,sasa mkuu unajitolea halafu unategemea kuheshimiwa? Yaani unajitolea halafu unataka mkataba wa matibabu?

Kwasababu kimsingi pesa anayolipwa mtu anaejitolea hata haikidhi mahitaji ya msingi ni suala la sisi majobless wote kuacha kitu kinaitwa kujitolea totally,hapo ndyo serikali na private sectors wataajili watu,watapewa mikataba na kila stahiki anazotakiwa kupatiwa mwajiliwa kwa mujibu wa sheria za kazi za nchi yetu.

Tofauti na kuacha kujitolea sisi wenyewe hakuna kitu kinaitwa ajira kitakuja kutakuwa rahisi kukipata kwenye hii nchi.
 
Acha upotoshaji mshahara wa Mwasibu anaye anza kazi Serikalini ni milioni 1.2?. Kwa mjibu wa muongozo anaye jitolea analipwa 80% ya mshahara na taasisi husika kipitia OC.Mwasibu Serikalini anae anza hulipwa 680,000. Anayejitolea hulipwa 544,000; Ukitoa paye,TRA,Bima n.k atajikuta anapaya chini ya 400,000/.

Madakta wanaonza kazi Serikalini hulipwa milioni 1.2 na wanaojitilea hulipwa 980,000. Tatizo lipo sikuzote makato ni mengi mpaka kupata take home hela inapungua.
Unaweza kuwa sahihi unachoongea lakini tatizoni je,taasisi zinafuata hzo sheria za mikataba ya wanaojitolea?
 
Shida sio kujitolea. Shida ni mfumo uliowekwa juu ya hilo suala. Sina hakika kama wanafanya monitoring and evaluation ya program hiyo .

Ningekuwa ni Mimi nineishawishi serikali iwekeze pia katika program hiyo huku nikiangalia namna ya kuwaingiza washiriki katika ajira rasmi iwe serikalini au kwenye sekta binafsi

Waziri kazubaa tu
 
Back
Top Bottom