Kijana atangaza kumng'oa Malecela Mtera

Ya Malecela unayakuza mwenyewe kwa kupingana hata na ukweli ulio wazi. Taabu ya kuuvaa umalecela kwa 100%.

- Sio kuvunja sheria, ila hayawasaidiii wananchi wa Tanzania, wala Mtera zaidi tu ya burudani za JF, ni taifa huru siku hizi ingekwua zamani zile enzi zenu ambazo hatukuwa na haki ya kuuvaa u-Malecela 100% kweli,

- lakini thanks to Mwinyi sasa tuko huru, kuuvaa u-Malecela 100% sio kuvunja sheria na Malecela is doing just fine na hizi kelele za mlango I love it bring it on!


FMEs!
 
- Sio kuvunja sheria, ila hayawasaidiii wananchi wa Tanzania, wala Mtera zaidi tu ya burudani za JF, ni taifa huru siku hizi ingekwua zamani zile enzi zenu ambazo hatukuwa na haki ya kuuvaa u-Malecela 100% kweli,

- lakini thanks to Mwinyi sasa tuko huru, kuuvaa u-Malecela 100% sio kuvunja sheria na Malecela is doing just fine na hizi kelele za mlango I love it bring it on!

FMEs!
Bahati nzuri Malecela mwenyewe ni wa enzi zetu. Tunamfahamu kiasi. Wewe ni zaidi ya yeye mwenyewe. Endelea kumwondolea madhambi na mapepo yote yanayoelekezwa kwake hasa baada ya "uhuru" aliotupatia Mzee Mwinyi ambaye pia ndiye aliye muumba upya Malecela wa sasa.
 
- Yale yale tu hakuna jipya na ni waste of our time, nini masilahi ya Mtera hapo juu zaidi tu ya chuki na fitina, Malecela alisema hakusema alisema, sasa hebu tubadili topic za waliosema mazuri tu maisha yao ya uongozi wa taifa, sasa kwa nini taifa limekwama?

- Si kuna waliosema hawawezi kuruhusu hili taifa kwenda mikononi mwa mbwa eti tofauti yake ni nini hasa? Bwa! ha! ha! ha


ES!

.......chongo ni chongo /mbwa ni mbwa/ fisi ni fisi tu huwezi kujibadilisha.....hata ukijtahdi namna gani...true colors zitaoneka tu...........we kama waona ni makengeza/kondoo/chui..........then hayo ni matatizo ya kipenda roho na fikra........... which is moja ya tatizo lililotupatia most of vilaza/majambazi waliopo ndani ya uongozi na kwenye system pia........... and thus to date we are doomed as Taifa........
 
huyu kada wa chama ana strategy nzuri tu ya kisiasa, ambayo naona kama inaweza kumpa umaarufu sana na kumfanya akapewa kura na wana mtera. Japokuwa kumshinda mzee Chigwiyemusi ni mtihani mkubwa sana, maana ana mikoba yote ya CCM yule...anaingia CC mpaka afe, sasa wenzake kweli watamtosa wampe Lusinde???

Hata hivyo hoja yake ya kukubaliana na Malecela si ilikuwa siri yao? Kulikoni anatuletea hoja rahisi rahisi namna hii....?

HK.
 
Mkuu FMEs, heshima mbele!

Aisee, mimi naomba umshauri mzee asigombee this time; hii nchi imedumaa sana kimaendeleo, na yeye ni part and parcel ya uongozi ambao umetufikisha hapa tulipo ... huu ni wakati wa kupata mawazo mapya, uongozi mpya ... nasikitika kusema hawa wazee, including mzee Malecela, hawana jipya ktk kuleta maendeleo, na hasa wakati huu wa karne ya sayansi na teknolojia.

BTW, huyo kijana aliyejitokeza kugombea huko Mtera mimi simfahamu na wala simpigii debe ... ila ninachopigania ni mabadiliko ktk uongozi ... ni vizuri tukapata damu mpya; siyo lazima huyto kijana ndiyo apitishwe kugombea kwa tiketi ya CCM; ninapendekeza mtu mpya apewe ... that's all!

Ni hayo tu mkuu; no pun intended.
 
Mkuu FMEs, heshima mbele!

Aisee, mimi naomba umshauri mzee asigombee this time; hii nchi imedumaa sana kimaendeleo, na yeye ni part and parcel ya uongozi ambao umetufikisha hapa tulipo ... huu ni wakati wa kupata mawazo mapya, uongozi mpya ... nasikitika kusema hawa wazee, including mzee Malecela, hawana jipya ktk kuleta maendeleo, na hasa wakati huu wa karne ya sayansi na teknolojia.

BTW, huyo kijana aliyejitokeza kugombea huko Mtera mimi simfahamu na wala simpigii debe ... ila ninachopigania ni mabadiliko ktk uongozi ... ni vizuri tukapata damu mpya; siyo lazima huyto kijana ndiyo apitishwe kugombea kwa tiketi ya CCM; ninapendekeza mtu mpya apewe ... that's all!

Ni hayo tu mkuu; no pun intended.

- Mimi, wewe na Malecela ndio sababu ya hili taifa kufika hapa tulipo, labda ifike mahali na sisi wananchi tujiuzulu, Bwa! ha! otherwise Mtera we are fine na Malecela! hatuwezi kuamuliwa na makonongo kutoka nje ya jimbo nani anatufaa majimbo yenu yamewashinda sasa mtaweza vipi Mtera nendeni huko pelekeni hao wazungu mahomeless kutoka Brooklyn wawasaidie, Bw! ha! ha!

FMEs!
 
.......chongo ni chongo /mbwa ni mbwa/ fisi ni fisi tu huwezi kujibadilisha.....hata ukijtahdi namna gani...true colors zitaoneka tu...........we kama waona ni makengeza/kondoo/chui..........then hayo ni matatizo ya kipenda roho na fikra........... which is moja ya tatizo lililotupatia most of vilaza/majambazi waliopo ndani ya uongozi na kwenye system pia........... and thus to date we are doomed as Taifa........

- We are doomed kwa sababu ya watu ambao mchana wanaweza kuwa one thing halafu giza likiingia wanakuwa something else, halafu ni wabongo kama sisi ndio maana hili taifa ni doomed, Bwa! ha! ha!


Es
 
Mkuu FMEs, heshima mbele!

Aisee, mimi naomba umshauri mzee asigombee this time; hii nchi imedumaa sana kimaendeleo, na yeye ni part and parcel ya uongozi ambao umetufikisha hapa tulipo ... huu ni wakati wa kupata mawazo mapya, uongozi mpya ... nasikitika kusema hawa wazee, including mzee Malecela, hawana jipya ktk kuleta maendeleo, na hasa wakati huu wa karne ya sayansi na teknolojia.

BTW, huyo kijana aliyejitokeza kugombea huko Mtera mimi simfahamu na wala simpigii debe ... ila ninachopigania ni mabadiliko ktk uongozi ... ni vizuri tukapata damu mpya; siyo lazima huyto kijana ndiyo apitishwe kugombea kwa tiketi ya CCM; ninapendekeza mtu mpya apewe ... that's all!

Ni hayo tu mkuu; no pun intended.

Hapa ndipo tunapokosea wakuu,kijana kaamua kugombea sawa,atakuja mwingine atataka kugombea,sawa,ni demokrasia,hakuna anaywazuia....Lakini ni kitu cha ajabu kumtaka mzee JSM asigombee(kwa sababu ya umri),kama katiba inamruhusu agombee nani atamzuia?,hakuna...muacheni mzee Malecela aitumie fursa yake kikatiba bana...Ni wananchi wa Mtera ndo wanaojua nini mzee JSM kawafanyia katika kipindi chote alichokuwa mwakilishi wao bungeni,so tuwaache wao(wananchi wa Mtera) waamue ni nani wanamtaka awe mwakilishi wao Bungeni kwa kipindi cha 2010-2015(tuiache demokrasia ichukue mkondo wake)

Ni hayo tu mkuu
 
Bahati nzuri Malecela mwenyewe ni wa enzi zetu. Tunamfahamu kiasi. Wewe ni zaidi ya yeye mwenyewe. Endelea kumwondolea madhambi na mapepo yote yanayoelekezwa kwake hasa baada ya "uhuru" aliotupatia Mzee Mwinyi ambaye pia ndiye aliye muumba upya Malecela wa sasa.

- Malecela is doing great na atashinda tena ubunge, aliumbwa na Mungu, Mwinyi alimuomba toka Commonwealth hakuwa jobless, never! pamoja na minjama yote ile, tizama tena historia, mnakuwa na chuki mno hata ukweli hamuuoni, he is just doing fine mkuu dua la kuku unajua halimpati mwewe!

Es!
 
Na Sadick Mtulya

MWANASIASA kijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Katibu wa chama hicho, wilayani Tarime mkoani Mara, Livingstone Lusinde (3 amesema mwanasiasa mkongwe nchini, John Malecela (75) ni mwenye siasa za chuki na pia amemsihi asigombee tena ubunge katika jimbo hilo.

Lusinde alisema kauli ambazo Malecela aliitoa jana, inaashiria kwamba anazeeka vibaya na atamaliza vibaya.

Lusinde ambaye ametoka kijiji cha Mvumi ambako Malecela pia anatoka, alimtuhumu Malecela kwamba ni mbinafsi na kwamba siku zote maneno na ahadi anazotoa si za kweli.

Lusinde alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari wakati akitangaza nia yake ya kugombea ubunge kupitia CCM katika jimbo hilo.

Kutokana na uchovu wa kushindwa kushawishi na siasa za chuki alizokuwa nazo mzee Malecela, uchu wa madaraka usiokuwa na kikomo pamoja na kugeuzwa na watu kumi kama taasisi ya Deci, amesababisha maendeleo duni katika Jimbo la Mtera mkoani Dodoma.

"Pia pamoja na kuwa amewahi kuwa msaidizi wa DC, Mkuu wa Mkoa, Balozi kwenye Umoja wa Mataifa na Uingereza, Waziri wa Kilimo, Mambo ya Nchi za Nje, Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais, Makamu Mwenyekiti wa CCM bara na Mbunge wa Jimbo la Mtera tangu lilipoanzishwa, amekuwa ni mbinafsi na kwamba siku zote maneno na ahadi anazotoa si za kweli,"alisema Lusinde.

Lusinde alifafanua kwamba ameamua kutoa kauli hiyo, kwa kuwa Malecela alikiuka makubaliano waliyoafikiana mwaka 2005 kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu kwamba mwaka huu Malecela, angeachiwa kugombea jimbo hilo.

"Pamoja na Malecela kunilea kisiasa, miaka mitano iliyopita aliniahidi kwamba hatogombea mwaka 2010 katika Jimbo la Mtera, na sio tu kugombea Mzee Malecela alifika mbali zaidi kwa kunibariki kwamba nitakuwa mbunge wa Mtera ninayemfuata yeye.

"Lakini amebadilika na kwenda kinyume na maneno pamoja na ahadi zake. Tayari ametangaza nia yake ya kugombea tena katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu," alisema

Lusinde ambaye pia amewahi kuwa katibu wa CCM Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma alisema katika mwaka 2005, ilipofika wakati wa mchakato wa kuteuliwa na CCM kwa ajili ya kugombea Ubunge, Malecela alimuomba ajiondoe katika kinyanganyiro hicho na akakubali kutokana makubaliano maalumu waliyowekeana mbele ya mashahidi.

"Keneth Salali ni mmoja wa mashahidi walikuwepo wakati mzee Malecela aliponiomba nijiondoe katika kinyanganyiro cha kuteuliwa na chama na aliniahidi kuwa mwaka 2010 hatogombea tena.

"Namsihi Mzee Malecela aache mara moja mpango wake wa kugombea ubunge Jimbo la Mtera,"alisema Lusinde

Hata hivyo, Lusinde hakuwa tayari kuyataja majina ya watu ambao anadai kuwa wamemgeuza Malecela kama taasisi ya Deci kwa kupanda na kumvuna.

Lakini alisema watu hao ni wanachama wa CCM na mmoja wao aliwahi kuwa mlinzi wa Malecela kabla hajaumia.

"Hawa watu kumi waliomgeuza Malecela kama DECI wapo kwa maslahi yao binafsi na muda ukifika kila mmoja nitawataja," alisema.

Gazeti hili lilipomtafuta Malecela, liliambiwa kuwa yupo nchini Uingereza kwa kushughuli za kichama.


Source: Gazeti la Mwananchi

My Take:

Naona kazi imeanza sasa Mtera,huyu kijana(Lusinde) ni mwanasiasa machachari hasa,nakumbuka mwaka 2005 alimuumiza kichwa sana mzee Malecela kiasi kwamba wakafikia makubaliano kwamba asubiri mwaka huu wa 2010,kijana alikubali hasa baada ya kupewa kazi ya kuwa Katibu msaidiz wa CCM wa wilaya ya Kongwa-Dodoma(Ikumbukwe kwamba kabla ya hapo alikuwa ni mwanachama wa TLP kama sikosei na mwakahuo wa 2005 alitaka kugombea kwa tiketi ya TLP na alikuwa tishio kiasi kwamba mzee Malecela hakuwa na la kufanya zaidi ya kumuomba ajitoe na pia kumshawishi ajiunge na CCM kisha akapewa nafasi hiyo ya Katibu msaidizi wa CCM(W).

Binafsi Lusinde ni mtu wangu wa karibu sana na ni mwanasiasa mzuri hasa(CCM wanamtumia sana kwenye kampeni zao),wakati wa uchaguzi mdogo wa jimbo la Tunduru Lusinde alitumika ipasavyo katika kampeni kiasi cha kupelekea mgombea wa CCM ndugu Mtutula kushinda,baada ya hapo Lusinde alipandishwa cheo na kuwa Katibu wa CCM wa wilaya ya Tunduru,kisha baadaye akahamishiwa Tarime aliko sasa...Kijana ana kipaji hasa kwenye siasa za kuongea/kujieleza...Mzee Malecela inabidi ajizatiti hasa kama kweli kaamua kugombea maana Lusinde anawezambwaga(endapo hakutatokea mizengwe ndani ya CCM

Pia kuna jamaa mwingine anaitwa Laurent Hoya(mmiliki wa mabasi ya Mshikamano na mabucha ya kisasa ya Mshikamano),huyu naye anakubalika sana Mtera na Mvumi,naye nasikia ana mpango wa kugombea ubunge wa Mtera na juzjuzi tu hapa kapewa Ukamanda wa vijana wilaya ya Chamwino...Kazi ipo Mtera mwaka huu,tusubiri na tuone
Mkuu wangu balantanda... muzee wa yanga na asenali!!

Binafsi napenda kuona wakongwe wanapata challenge toka kwa rookies...

Ninasapoti yeyote anayekuja na jipya kwani hii "status quo" ndiyo inayotuhenyesha watanzania... labda niseme yafuatayo;

  • kule kondoa kaskazini naskia nyang'anyi anataka kurudi, sijui amesahau nini kule maana hata vile vivuko feki vya kuua watu alileta yeye
  • natamani na bariadi aje mwingine
  • Nasubiri wa mkuranga janguo aishie
  • tina wengi including mtulia, etc
sadly, hata huyo dogo ataambiwa asubiri tena
 
Mkuu wangu balantanda... muzee wa yanga na asenali!!

Binafsi napenda kuona wakongwe wanapata challenge toka kwa rookies...


Ninasapoti yeyote anayekuja na jipya kwani hii "status quo" ndiyo inayotuhenyesha watanzania... labda niseme yafuatayo;

  • kule kondoa kaskazini naskia nyang'anyi anataka kurudi, sijui amesahau nini kule maana hata vile vivuko feki vya kuua watu alileta yeye
  • natamani na bariadi aje mwingine
  • Nasubiri wa mkuranga janguo aishie
  • tina wengi including mtulia, etc
sadly, hata huyo dogo ataambiwa asubiri tena

- Saafi sana tupo pamoja sana hapo mkuu kwa mara ya kwanza!


Es!
 
Mkuu wangu balantanda... muzee wa yanga na asenali!!

Binafsi napenda kuona wakongwe wanapata challenge toka kwa rookies...

Ninasapoti yeyote anayekuja na jipya kwani hii "status quo" ndiyo inayotuhenyesha watanzania... labda niseme yafuatayo;

  • kule kondoa kaskazini naskia nyang'anyi anataka kurudi, sijui amesahau nini kule maana hata vile vivuko feki vya kuua watu alileta yeye
  • natamani na bariadi aje mwingine
  • Nasubiri wa mkuranga janguo aishie
  • tina wengi including mtulia, etc
sadly, hata huyo dogo ataambiwa asubiri tena

Umepotea sana mtani...Jana umewaona vijana lakini???...Back to the point;

Mkuu ni vigumu mnoo kuwa na Bunge lenye vijana watupu,si vibaya wakawepo wazee wawili watatu(wenye uwezo) wa kuwaongoza hawa vijana(huu ni mtizamo tu)...Halafu kila mtu ana haki ya kugombea mradi tu ametimiza sifa zinazotakiwa....Ni busara tu za mhusika ndio zitapelekea aisgombee na si maneno ya watu(kumlazimisha)....Ukubwa dawa ati

 
Umepotea sana mtani...Jana umewaona vijana lakini???...Back to the point;

Mkuu ni vigumu mnoo kuwa na Bunge lenye vijana watupu,si vibaya wakawepo wazee wawili watatu(wenye uwezo) wa kuwaongoza hawa vijana(huu ni mtizamo tu)...Halafu kila mtu ana haki ya kugombea mradi tu ametimiza sifa zinazotakiwa....Ni busara tu za mhusika ndio zitapelekea aisgombee na si maneno ya watu(kumlazimisha)....Ukubwa dawa ati

Naugulia timu yangu iko ICU kwa mara ya pili in 4 months, sijui ni kansa au HIV!!!

eniwei mkuu, i am in full support kwenye democracy and there is no way i will support someone simply because he/she is young especially after seeing the likes of ngeleja and malima on board!!... my youth/new faces preference iko kwenye baadhi ya majimbo na dio maana sikugusa mwandosya, ndesamburo etc

pia naamini kijana kuonyesha interest ni demokrasia, ila sijui kama itakua long lasting or what!!!

i cae for tanzania kuliko chama chochote kile
 

- Saafi sana tupo pamoja sana hapo mkuu kwa mara ya kwanza!


Es!
aaah mkuu, mara nyingi tu tuko pamoja ila lugha yangu ndio kidogo ya kifyomi kuliko ya kiswahili mkuu

there are gurus we need to brush-up young people, and it has proven that they are always more important than we think!!!

Lets see how things will turn out...
 
aaah mkuu, mara nyingi tu tuko pamoja ila lugha yangu ndio kidogo ya kifyomi kuliko ya kiswahili mkuu

there are gurus we need to brush-up young people, and it has proven that they are always more important than we think!!!

Lets see how things will turn out...

- Huyu kijana Lusinde anasumbuliwa na Shillingi Millioni 50 alizopewa na Makamba ambaye ametumwa na Lowassa, Rostam, na Chenge, ndio maana nilisema hivi huu mjadala ni bure maana hauna masilahi yoyote kwa taifa, huyu kijana ni melvi flani hivi hawezi kutusadia Mtera!

- Wamewapa hizo hela yeye na kituko mwingine anaitwa Anna Claudia ili aende agombee Same, Bwa1 ha! ha! Makambaaa aaaggggjhhhhrrrr!


FMEs!

 
- Huyu kijana Lusinde anasumbuliwa na Shillingi Millioni 50 alizopewa na Makamba ambaye ametumwa na Lowassa, Rostam, na Chenge, ndio maana nilisema hivi huu mjadala ni bure maana hauna masilahi yoyote kwa taifa, huyu kijana ni melvi flani hivi hawezi kutusadia Mtera!

- Wamewapa hizo hela yeye na kituko mwingine anaitwa Anna Claudia ili aende agombee Same, Bwa1 ha! ha! Makambaaa aaaggggjhhhhrrrr!

FMEs!

FMEs,nakushauri uwe unachagua sana maneno ya kuandika hasa kwa sababu wewe ni mtu wa karibu wa Mzee Malecela;watu wanaweza tafsiri maneno yako na kuya-link kuwa yamepata baraka za Mzee Malecela za kumuhusisha Katibu mkuu wa CCM na rushwa!

Kwa nini akina ALwaungane na Mzee Makamba kumuondoa Mzee Malecela Mtera?Tufafanulie tafadhali!
 
FMEs,nakushauri uwe unachagua sana maneno ya kuandika hasa kwa sababu wewe ni mtu wa karibu wa Mzee Malecela;watu wanaweza tafsiri maneno yako na kuya-link kuwa yamepata baraka za Mzee Malecela za kumuhusisha Katibu mkuu wa CCM na rushwa!

Kwa nini akina ALwaungane na Mzee Makamba kumuondoa Mzee Malecela Mtera?Tufafanulie tafadhali!

........hivi hujammanya tu!!.........anamuondoa Mzee kwenye "kundi" kiaina............hii inaitwa FUNIKA KOMBE (by whatever means possible)...................if you know what i mean............some of the things vinaongelewa hapa viliwa-cost watu huko nyuma............
 
- Malecela is doing great na atashinda tena ubunge, aliumbwa na Mungu, Mwinyi alimuomba toka Commonwealth hakuwa jobless, never! pamoja na minjama yote ile, tizama tena historia, mnakuwa na chuki mno hata ukweli hamuuoni, he is just doing fine mkuu dua la kuku unajua halimpati mwewe!

Es!
Alimwomba toka Commonwealth? Nakumbuka alikuwa jobless baada kutoka kule kwenye U-eminence, akapewa U-RC kule Iringa, akapelekwa London kuwa HC wetu. Kisha akaangushiwa U-WM na Makamu wa Rais( Mtu pekee kuteuliwa hivo bila kuwa na Jimbo!).

Hii ikasababisha Bunge kupitisha kipengele kwenye KATIBA yetu kinachotaka anayeteuliwa kuwa WM ni lazima awe Mbunge wa Jimbo. Unapojaribu kuiandika upya historia ya mzee wetu huyu unawakosea Watanzania waliomwamini na kumpa nafasi hizi nyeti katika Taifa.
 
Alimwomba toka Commonwealth? Nakumbuka alikuwa jobless baada kutoka kule kwenye U-eminence, akapewa U-RC kule Iringa, akapelekwa London kuwa HC wetu. Kisha akaangushiwa U-WM na Makamu wa Rais( Mtu pekee kuteuliwa hivo bila kuwa na Jimbo!).

Hii ikasababisha Bunge kupitisha kipengele kwenye KATIBA yetu kinachotaka anayeteuliwa kuwa WM ni lazima awe Mbunge wa Jimbo. Unapojaribu kuiandika upya historia ya mzee wetu huyu unawakosea Watanzania waliomwamini na kumpa nafasi hizi nyeti katika Taifa.

- Hujui histioria mkuu, Mwinyi alimuomba kutoka Jumuiya ya madola ili akasimamie kudai haki yetu katika EAC na madeni yake kule Canada kabla ya Iringa, na ilikuwa baada ya kushauriwa na World Bank kwamba ni Malecela peke yake ndiye anayeweza ku-deal na hiyo ishu, Wildcard mbona unataka kujivua nguo na historia usiyoijua, uliza kwanza kabla hujakurupuka, mzee hajawahi kuwa jobless never! no facts or research no rights to speak!

- Pole sana mkuu historia haindikwi na watu wanaowatwala wengine kwa mabavu, inaandikwa sasa maaana tuko huru! Historia ya Hitler inaandikwa sasa na ndio maana hata movies zake zinachezwa sasa, watu wakiwa huru!

Respect.


FMEs!
 
FMEs,nakushauri uwe unachagua sana maneno ya kuandika hasa kwa sababu wewe ni mtu wa karibu wa Mzee Malecela;watu wanaweza tafsiri maneno yako na kuya-link kuwa yamepata baraka za Mzee Malecela za kumuhusisha Katibu mkuu wa CCM na rushwa!

Kwa nini akina ALwaungane na Mzee Makamba kumuondoa Mzee Malecela Mtera?Tufafanulie tafadhali!

- Malafyale acha uzushi, mimi sina anything to do na Malecela, Malecela hana mtoto anayeitwa FMES mimi ni mzuka tu wa sauti ya umeme, sasa it is up to you ukitaka kuni-link naye hayo ni yako ila unachojaribu kukifanya ni kukiuka sheria za JF yaani una-speculate, acha hizo mkuu niko karibu na viongozi wengi wa CCM na wa upinzani, lakini sijawahi kumuongelea anybody na besdies FMES hana baba wala mama ni just FMEs sauti ya umeme!

Respect.


FMEs!
 
Back
Top Bottom