MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,009
- 2,173
Kwa wale wahenga watanielewa. Kwamba kuna watu walistahili wapotee kabisa ktk siasa za TZ kutokana na tabia zao na hata tuhuma walizonazo. Mmojawapo ni huyu Nchimbi.
Akiwa Umoja wa Vijana, alikuwa mtu hovyo.
Akawa Mkuu wa wilaya akapoa kidogo maana wilaya yenyewe, Bunda, siyo ya mzaha
Akawa waziri wa mambo ya Ndani akawa mtu hovyo! Akina Mwangosi wakauwawa!
Huko umoja wa vijana kuna mengi sana ambayo hata haistahili kuyazungumzia, lakini alikuwa na watu wema sana ambao walistahili kuisaidia nchi hii kuliko yeye. Kama kweli Nchimbi anastahili kuwa Katibu wa chama kama CCM, leo nimemkumbuka Ipyana Malecela ambaye hapa JF aliwahi kuandikiwa kumbukumbu yake. TUMKUMBUKE IPyana aliyekuwa naye UVCCM.
Akiwa Umoja wa Vijana, alikuwa mtu hovyo.
Akawa Mkuu wa wilaya akapoa kidogo maana wilaya yenyewe, Bunda, siyo ya mzaha
Akawa waziri wa mambo ya Ndani akawa mtu hovyo! Akina Mwangosi wakauwawa!
Huko umoja wa vijana kuna mengi sana ambayo hata haistahili kuyazungumzia, lakini alikuwa na watu wema sana ambao walistahili kuisaidia nchi hii kuliko yeye. Kama kweli Nchimbi anastahili kuwa Katibu wa chama kama CCM, leo nimemkumbuka Ipyana Malecela ambaye hapa JF aliwahi kuandikiwa kumbukumbu yake. TUMKUMBUKE IPyana aliyekuwa naye UVCCM.
Ipyana Malecela (10 years on) - RIP
Katika maisha ya Binadamu hakuna jambo linalouma kama mzazi kumzika mwanae, lakini inauma zaidi hasa mwanae anapokuwa ni mtu wa watu na mtu mwema. Vijana wengi wa JF mtakuwa hamumjiui huyu lakini 10 years ishapita tangu Brother Ipyana Malecela atutoke na bado nakumbuka vividly siku ile...
www.jamiiforums.com