Kimilidzo
JF-Expert Member
- Jan 3, 2011
- 1,346
- 627
Kusema kweli hii ya Dowans ni kama sinema, kwasababu mambo yanabadilika na hayatabiriki.
Ebu tujikumbushe kidogo matukio juu ya Dowans:
Jamani Tanzania hii, kila kitu kinawezekana!
- Dowans anaingia kwa mkwara na kuchukua nafasi ya Richmond
- Kamati ya Mwakwembe inashauri mkataba wao uvunjwe kwasababu ni batili
- Tanesco anavunja makataba
- Dowans anakimbilia mahakama ya usuluhishi na kushinda kesi
- Wananchi wanahoji nani mmiliki wa Dowans, Ngeleja anawataja wamiliki
- Baadaye Rais anasema yeye hawajui wamiliki
- Wabunge wa ccm wanasema wataongea nao deni lipungue
- January Makamba anaandika barua kwa Waziri
- January anapendekeza mitambo iwashwe kwa mkataba wa dhalura
- Brugedia Gen. anajitokeza na kusema mmiliki lakini asipigwe picha
- Kesho yake mitambo inawashwa kidogo
- January Makamba anakuwa msemaji wa Dowans, Tanesco, Wizara na Kamati ya Bunge
- Dowans anaanza kumnyemelea Tanesco na kumwambia atamfutia deni lake!
- ........
- .........
- Ongeza mengine...!
Maoni yangu:
Kikwete asipokuwa makini awamu zake za utawala zitakuwa defined na hii kitu inayoitwa Richmond/Dowans
Hii filamu ya Dowans ni kali sana. Imefunika zote, hadi ile filamu ya Gongolamboto imefunikwa na kumuacha Hussein Mwinyi anakula kuku tu no presha tena.