PostGE2025 Kihongosi: Jaji Warioba asiwe na chuki kwa viongozi waliopo, tunakuheshimu, staafu vizuri

PostGE2025 Kihongosi: Jaji Warioba asiwe na chuki kwa viongozi waliopo, tunakuheshimu, staafu vizuri

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Katibu Mwenezi wa CCM, Kenani Kihongosi amemwomba Jaji Mstaafu, Joseph Warioba asiwe na chuki kwa viongozi waliopo bali awashauri kwa hekima badala ya kulalamika mtandaoni.

Akizungumza na wanahabari jijini Dodoma siku ya Jumamosi, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Kenani Kihongosi ameeleza kusikitishwa na hatua ya Jaji Warioba kutoa kauli ambazo chama hicho kinaziona kama zenye chuki na ulalamishi, siku chache tu baada ya kukutana na Rais Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa.

“Warioba amekutana na Rais siku nne hazijapita yupo tena mtandaoni. Sasa inasikitisha kidogo lakini tunachomuomba kwamba astaafu vizuri aendelee kupumzika lakini asiwe na chuki kwa viongozi waliopo kwa sababu ana uwezo wa kushauri na kufika katika mamlaka husika na kuweza kuishauri kwa hekima kuliko kwenda kulalamika kwenye mitandao”, amesema Kihongosi.


 
Machawa ya kijani kwao kila kitu ni kutetea tu ili mradi mkono uende kinywani!
 
CCM YA WATANZANIA WOTE. Acha ujinga dogo. Nitoe kwenye hao watanzania wa ccm.
Tatizo ni kwamba nyinyi ndio mnaotumiwa sasa kama kinga ya hao hao waovu. Wanafanya maovu, halafu wanageuka na kujifanya wao na nyinyi ni wamoja ndani ya CCM.

Na kama wewe ni CCM ukinyanyua mdomo kama alivyofanya Polepole, unajuwa nini kitakupata.

Kiufupi, wakati huu kujitambulisha kuwa wewe ni mtu wa CCM ni karaha tupu kwa waTanzania.
 
Katibu Mwenezi wa CCM, Kenani Kihongosi amemwomba Jaji Mstaafu, Joseph Warioba asiwe na chuki kwa viongozi waliopo bali awashauri kwa hekima badala ya kulalamika mtandaoni.

Akizungumza na wanahabari jijini Dodoma siku ya Jumamosi, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Kenani Kihongosi ameeleza kusikitishwa na hatua ya Jaji Warioba kutoa kauli ambazo chama hicho kinaziona kama zenye chuki na ulalamishi, siku chache tu baada ya kukutana na Rais Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa.

“Warioba amekutana na Rais siku nne hazijapita yupo tena mtandaoni. Sasa inasikitisha kidogo lakini tunachomuomba kwamba astaafu vizuri aendelee kupumzika lakini asiwe na chuki kwa viongozi waliopo kwa sababu ana uwezo wa kushauri na kufika katika mamlaka husika na kuweza kuishauri kwa hekima kuliko kwenda kulalamika kwenye mitandao”, amesema Kihongosi.

mzee warioba amekasirishwa mno kutokuteuliwa kua mjumbe wa tume ya kimahakama ya uchunguzi.

ana hasira mno kwenye hilo,
mzee na uchu na hela balaa, halafu anavuta sana sigara :HAhaa:
 
Katibu Mwenezi wa CCM, Kenani Kihongosi amemwomba Jaji Mstaafu, Joseph Warioba asiwe na chuki kwa viongozi waliopo bali awashauri kwa hekima badala ya kulalamika mtandaoni.

Akizungumza na wanahabari jijini Dodoma siku ya Jumamosi, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Kenani Kihongosi ameeleza kusikitishwa na hatua ya Jaji Warioba kutoa kauli ambazo chama hicho kinaziona kama zenye chuki na ulalamishi, siku chache tu baada ya kukutana na Rais Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa.

“Warioba amekutana na Rais siku nne hazijapita yupo tena mtandaoni. Sasa inasikitisha kidogo lakini tunachomuomba kwamba astaafu vizuri aendelee kupumzika lakini asiwe na chuki kwa viongozi waliopo kwa sababu ana uwezo wa kushauri na kufika katika mamlaka husika na kuweza kuishauri kwa hekima kuliko kwenda kulalamika kwenye mitandao”, amesema Kihongosi.

Big WRONG move

CCM ni magaidi na hawaogopi kufanya unyama

Kihongpsi keshatapika shombo
 
Back
Top Bottom