Kigwangalla aitwa na kamati ya maadili na maandamano yake kusitishwa na CCM, yeye asisitiza yapo!!

Ana bahati uciku huu natumia cimu hapa.. Ningeperuzi na kupata post yake moja ambayo alikuwa akitetea kwa nini hakutia saini kwenye kumuwajibisha PM.. Yaani jamaa ni mnafiki pitiliza huyu..
 
Daktari mjinga huyu si ndiye alisema serikali lazima ifurahie wao waccm kuwa bungeni na hawawezi kuiangusha? hii double standard anaitoa wapi??
 
Bwana Kingwa umejitahidi kujibu kwa kujiamini, safi sana. Hatutaki mtu ambaye anakimbia hoja kama wale wenzio
 
Mkuu Chikatata, kuna mambo mawili hapo,
1. Maandamano
2. Mkutano wa hadhara.

1.Kwa vile Dr. Kigwa ni mbunge kupitia CCM, jambo lolote atakalofanya jimboni kwake lazima kipate baraka za chama chake. Maadam CCM haijatoa baraka kwa maadamano yale, then maandamamo hayatakuwepo!. Hata kama umechat na Dr kule fb akakuhakikishia maandamano yapo, amekudanganya na kujidanganya!.

2. Kama ni kweli amekuambia kuwa "chama hakina sababu ya kumzuia na wala hakina uwezo huo" pia atakuwa amekudanganya na kujidanya kwa sababu tayari chama kimeshamzuia na sababu za kumzuia kimezitoa ila ni kweli chama hakina uwezo wa kumzuia, ila chama kimewaandikia jeshi la polisi ambao ndio wenye uwezo wa kumzuia na watatumia uwezo huo kuyazuia maandamano yake, hivyo hayatakuwepo!.

3. Hilo la kusema kwamba katibu wa ccm wilayani pale amekurupuka kuandika barua ile pia amekudanganya wewe, japo ni kweli barua ile haina nguvu yoyote kisheria, ila imeandikwa kufuatia vikao halali vya ccm wilaya ambavyo Dr. Kigwa ni mjumbe halali wa vikao hivyo!, vinginevyo aseme huyo katibu amejiandikia tuu na vikao hivyo havikuwepo wala havikujadili kuhusu maandamano yake!.

4. Hata hivyo naomba nikiri wazi Dr. Kigwa ameonyesha ujasiri mkubwa wa kuwatumikia wananchi wake bila kujali chama chake kinataka nini, mgombea ubunge huwa ni mgombea wa chama na anawajibika kwa chama, lakini akishachaguliwa kuwa mbunge ni mtumishi wa wananchi na anawajibika kwa wananchi na sio kwa chama tena, hivyo anachokifanya Dr. Kigwa ndicho sahihi kabisa kinavhopaswa kufanywa na wabunge wote wa kuchaguliwa kwa kuweka mbele maslahi ya wananchi na sio ya chama!.

5. Kwa mkutano huu, naomba nikiri wazi kuwa Dr. Kigwa anajiunga na timu ya kina Deo Filikunjombe kusimama kuhesabiwa na 2015 ataendelea kuwa mbunge wa Nzega kwa sababu ameweza kuona mbali!. Bashe ndie aliyekuwa kipenzi cha wana Nzega, baada ya kupigwa zengwe, na baadaye kusafishwa, Dr. Kigwa ameshaona picha ya 2015 na kujua there is no way CCM itamsimamisha kwa sababu kipenzi chao Bashe ameshakuwa cleared, hivyo dawa pekee ya kusurvive ni kuachana na CCM na kuivest kwenye wananchi ndio maana barua yake ya maandalizi ya mkutano hakuipitishia CCM I doubt kama hata vikao vya CCM wilaya anahudhuria!.

Wabunge wenye akili ni wale wanaojua kutazama mbali, 2015 jahazi la CCM linazama, wabunge wa CCM ambao wanaitegemea CCM kuwaokoa, watazama nayo, na wale wenye akili, wana invest on people na ndio watakao waokoa kiukweli, not CCM anymore!.

Wish you all the best Dr. Kigwa!.

Pasco.

Kama ni kweli anatetea maslahi ya wananchi na sio chama, mbona kwenye hoja ya kamati ya Mh. Zitto ya kumwondoa waziri mkuu hakuweka saini na badala yake aliangalia maslahi ya chama na sio ya wananchi. Huyu ni mchumia Tumbo tu hana lolote. Akina Filikunjombe angalau walionyesha msimamo wa kutetea maslahi ya nchi na wananchi wake.

Hiyo ni janja ya nyani kula hindi bichi
 
Mimi nina ishu tofauti kabisa na mada ya thread hii, ila inatokana na thread yenyewe.

(1) Hivi katibu wa CCM wa wilaya ana mamlaka gani ya kutoa amri kwa mbunge aliyechaguliwa na wananchi? Swala la kuunganisha mbunge na chama ni jambo linalohitaji kuangaliwa sana kwenye katiba mpya. Mbunge anachaguliwa na wananchi na anatakiwa awe ni above chama chake, kwa sababu wananchi ndani ya wilaya yake siyo wanachama wa chama chake tu.

(2) Halafu katibu huyo ana elimu gani? Angalia muundo wa sentensi zake kwenye barua amabayo ni official communication ya ofisi yake.
....


Tafadhari husika na somo hilo hapo juu.

...

Barua hiyo iliyosainiwa na wewe mwenyewe ambayo inaelezea kwa kina lengo na madhumuni ya wewe kuhitaji mkutano wa hadhara na maandamano ya Amani kwa ajili ya kujaribu kuielezea hoja yako kwa wananchi unaowawakilisha Bungeni juu ya uwepo wa Mgodi wa dhahabu wa RESOLUTE TANZANIA LIMITED na dhuluma waliyofanyiwa wananchi wa maeneo hayo kwa mujibu wa barua yako hiyo, mara baada ya wewe kuwasilisha hoja binafsi zaidi ya mara tano kwa Spika wa Bunge na haikupata nafasi ya kusikilizwa.


...

Hiyo ni sentensi moja yenye comma moja na full stop moja tu. Comma yenyewe iko misplaced! Kuna maneno yaliyokuwa capitalized bila sababu ya kueleweka. Huyu mtu ana elimu gani? Atakuwaje katibu ilihali hajui kuandika? Anaandika kama anaongea kwa kusutana na mheshimiwa mbunge. Kuna tofauti sana baina ya mawasiliano ya mdomo (oral) na mawasiliano ya kimaandishi (written). Nilitegemea maafisa mbalimbali katika jamii yetu wawe wanajua mawasiliano mazuri kwa vile sehemu ya mawasiliano yao huweza kutumika pia kama mafunzo kwa watoto ambao bado wako shuleni.
 
sasa nakala kwa mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya za nini wakati kila siku watu wanalalamika kuwa hawa viongozi wa wilaya na mikoa hawapaswi kufanya kazi za chama bali kazi za wananchi wote?
 
Hiyo tarehe 16/6/2012, mbona IMESHAPITA? Tena, CCM wanasemaga Maandamano hayajengi? Sasa ndo wanaona Umuhimu wake?
 
Back
Top Bottom