Kigwangalla adai mkataba wa mgodi anajitakia mema kweli?

Kuna mambo mengi sana kuhusiana na huu mgodi wa Golden Pride ambayo wapiga kura wa Nzega wamekuwa wakiyalalamikia kwa zaidi ya miaka kumi na tatu sasa, na haya mambo yanajulikana kila ngazi ya watendaji wa serikali na hakuna jitihada za kuyatatua...mimi Muwakilishi wao nimeamua kuyafuatilia na kwa hakika sintowaangusha wanaNzega wenzangu...nitayafuatilia mpaka pale nitakapoona yanatatuliwa la sivyo hapatatosha Bungeni!

Hivi juzi, baada ya utafiti wa muda mrefu, nimekabidhi kwa Katibu wa Bunge kusudio la kuliomba Bunge lipitishe azimio la kuufunga mgodi huo kwa kuwa hauna manufaa kwa Taifa, pamoja na mambo mengine mengi!

Kuleta mapinduzi ya kifikra siyo lazima uwe upinzani; wengine tunaamini katika kuleta mabadiliko 'from within the system' na there is plenty you are yet to see from people like me...naanza na hili na kuna mengi yapo njiani! Na siyo lazima kila mtu mwenye fikra mbadala basi ajiunge na CHADEMA...

Stay put,
HK.

kama Mwalimu alivyosema kuwa upinzani wa kweli ni lazima utokee ndani ya CCM. Nami naamini huenda ipo siku baadhi ya wana CCM wataona na kuyakataa maovu haya ambayo yanatia aibu taifa letu.

Tatizo kubwa ambalo watanzania tunalo ni kukosa moyo wa uzalendo, utaifa na mawazo ya kujenga future ya nchi kama Tanzania. Kama tungekuwa na moyo huu si rahisi kuingiza nchi mikataba ya kuua kabisa nchi.
mapinduziiii daimaaaaaa:clap2:
 
Hili ndilo tatizo tulilonalo baadhi ya wana jf,mda mwingi hatuamini kile kinachofanywa na baadhi ya wanaccm,umefika wakati wa kuweka ushabiki nyuma na kuwapa moyo wale wanaojaribu kudiliki kufanya jambo fulani,najuwa ukitakacho mkuu,unahitaji tumtukane MBUNGE na tusimpe moyo wala kumpa nguvu kwa kile alichokianzisha kwa kuwa ni mbunge wa ccm nasema NO kwa hili

hata kama huikubali kambi usinyeeeee mlangoni ipo siku utapita ktk huo mlango

mimi ninatabia tofauti kidogo na wewe mkuu,huwa napenda kumpa mtu moyo na nguvu kwa udiliki wake kwani naelewa ktk ccm ni vigumu sana hata kuanza kuongelea kile ambacho kinawagusa wakubwa,lakini Dr kajaribu mpe sifa yake usiwe ni mtu wa FIKRA MGANDO mda wote hata kwa yale mema wafanyayo wengine hususani wale wasio ktk bega lako la kulia

KWA MTINDOOOOO HUUUU HATUTAFIKA,HATA CDM IKIWA MADARAKANI,KWANI NI VIGUMU SANA KUWARIDHISHA WATU WA KADA YAKO


mapinduziiiiii daimaaaa:clap2::first:
watu kweli wepesi wakisikia mh utetemeka mnajua huyo mbunge kaingiaje hapo? je unajua CCM kuna makundi?na unajua huo mgodi unanufaisha kundi lipi? na yeye anawakilisha kundi gani? eng vipi? mbona mhandisi unashindwa ku brainstorm?sasa hivi nikwambie CCM nikuviziana tu kwa kisingizio cha wananchi.hivi Nzega kuna umeme kama Segerea?
 
@Samora10, hawa jamaa wamekuwa na historia ya kurefusha kitu wanachokiita 'mine life' na wamekuwa wakisema kila siku kwamba mgodi utafungwa soon...maybe baada ya miaka miwili...na ikikaribia kufika wanasogeza mbele...kila siku wanafanya utafiti na kugundua mahala kwenye dhahabu nyingi zaidi ya pale pa jana, na mwaka 2006 waliongeza kiwango cha uzalishaji per day ili wavune ndani ya muda mfupi zaidi...hivi ni kweli 6 years later wanaweza kuwa tayari kufunga mgodi?

Hata hivyo hoja yangu ina options nyingi, moja kubwa ikiwa kuwataka wa-renegotiate mkataba na serikali yetu, watupe share/waongeze mrahaba na walipe kodi ipasavyo...maana katika miaka yote hiyo zaidi ya 13 wameanza kulipa kodi (corporate tax) mwaka 2009............(toka mgodi huo ufunguliwe mwaka 1999!!!!!!!!!!!!) - WAKIMAANISHA NDIPO WALIPOANZA KUTENGENEZA FAIDA KWENYE BIASHARA YAO!

Mheshimiwa nakupongeza kwa kuthubutu!
Wasiwasi wangu ni support kiasi gani unapata toka kwa viongozi wenzako jimboni maana naona wanaongea lugha tofauti ama kwa upeo mdogo au ndo washashikishwa bahasha!...
 
watu kweli wepesi wakisikia mh utetemeka mnajua huyo mbunge kaingiaje hapo? je unajua CCM kuna makundi?na unajua huo mgodi unanufaisha kundi lipi? na yeye anawakilisha kundi gani? eng vipi? mbona mhandisi unashindwa ku brainstorm?sasa hivi nikwambie CCM nikuviziana tu kwa kisingizio cha wananchi.hivi Nzega kuna umeme kama Segerea?
Nachokiongelea hapa ni udiliki wake wa kusema jambo,siangalii kama nae ni mnufaika ama vipi ama pia siwezi elewa yeye yupo ktk kundi gani,nacho kisema juu ya Dr ni kuweza kudhubutu kusema jambo ambalo baadhi ya wadau wa ccm waitwao vigogo wameshilikia mrija wa maziwa na kuuelekeza mdomoni mwao na Dr anataka kuukata mrija huo,so kwanini nisimpe pongezi kwa hilo?

mdao kila mala ukiwa na shaka ya kuchukuliwa mke ipo siku utachukuliwa kweli kwani yawezekana umesaidia kutoa mbinu ya mke wako kuchukuliwa so lets be realistic mpe kaisali yake na mungu mpe yake

Tuzidi kumpa moja Dr ili aweze kuikombowa nzega

mapinduziiiii daimaaaaaaaa:popcorn::sick:
 
Naomba nimpongeze rafiki yangu Kigwangalla kwa ujasiri wake wa kuwasilisha hoja binafsi bungeni akitaka serikali ipatiwe angalau 20% ya hisa ya kila mgodi.

Tunajua ni hoja nguvu kutekeleza lakini pia tunajua inawezekana, nampongeza pia kwa kuomba migodi iendeleze maeneo ya migodi yao ili yafanane na utajiri yanaouzunguka.

Naomba nikutakie kila la kheri na bila shaka utaungwa mkono na wabunge wengine katika kuandika historia mpya ya uwekezaji Tanzania, badala ya kuwa shamba la bibi sasa na sisi kama taifa tutanufaika na faida inayopatikana kutokana na biashara ya migodi.

Source: Mbunge awasha moto mwingine bungeni
 
Hoja yake ikoje kisheria? anacho-demand kinaezekana under current situation, maana kupiga mayowe per se is not an issue.
 
Simple. Anachodai hakiwezekani kwani hakipo ndani ya mikatba ya sasa (''under current situation'' , kama ulivyouliza)

Hivyo ndivyo Mkwere alivyowadanganya, mbona nchi nyingine wanafanya bila kujali mikataba iliyopo. BTW, mikataba yenyewe ni mirefu zaidi ya miaka 20 kipindi hicho kikifika yatabaki mashimo tu wenyewe watakuwa walishajiondokea...

Angalia nchi kama Zambia, Guinea, Ghana, Zimbabwe, Venezuela wame/wanabadilisha sheria ili rasilimali zao ziwanufaishe zaidi bila kujali kama mikataba ya awali ime-expire au la....
 
naitaji kama mwaka kumpima huyu jamaa manake nimjuavyo si mtu wa ujasiri huo.labda ameshaongea na spika kuwa nitatangaza kuleta hoja ila naomba mwishowe uikatae mheshimiwa.INAELEKEA MEMBA HAMUMJUI HUYU JAMAA KIUNDANI
 
Hii issue kisheria ni ngumu, nitafafanua ninachokijua:

Makosa makubwa ambayo serikali ya Tanzania imeyafanya kwenye sekta hii ya madini ni kutoa Prospecting Lisence (PLs) kwa asilimia 100 kwa mwekejazi, hao wawekezaji wakishamaliza utafiti na kama kuna mali wanapewa Special Mining Lisence (SMLs) nayo pia huwa ni 100% owned na mwekezaji na serikali imejiweke kwenye kundi la kuchukua kodi tu, hiyo ndio sheria tuliyojiwekea Watanzania, hizo 3 to 5% tunazopewa ni zawadi tu na ni makubaliano na wala sio sheria, ni mikataba mizito mno, chukulia kama ule wa Buzwagi, Karamagi kapanda ndege kwenda UK kumpelekea mwekezaji mkataba asaini.

Nchi zinazofaidika na madini eg Botswana, wao walikopi ile sysytem ya Nyerere kuwa madini yote ni mali nya serikali, sasa kama mwekezaji anakuja anapewa viwanja afanye utafiti na mali ikishapatoikana inakuwa 50-50, lakini mara nyingi serikali huwa inaconsider yafuatayo:

1) kwa sababu jamaa amefanya utafiti ambao una gharama ya mamilioni ya USD basi serikali inapunguza 50 yake na kuwa 40%
2) Serikali mara nyingi wanajitoa katika uendeshaji wa hiyo migodi, hivyo basi uendeshaji unabaki kwa mwekezaji na serikali anapunguza tena share zake to 30%

Kwa hiyo anapata 30% na anachukua kodi, Botswana haina rasilimali kama Tanzania lakini kidogo walichonacho kinawasaidia sana, na Tanzania kabla ya kuingia kwenye uwekezaji mkubwa wa madini kuna timu ya watu ilikwenda Botswana, Ghana na walikuja na riport nzuri tu, lakini walikuwa serikalini wakati ule (JK kama Waziri) baada ya kushughulikia ile ripoti wao wakaingiza siasa na ndipo tulipo sasa

NI KWA NGUVU TU NDIO TUTAWEZA LAKINI KIMKATABA TUMEJINYONGA WENYEWE.

BARRICK ANA MIGODI ZAIDI YA MINNE TANZANIA NA ANAIPATA KIURAHISI TU, LAKINI JUZIJUZI TU AMESHINDWA KUFUNGUA MGODI WA SEDIBERO SOUTH AFRICA KWA SABABU WAZAWA WALIKUWA WANATAKA 30% SHARE, BARRICK WAKAONA BORA WAJE HUKU KWENYE SHAMBA LA BIBI
 
Mkuu, madini ni yetu na uzuri tayari tumeshajua yako wapi! sasa kama watakataa ni bora waondoke halafu sisi twende mashariki ya mbali na kuwaleta ndugu zetu wa-China.

Mbona Mchuchuma na Liganga tumeweza kupata 50-50 deal...
 
nahisi atakuwa na influence, pamoja na kuwa alikuwa watatu katika kura za maoni, akapitishwa kugombea nafasi ya ubunge.
Kila la heri Dr. pigania nchi kaka
 
Hakuna kitu hapo. Kigwangala amepata wapi ujasiri wa kukata tawi alilokalia?! Huyu ni mtoto wa JK, RA na Makamba na ndiyo waliomuweka hapo alipo na mikataba ya madini ni ya haohao. Kaanzisha tu hiyo hoja ili atangazwe na vyombo vya habari angalau wananchi wajue kuwa yuko Kigwangalla.
 
Back
Top Bottom