KIgugumizi cha JK

Teeh!Teehee wacha huyo umeshawahi kumsikia yule mama aliepewa secta ya viwanda na biashara (maria naugua), acha kaka. Siku hiyo alijua anaongea na wahindi wanatengeneza vyuma balaa,sasa cjui ni ule moshi wa kiwanda ama, kuvunja mayai kazi jamani ila vitoto vya sasa hivi usicheze navyo utafikliri wapo kwa baba moi
 
Teeh!Teehee wacha huyo umeshawahi kumsikia yule mama aliepewa secta ya viwanda na biashara (maria naugua), acha kaka. Siku hiyo alijua anaongea na wahindi wanatengeneza vyuma balaa,sasa cjui ni ule moshi wa kiwanda ama, kuvunja mayai kazi jamani ila vitoto vya sasa hivi usicheze navyo utafikliri wapo kwa baba moi

Huyu??



 
Last edited by a moderator:
HATUCHEKANI kwenye LINGUA FRANCA BIN PIGIN NA CREOLE

...labda ilikuwa isomeke ".....as citizens...."!!Lakini lugha isiwe kigezo cha uongozi bora. Kieengereza ni lugha ya biashara duniani hivyo hicho anachojua kinamtosha.Swali ni kuhusu utendaji.Nchi imenufaika vipi na uongozi wake?Je, maisha yalivyokuwa wakati wa Mkapa na wengineo yameboreshwa ukifananisha na uongozi wake?Vigezo kama hivi ndivyo vya kuzungumza.

Ninaamini kuwa kiongozi yeyote duniani hapimwi kwa kuweka idea zake kinadharia BALI VITENDO au KUTEKELEZA hizo idea zake.Kuongea ni rahisi,kutekeleza ni ngumu!"Talk is cheap..."Ni kwa nini tunafanya mambo kwa kujaribu?Ni kwa nini tusiwe na vigezo ambavyo vitatujali sisi kama wananchi na siyo vigezo vya kupumbavu kama ..."Rais mwenye mvuto..."??Ndio anaweza kusema kuwa wananchi wameifanyia nini nchi yetu na siyo kumtegemea yeye LAKINI yeye si ndio kiongozi?Si ni yeye anachagua viongozi/mawaziri wabovu na wenye vyeti feki(allegedly)?Inakuwaje basi leo tufinge macho na kusahau kauli mbio ya uchaguzi uliopita,je huu ni ujinga wetu au umasikini unatufanya tuishi kwa matumaini?Inatia hasira kwamba kila siku tunaongea tu humu ndani na mabo yale yale yanazidi kuendelea kutendwa!Wakati wote huwa nasema ikifika wakati wa kubadilika, tubadilike!Sisi tuna uwezo ambao bado nadhani hatujauelewa.The power to elect someone is something that we should never undermine.
 
Jamani lakini hii ni kama National Issue. waTZ wengi ki-inglish ni issue, wachache sana wanaweza kuongea bila kukunja sura au kuwa wadogo. na wengi wa dizaini hiyo nadhani hawajakulia bongo. kwa sisi ambao ki-inglishi ni lugha ya 3 au 4 huwa inatupa tabu sana kuongea. tunajitahidi kuongea tu sababu wakati mwingine unakuwa umebanwa.
 
Lugha ni chombo muhimu sana katika mawasiliano. Viongozi wenye kujiamini kwamba lugha sio issue huwa wanakuwa na wakalimani ili kuwa huru katika kuwasilisha mada hata kama lugha hii ya kikoloni sio weupe. Kwa matatizo kama haya ni rahisi sana kuingia katika mikataba ya kina kinjekitile.

Na wazungu wengi wanaopata fursa ya kuingia mikataba mbalimbali hapa tanzania hutumia lugha ngumu sana za kisheria. Na watu wetu kwa kujitutumua huwa hawataki kuonyesha kwamba wameachwa bila kuelewa maneno fulani katika mkataba yana maana gani matokeo hu sign wasichokijua sawasawa na mwishowe mikataba mingi imetuletea madhara.

Nakumbuka mkataba wa kubinafsisha kampuni moja ya umma ulikuwa na maelekezo ya mkataba kama kurasa miatano hivi, waswahili waliingia kuusoma sidhani kama hata siku mbili zilifika, mkataba mkataba ukasainiwa. Leo hii watu wamerudi nyuma kama miaka ishirini hivi. Sababu ya kukumbatia lugha ambayo hatuifahamu sawasawa.

Tukubali yaishe kama tulivyoamua lugha ya taifa ni kiswahili. Shuleni sasa hivi tunao waalimu wa kiingereza ambao hawakufundishwa kiingereza kwa kuwa wakati wanasoma walimu wa kiingereza hawakuwapo, tutegemee nini katika hili? Naamini tusiishi kwa kutegemea miujiza na badala yake tuishi kwa kutegemea mipango ndio silaha pekee itakayo tuokoa.
 
Lugha ni chombo muhimu sana katika mawasiliano. Viongozi wenye kujiamini kwamba lugha sio issue huwa wanakuwa na wakalimani ili kuwa huru katika kuwasilisha mada hata kama lugha hii ya kikoloni sio weupe. Kwa matatizo kama haya ni rahisi sana kuingia katika mikataba ya kina kinjekitile.

Na wazungu wengi wanaopata fursa ya kuingia mikataba mbalimbali hapa tanzania hutumia lugha ngumu sana za kisheria. Na watu wetu kwa kujitutumua huwa hawataki kuonyesha kwamba wameachwa bila kuelewa maneno fulani katika mkataba yana maana gani matokeo hu sign wasichokijua sawasawa na mwishowe mikataba mingi imetuletea madhara.

Nakumbuka mkataba wa kubinafsisha kampuni moja ya umma ulikuwa na maelekezo ya mkataba kama kurasa miatano hivi, waswahili waliingia kuusoma sidhani kama hata siku mbili zilifika, mkataba mkataba ukasainiwa. Leo hii watu wamerudi nyuma kama miaka ishirini hivi. Sababu ya kukumbatia lugha ambayo hatuifahamu sawasawa.

Tukubali yaishe kama tulivyoamua lugha ya taifa ni kiswahili. Shuleni sasa hivi tunao waalimu wa kiingereza ambao hawakufundishwa kiingereza kwa kuwa wakati wanasoma walimu wa kiingereza hawakuwapo, tutegemee nini katika hili? Naamini tusiishi kwa kutegemea miujiza na badala yake tuishi kwa kutegemea mipango ndio silaha pekee itakayo tuokoa.

Mzee nakubalina nawe kabisa. Japo kuwa wengi wandai kuwa lugha si muhimu, lakini ndio msingi wa kujua na kupima uelewa wa mtu katika mambo. Lugha kama chombo cha Mawasiliano, inaweza kukufanya upate au ukose kile unachokitaka.

Kwa mfano kama kiongozi wa nchi hawezi kutumia vizuri lugha ya Kigeni pale anapoonana na wakulu wenzake kuwasilisha hoja za nchi yake, pengine anaweza kushindwa kueleweka vizuri kwani kwenye eneo ambalo anapaswa kutoa kauli za mkazo, anaonekana hawezi kupangilia maneno na kuonyesh hilo wazi kwani inamgharimu kufikiri kufikiri sana kupata tafsiri ya hilo neno anayoltaka kusema kwa lugha ya kwao ili na baadae kutamka kwa lugha ya kigeni. Hali hii haipo kwa baadhi ya viongozi wa mataifa mengine kama ya Kiarabu na hata Russia pia wamekuwa wakijaribu kukuza lugha yao.

Kutokujua lugha vizuri kuna kunyima ujasiri na kukosa uhuru wa kujieleza vizuri...kwa upande mwingine, kutokuijua lugha ambayo unataka kuwasiliana na mwingine, kunakufanya uonekane upo "shallow" hususan pale ambapo unapaswa kuzungumzia vitu kitaaluma. Nadhani wengi ambao mtakuwa mmefuatilia kongamano la WEF lililoisha hivi karibuni mmeweza kuona jinsi gani ambavyo Mhe. amekuwa akibabaika kufikisha hoja nyeti kwa kizingiti cha lugha ya mawasiliano japo kuwa kuna yale aliyokuwa akiyaeleza kwa kiingereza yangeonekana kuwa na mkazo zaidi kama ingerhusiwa kutumia lugha ya Kiswahili ambayo ni nyepesi kwake na viongozi wengi wa Taifa hili.

Ikishindikana sanaaaa, tutumie chakwetu na watafisri kama wengine wafanyavyo.
 
Huyo ni msanii mkubwa, hajui kiingereza, analeta usanii tu na ubishoo
 
Communication skills ndio zinahitajika, kwa lugha yo yote ile. Iwe kiingereza, kiswahili au kikabila.

Na huu ni utaalamu na kipaji cha mtu.
 
natamani niwaone nyinyi mnaomcheka MH RAIS na kiingereza chake mkiongea under pressure,unaweza ukajua kiingereza na ukaulizwa maswali ukajikanyaga sababu ya ugumu wa maswali au wewe kutojiandaa na hayo maswali,sasa sioni cha ajabu rais akipata tabu kujibu hapo,hata ingekuwa kiswahili angeulizwa maswali magumu haswa kuhusu hatua alizochukua kukomesha rushwa na mafisadi lazima angejichanganya,kumbukeni hapo hapigi soga anajibu maswali,by the way washasema sasa hivi lugha ya kiserikali ni kiswahili so to hell na english yenu.
 
natamani niwaone nyinyi mnaomcheka MH RAIS na kiingereza chake mkiongea under pressure,unaweza ukajua kiingereza na ukaulizwa maswali ukajikanyaga sababu ya ugumu wa maswali au wewe kutojiandaa na hayo maswali,sasa sioni cha ajabu rais akipata tabu kujibu hapo,hata ingekuwa kiswahili angeulizwa maswali magumu haswa kuhusu hatua alizochukua kukomesha rushwa na mafisadi lazima angejichanganya,kumbukeni hapo hapigi soga anajibu maswali,by the way washasema sasa hivi lugha ya kiserikali ni kiswahili so to hell na english yenu.
Sawa kaka nimekusoma.
 
Jamani lakini hii ni kama National Issue. waTZ wengi ki-inglish ni issue, wachache sana wanaweza kuongea bila kukunja sura au kuwa wadogo. na wengi wa dizaini hiyo nadhani hawajakulia bongo. kwa sisi ambao ki-inglishi ni lugha ya 3 au 4 huwa inatupa tabu sana kuongea. tunajitahidi kuongea tu sababu wakati mwingine unakuwa umebanwa.

duh umenichekesha sana.
 
Hakuna ajabu yoyote, naamini hata wewe ni hivyo hivyo- you must be extra careful when you talk other people's language. Kiingereza si lugha ya asili.

Nakubaliana nawe mkuu. Kiingereza ni lugha ya kujifunza na hakiongei kila siku. Mtu yeyote ambaye kiingereza siyo "mother tongue" yake anaweza kukosea. Ndo maana marais wa nchi zote ukiondoa Africa huwa wanaongea Lugha zao hata kwenye mikutano ya kimataifa au hata kama amealikwa na raisi wa nchi nyingine, kwa mfano Sarkozy akialikwa na Obama atakuwa anaongea kifaransa hata kwenye dhifa ya kitaifa.

Ninachoweza kukisoma hapa kwa wachangiaji wengi ni chuki kwa rais kwa sababu ya kutotimiza ahadi zake na kutojali hali mbaya ya nchi kiuchumi huku watu wachache wakifaidi na mtu wa chini akiendelea kuwa na hali ngumu zaidi. Nafikiri kama JK angekuwa serious katika kusimamia haki na kutuletea watanzania maendeleo kwa kutumia vyema rasilimali zetu nafikiri hata Ngoswe asingeleta hapa hii hoja.
 
Jana mlimani city alisema hivi........"ku empower" ....the akashituka mzima mzima akarudia "to empower"
Kiswahili lugha ya taifa.... anakipenda sana naona kiko damuni.
Hivi mbayuwayu kwa kiwingereza ni nini? Najaribu kutafuta picha ingekuwaje kama angelihutubia taifa kwa kiwingereza kupitia wazee wa salidarama.
 
nyerere rip big time,umesikia umombo kama wa babu zetu wasomi ila huyu wa saizi (eti naogopa kumtaja)hamna kitu lugha haipandi,anatia huruma akiongea kingereza kama kanumba.....
 
hahahahahaha he!

But Nkapa naye alikuwa kichwa kwa "Queen language", but aisee kuna mtu ashamfuatilia Bob pale bondeni kwa Chimurenga, du hicho kienglish chake huwa kinaflow tu kama katoka kwa Queen country! Manake mpaka Wazim wenyewe pamoja na hasira za maisha huwa wanam admire!! Basi sie tuendelee tu na kiswahili manake ndo tunachokiweza!!hahahaaaaa.....
 
Back
Top Bottom