Kigoma: Walioshtakiwa kuua askari waachiwa huru

Synthesizer

Platinum Member
Feb 15, 2010
11,578
19,887
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Kigoma, imewaachia huru washtakiwa 11 waliokuwa wakikabiliwa na kosa la kuua kwa kukusudia askari wawili wa Jeshi la Polisi na kukata sehemu za siri za mmoja wa askari hao katika mapigano yaliyotokea wakati wa kuwaondoa wananchi waliovamia eneo la Hifadhi ya Ranchi za Taifa (NARCO), wilayani Uvinza.

Hukumu hiyo ilisomwa Ijumaa (Agosti 14), na kesi hiyo ilihusu tukio lililotokea Oktoba, mwaka 2018, wakati wananchi karibu 1,000 walipojiunga kupambana na askari wakiwa na silaha za jadi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma, Ilvi Mgeta, alisema sababu za kuwaachia huru ni ushahidi alioutoa daktari wa Kituo cha Afya cha Lugufu, aliye wahudumia baadhi ya washtakiwa na kueleza kuwa risasi walizopigwa zilipita juu ya ngozi wakati washtakiwa wana makovu makubwa yanayoonyesha risasi zilipita upande mmoja na kutokea mwingine tofauti na shahidi ulivyoeleza.

“Tunashindwa kuelewa kwa nini shahidi huyu alitoa ushahidi wenye nia ya kuidanganya mahakama wakati akiwa anajua ukweli ni ushahidi wa askari walioeleza kuwapo katika mapigano hayo.”

Ushahidi mwingine ulioelezwa kuwa dhaifu ni wa askari walioeleza kushiriki operesheni hiyo kuwa walipambana na wananchi hao uso kwa uso na kufanikiwa kuwapiga risasi wakati wa mapigano, wakati makovu ya risasi hizo kwa watu 10 kati ya 11 walioshtakiwa, yakionyesha kuwa walipigwa upande wa nyuma na kutokea mbele hivyo wapigaji wa risasi hizo hawakuweza kuwaona uso kwa uso washtakiwa.

Pia, Jaji alisema gwaride la utambuzi halikufuata misingi ya sheria kwa kuwa mmoja wa washtakiwa alieleza kuwekwa kwenye mstari akiwa peku na wengine wakiwa na nguo zilizo jaa damu kutokana na majeraha ya risasi, hivyo kurahisisha kutajwa kuwa walihusika na mauaji hayo.

Kadhalika, alisema ushahidi wa aliyeshuhudia gwaride la utambuzi kuiambia mahakama kuwa hakuwaona washtakiwa hao katika gwaride la utambuzi pamoja na maelezo ya onyo yaliyoelezwa kuandikwa na washtakiwa, ambayo wote waliyakana mahakamani kuwa sio yao pamoja na kukamatwa eneo tofauti na tukio lilipotokea katika maeneo tofauti.

Baada ya Jaji Mgeta kupitia uchambuzi wa hoja za pande zote mbili za upande wa Jamhuri uliowakilishwa na Happyness Mayunga, Shaban Masanja na Riziki Matitu na upande wa utetezi ukiwakilishwa na Wakili Sadick Aliki, Kagashe Rweyumamu na Eliuta Kiviylo, alisema kwa kuzingatia uhalisia wa ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo kuonyesha kuwa na taarifa zinazopingana, ushahidi huo ni dhaifu na hauwezi kuwatia hatiani washtakiwa hao na mahakama hiyo imeamua kuwaachia huru washtakiwa wote 11.

Askari waliopoteza maisha kwenye tukio hilo ni Inspekta Ramadhani Mdimu na Koplo Mohamed Nzengohuku. Washtakiwa 11 waliochiwa huru ni Gelya Gisega, Jumanne Jackson, Nkono Mwandu, Shishi George, Masanja John, Hamis Masalu, Walwa Malongo, Makenzi Lukelesha, Masalu Inambali, Petro Bucheyeki na Charles Maduhu.

NIPASHE

------

Nimesoma taarifa za hukumu ya Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma iliyowaachia watuhumiwa wa mauaji ya askari wawili katika tukio lililotokea huko Kigoma Oktoba 2018.

Wakati Polisi walitoa ushahidi kwamba watuhimiwa walijeruhiwa wakiwa wanapambana na askari uso kwa uso, ushahidi kutokana na makovu ya majeraha ya risasi ya watuhumiwa 10 umeonesha kwamba walipigwa risasi nyuma, sio mbele, ikionyesha kwamba Polisi waliwapiga risasi watuhimiwa wakati wakikimbia kuondoka kwenye tukio (shot in the back). Kwa hiyo jambo jingine hapa ni kwamba tuna jeshi la Polisi lenye askari waongo, na ambao hawaoni aibu hata kusema uongo Mahakamani ili kukandamiza washitakiwa!

Baadhi tunakumbuka mauaji ya Sharpville Afrika Kusini yaliyofanywa na askari wa Makaburu kwa wanafunzi ambao walikuwa wakiwakimbia Polisi na kuuwawa au kujeruhiwa kwa kupigwa risasi za nyuma. Dunia nzima, pamojana Tanzania, ililaani kitendo hiki na kukiita ni cha uuaji, ukatili, kisichofuata haki za binadamu, kilichofanywa na polisi wahuni wenye kukosa mafunzo na waoga!

Leo hii kitendo hicho hicho kinafanywa na askari polisi wa Tanzania katika nchi ambayo ilikuwa mstari wa mbele kulaani kile kilichofanywa na askari wa Makaburu!

Ikumbukwe kwamba katika ugomvi kuvamiwa na majambazi ukampiga risasi aliyekuvamia na kumuua, huwezi kujitetea kwamba ilikuwa ni self defence kama ulimpiga huyo mtu risasi ya mgongoni!

Lakini Polisi wetu wanashambulia raia na kuwapiga risasi za migongoni na kujaribu kuidanganya Mahakama kwamba waliwajeruhi hao raia katika mapambano ya uso kwa uso!

Tunasikitika kwamba katika mgogoro huu huko Kigoma kuna Polisi wawili waliuwawa. Lakini hilo halihalalishi Polisi wetu kuanza kuwapiga raia wanaokimbia eneo la tukio risasi za migongoni.

Tungependa kuona serikali ikichukua hatua kali kwa askari wote waliohusika na tukio hili, na kuwawajibisha viongozi wote ambao kwa namna moja au nyingine wanawajibika na hili. Hatuwezi kuwa katika nchi huru ambayo Polisi inapiga raia wake risasi za migongoni na kuwaua au kuwajeruhi. Lazima tuonyenye kwamba nchi hii naendeshwa kwa sheria ambazo zinawahusu hasa askari wanaopewa silaha kwa lengo la kutunza usalama, sio kutumia silaha hizo kuua raia wanaokimbia tukio.

Tuelewe kwamba polisi waliwafyatulia risasi za nyuma kwa lengo la kuua raia wa Tanzania waliokuwa wanakimbia tukio, sio adui adui wa nchi ningine.

Source: Walioshtakiwa kuua askari waachiwa huru
 
Is shooting someone in their back a crime?

We really don’t want to shoot them at all, do we? If we find ourselves in a situation where we feel we must discharge a firearm into another person, the odds are we will have committed a crime. Even if the person was a threat, we will need to show justification for such a level of response. If our actions are excessive, we will likely be charged with some form of manslaughter. The problem with shooting someone in the back is that it is harder to sell Law enforcement, prosecutors and jurors on the idea that we were in clear and present danger.

That is not to say it could not be the truth. If the adversary was reaching forces a weapon, you might be tempted to not wait to see how fast and accurate he might be when he turned around. Just remember, it is a much greater burden of proof.
 
mhh maelezo yako yanakaukakasi ila Mungu ndo anajua haki i upande upi
 
Maelezo yako yamekaa kiushabiki na chuki had umeshindwa kubalance story
Najua wewe ni polisi, huna jingine la kusema zaidi ya kuwa mwongo, mwoga, muuaji, usiye na mafunzo ya kutosha na mkiukaji mkubwa wa haki za binadamu. Unapiga watu risasi mgongoni halafu unajiita mwanaume!
 
Aisee kumbe Raha sana,jambazi ukivamia sehemu polisi wakitokea unawapa mgongo tu hawakufanyi kitu maana hawaruhusiwi kukushoot
 
Najua wewe ni polisi, huna jingine la kusema zaidi ya kuwa mwongo, woga, muuaji, usiye na mafunzo ya kutosha na mkiukaji mkubwa wa haki za binadamu. Unapiga watu risasi mgongoni halafu unajiita mwanaume!
Mihemko inaweza kukufanya uonekane mtu mwenye upeo mdogo wa kufikiri
 
Aisee kumbe Raha sana,jambazi ukivamia sehemu polisi wakitokea unawapa mgongo tu hawakufanyi kitu maana hawaruhusiwi kukushoot
Na aliekuambia Polisi anaruhusiwa kukushoot ni nani? Unajua mazingira ambayo polisi anaruhusiwa ku-shoot? Polisi wa Tanzania wana washoot kina Akwilina bila kuchukuliwa hatua basi watu wanafikiri Polisi wanaruhisiwa kushoot ovo kama wanavyotoa hewa chafu.
 
Sema maelezo yana utata gani tujadirli maana umejibu kama vile wewe ni askari uliekuwapo kwenye tukio
swadakta mkuu, vile umeeleza umeeleza kwa kuangalia upande mmoja zaidi kwahiyo hakuna uzani ulio sawa maana ka askari wawili walifariki inamaanisha walifariki kwa wananchi kukimbia ama kwakushambuliwaa?
yafaa mada iwe bayana ieleweke kwa wote kuwa ilikuwaje watu kumi kufa na hao askari wawili kufa. au na hao askari walifariki wakati wanakimbia? mie sifungamani na upande wowote sema nimeiona stori haijawa na uwiano nikatumia akili ya kawaida kujiuliza
 
swadakta mkuu, vile umeeleza umeeleza kwa kuangalia upande mmoja zaidi kwahiyo hakuna uzani ulio sawa maana ka askari wawili walifariki inamaanisha walifariki kwa wananchi kukimbia ama kwakushambuliwaa?
yafaa mada iwe bayana ieleweke kwa wote kuwa ilikuwaje watu kumi kufa na hao askari wawili kufa. au na hao askari walifariki wakati wanakimbia? mie sifungamani na upande wowote sema nimeiona stori haijawa na uwiano nikatumia akili ya kawaida kujiuliza
MKuu, umeona source lakini? Kama nimeeleza kulingana na hukumu ya Mahakama Kuu ambayo imeangalia maelezo ya pande zote kwa muda mrefu ni kitu gani unataka nifane zaidi ya hapo? Kwamba nianze kusema Mahakama Kuu haikuangalia pande zote au niseme wewe una uelewa zaidi ya hukumu iliyotolewa na majaji wa Mahakama Kuu?

Suala sio askari waliuwawa, hiyo ni thread nyingine pia. Suala ni kwamba hawa watu walipigwa risasi za migongoni wakikimbia, na polisi wakadanganya na kuficha ukweli.
 
MKuu, umeona source lakini? Kama nimeeleza kulingana na hukumu ya Mahakama Kuu ambayo imeangalia maelezo ya pande zote kwa muda mrefu ni kitu gani unataka nifane zaidi ya hapo? Kwamba nianze kusema Mahakama Kuu haikuangalia pande zote au niseme wewe una uelewa zaidi ya hukumu iliyotolewa na majaji wa Mahakama Kuu?

Suala sio askari waliuwawa, hiyo ni thread nyingine pia. Suala ni kwamba hawa watu walipigwa risasi za migongoni wakikimbia, na polisi wakadanganya na kuficha ukweli.
chanzo cha habari kwangu ni wewe kwahiyo nimechangia kulingana na vile umeandika, kwahiyo ka umeandika kwakuacha baadhi ya taarifa nyingine kwa utashi wako namie nimechangia kulingana na utashi wangu baada ya kuisoma na kuielewa, ndo maana awali nilisema anaejua haki i upande gani ni Mungu tuu. mimi na wewe hatujui ukweli u wap tunadhani haki i upande flatu.
 
chanzo cha habari kwangu ni wewe kwahiyo nimechangia kulingana na vile umeandika, kwahiyo ka umeandika kwakuacha baadhi ya taarifa nyingine kwa utashi wako namie nimechangia kulingana na utashi wangu baada ya kuisoma na kuielewa, ndo maana awali nilisema anaejua haki i upande gani ni Mungu tuu. mimi na wewe hatujui ukweli u wap tunadhani haki i upande flatu.
Usiwe mvivu kusoma Mkuu, nimekuwekea link kwa hiyo ulipaswa kuiangalia kabla ya kukimbilia kuandika comments zako. Ukishaambiwa "source" usibishane na thread, nenda kwanza kaangalie source, la sivyo utajionyesha mapungufu katika kiwango cha elimu.
 
Back
Top Bottom