Kigoma: Tundu Lissu adai Barabara za Kigoma zilitelekezwa, zajengwa baada ya Phillipo Mpango kuwa Makamu wa Rais

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,715
218,260
Akifundisha somo la Katiba Mpya kwenye jimbo la Buhigwe, ambalo Mbunge wake alikuwa Phillipo Mpango, kwenye Mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Umati wa Wananchi, Tundu Lissu amedai kwamba, mkoa huo ulitelekezwa kwa miaka mingi kwenye ujenzi wa barabara.

Hata hivyo mara baada ya Dr Mpango kuwa Makamu wa Rais barabara za Kigoma zinajengwa kwa kasi, akiendelea kusema Lissu amedai kwamba hana shida na wana Kigoma kujengewa barabara, maana ni haki yao kabisa, lakini ameshangazwa na ujenzi ambao umesubiri kwa miaka zaidi ya 50 ili Kigoma ipate kiongozi wa Juu ndio ijengewe barabara.

Lissu amesisitiza Umuhimu wa Katiba Mpya kwa vile haitasubiri mtu fulani awe kiongozi ili maendeleo yapelekwe kwao, kwamba Katiba Mpya itaweka haki kwa hata yale maeneo yasiyotoa viongozi ili yapate maendeleo.

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
 
Kwa hiyo na sisi huku kusini tunasubiri tupate makamu wa Rais ndiyo barabara za lami zijengwe? Au sisi barabara zote ni za lami kama huko kaskazini na Zanzibar mnakotoa marais? Lissu ni mjinga tu.
 
Kwa hiyo na sisi huku kusini tunasubiri tupate makamu wa Rais ndiyo barabara za lami zijengwe? Au sisi barabara zote ni za lami kama huko kaskazini na Zanzibar mnakotoa marais?
Lisu ni mjinga tu.
Kwa taarifa kesho lisu anafika kata yakalya tunataka kujuwa chadema ikichukua nchi nini itafanya kwa wavuvi tuliodhulumiwa nakuchomewa malizetu na vichaa magufuli nawaziri wake mpina je wapotayari kuwauliza waiotekelezaji unyama huo walikusanya pesa kiasigani nazipowapi pia machine walichukuwa ngapi na zipowapi?
 
Akifundisha somo la Katiba Mpya kwenye jimbo la Buhigwe, ambalo Mbunge wake alikuwa Phillipo Mpango, kwenye Mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Umati wa Wananchi, Tundu Lissu amedai kwamba, mkoa huo ulitelekezwa kwa miaka mingi kwenye ujenzi wa barabara.



Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
Lissu huwa namkubali kwa kutomung'unya maneno. Mungu aliyemuokoa kwa wauaji wa Magufuli, ampe maisha marefu, Amin
 
Mpaka hapo tayari ni credit Kwa Mama 🔥🔥

Ukiacha Kanda ya Ziwa, Dom na Dar kiukumla Mwendazake alitelekeza miradi ya Barabara Mikoa karibu yote.
 
Tundu Lissu kachemka sana, ndio maana hata yeye mwenyewe hakuongea kwa confidence. Kaongea kwa kurudia rudia weee......bila facts zozote. Mikoa yote ipo kwenye mpango wa kuwekewa rami, barabara za mkoa kwa mkoa au wilaya kwa mkoa. Sasa anashangaa nini barabara kumaliziwa.
 
Akifundisha somo la Katiba Mpya kwenye jimbo la Buhigwe, ambalo Mbunge wake alikuwa Phillipo Mpango, kwenye Mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Umati wa Wananchi, Tundu Lissu amedai kwamba, mkoa huo ulitelekezwa kwa miaka mingi kwenye ujenzi wa barabara.

Hata hivyo mara baada ya Dr Mpango kuwa Makamu wa Rais barabara za Kigoma zinajengwa kwa kasi, akiendelea kusema Lissu amedai kwamba hana shida na wana Kigoma kujengewa barabara, maana ni haki yao kabisa, lakini ameshangazwa na ujenzi ambao umesubiri kwa miaka zaidi ya 50 ili Kigoma ipate kiongozi wa Juu ndio ijengewe barabara.

Lissu amesisitiza Umuhimu wa Katiba Mpya kwa vile haitasubiri mtu fulani awe kiongozi ili maendeleo yapelekwe kwao, kwamba Katiba Mpya itaweka haki kwa hata yale maeneo yasiyotoa viongozi ili yapate maendeleo.

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
Kwani akisema tuu ukweli kwamba zimejengwa baada ya Samia kuwa Rais hatoeleweka Hadi azunguke zunguke?
 
Back
Top Bottom