ngoja waje waongee wengine,
ila mimi mume wangu ni mkubwa kwangu kwa miaka 9 na sasa tuna miaka
mitatu ya ndoa na tayari tuna watoto wawili wa kike(pacha) wana miezi
11, sijawahi kujuta na wala sijawa na wazo, jinsi anavyonilea nikifanya
kitu utasikia no honey wewe bado mtoto acha nitafanya mimi kiukweli ni
maelewano ya kwenda mbele, nilivyojifungua akaniambia miezi 9 uliyobeba
mimba imekutosha sasa ni zamu yake kuhudumia watoto, na akitoka ofisini
unaona masikio yamemsimama kama popo mgeni anawahi kufanya kazi
nyumbani. kiukweli umri ni jambo la muhimu. nadhani ningekuwa na waumri
wangu mambo yangekuwa mengine.