ICHANA
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 4,765
- 3,597
Tufanye jumapili ukirudi kanisani kama kawaida yetu, leo itakuwa vigumu au sio wangu?!
Noted wangu ....usihofu ntakusubir
Tufanye jumapili ukirudi kanisani kama kawaida yetu, leo itakuwa vigumu au sio wangu?!
ngoja waje waongee wengine, ila mimi mume wangu ni mkubwa kwangu kwa miaka 9 na sasa tuna miaka mitatu ya ndoa na tayari tuna watoto wawili wa kike(pacha) wana miezi 11, sijawahi kujuta na wala sijawa na wazo, jinsi anavyonilea nikifanya kitu utasikia no honey wewe bado mtoto acha nitafanya mimi kiukweli ni maelewano ya kwenda mbele, nilivyojifungua akaniambia miezi 9 uliyobeba mimba imekutosha sasa ni zamu yake kuhudumia watoto, na akitoka ofisini unaona masikio yamemsimama kama popo mgeni anawahi kufanya kazi nyumbani. kiukweli umri ni jambo la muhimu. nadhani ningekuwa na waumri wangu mambo yangekuwa mengine.
Ukitaka raha baada ya kazi pitia hapa utaondoa stress zote
Habarini
Natumai nyote mu wazima kabisa nami namshukuru Mungu nipo vyema!
Hebu tuligeukie suala hili la umri kwenye mahusiano yetu ya kimapenzi!
mimi sio mfanya utafiti ila naongea kwa ufahamu wangu tu
Utofauti wa umri je pia ni kigezo cha kujenga mahusiano bora? Namaanisha age difference maana nimekuwa nikiona vijana kwa vijana wanasumbuana mfano, kijana mwenye 25 akiwa na binti wa 22 yrs au juu yake kidogo kunakuwa na msuguano usioisha!
Au wao kwa wao kupishana ndani ya miaka mitano hadi saba hivi bado kunakuwa na fukuto lisiloisha la mara kwa mara!
lakini kwa watu waliopishana zaidi ya miaka kumi na kuendelea hali huwa shwari kidogo!
Je ni kweli kigezo cha Umri ni muhimu kwa wahusika kabla ya kuanza mahusiano?? Epuka kejeli na matusi pia.......nawasilisha
Asanteni
Machache nae utasemaje?
ngoja waje waongee wengine, ila mimi mume wangu ni mkubwa kwangu kwa miaka 9 na sasa tuna miaka mitatu ya ndoa na tayari tuna watoto wawili wa kike(pacha) wana miezi 11, sijawahi kujuta na wala sijawa na wazo, jinsi anavyonilea nikifanya kitu utasikia no honey wewe bado mtoto acha nitafanya mimi kiukweli ni maelewano ya kwenda mbele, nilivyojifungua akaniambia miezi 9 uliyobeba mimba imekutosha sasa ni zamu yake kuhudumia watoto, na akitoka ofisini unaona masikio yamemsimama kama popo mgeni anawahi kufanya kazi nyumbani. kiukweli umri ni jambo la muhimu. nadhani ningekuwa na waumri wangu mambo yangekuwa mengine.
Unebarikiwa kuliko wanawake wote. Mko wachache. Mama Furaha njoo ujiunge JF uungane na huyu binti kuwaambia umma kuwa wapo wanaume wanaojali. Nakumbuka enzi zetu mke wangu akijifunga ile miezi 3 ya uzazi nilikuwa nampikia kabla ya kwenda kazini. Na nikirudi usiku mtoto nilikuwa nabadilisha mimi nepi maana hatukuwa na dusposable na pia kama zingekuwepo kwa mshahara ule tusingeweza. Nimemzidi miaka 5. Cha msingi pendaneni na msiangalie pembeni wanasema nini. Mama alikuja kumtunza mama Furaha alipojifungua alichoshangaa ni kuamka asubuhi na kukuta nimeshachemsha supu!!! Tulijifunza kwa mume wake (baba) na alifurahi. Kitunze kidumu na kila siku kinakuwa kipya.
kwa mtazamo wangu umri unachukuliwa kama kigezo kutokana na ...
1.mwanamke anawai kupevuka sana kiakili kuliko mwanaume.hivyo wapenzi wa umri sawa mf 24.mwanamke atakuwa na uwezo mkubwa wa kufikili kuliko mwanaume..hivyo inapendeza kama mwanaume akamzidi miaka kidoo mpenzi/mke wake ili uelewa wake ukue.
2.kimaumbile mwanaume anachelewa sana kuzeeka kuliko mwanamke.hasa baada ya kujifungua mwili wa mwanamke unachoka halaka..xo ili kuepusha utofauti wao ni vema mwanaume akamzidi kidogo mwanamke ili waweze kwenda sawa...
3.heshima..mwanamme akimzidi umri mwezake heshima inakuwepo kwani atakuwa na uelewa mkubwa sana wa jinsi ya kuiongoza familia yake.na mwanamke atamuheshimu..mtazamo tuuu..
alisema marehemu....Age aint nothing but a number