Kigezo cha Umri kwenye mahusiano

Kigezo cha Umri kwenye mahusiano

stable woman

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2013
Posts
3,883
Reaction score
4,484
Habarini

Natumai nyote mu wazima kabisa nami namshukuru Mungu nipo vyema!

Hebu tuligeukie suala hili la umri kwenye mahusiano yetu ya kimapenzi!
mimi sio mfanya utafiti ila naongea kwa ufahamu wangu tu

Utofauti wa umri je pia ni kigezo cha kujenga mahusiano bora? Namaanisha age difference maana nimekuwa nikiona vijana kwa vijana wanasumbuana mfano, kijana mwenye 25 akiwa na binti wa 22 yrs au juu yake kidogo kunakuwa na msuguano usioisha!

Au wao kwa wao kupishana ndani ya miaka mitano hadi saba hivi bado kunakuwa na fukuto lisiloisha la mara kwa mara!
lakini kwa watu waliopishana zaidi ya miaka kumi na kuendelea hali huwa shwari kidogo!

Je ni kweli kigezo cha Umri ni muhimu kwa wahusika kabla ya kuanza mahusiano? Epuka kejeli na matusi pia.......nawasilisha


Asanteni
 
Umri una determine v2 vingi sana katika uhusiano
 
Jamani!labda mpishane kuanzia hiyo miaka 10,iwe mi5 au 7 me naona mambo ni yaleyale tu!me nadhani tabia ni suala la msingi zaidi haijalishi umri wa mtu!kuna mwingine anaweza kuwa kakuzidi hata miaka 7 lakini ana tabia za ajabu ajabu
 
Vijana wa kuanzia miaka 20 mpk 27 wanakuwa wengi wasumbufu sana kwny mahusiano
 
ngoja waje waongee wengine, ila mimi mume wangu ni mkubwa kwangu kwa miaka 9 na sasa tuna miaka mitatu ya ndoa na tayari tuna watoto wawili wa kike(pacha) wana miezi 11, sijawahi kujuta na wala sijawa na wazo, jinsi anavyonilea nikifanya kitu utasikia no honey wewe bado mtoto acha nitafanya mimi kiukweli ni maelewano ya kwenda mbele, nilivyojifungua akaniambia miezi 9 uliyobeba mimba imekutosha sasa ni zamu yake kuhudumia watoto, na akitoka ofisini unaona masikio yamemsimama kama popo mgeni anawahi kufanya kazi nyumbani. kiukweli umri ni jambo la muhimu. nadhani ningekuwa na waumri wangu mambo yangekuwa mengine.
 
Umri ni no tuuu....
Kikubwa weng wanasema mpishano uzizid 5 yrs
 
kwa mtazamo wangu umri unachukuliwa kama kigezo kutokana na ...
1.mwanamke anawai kupevuka sana kiakili kuliko mwanaume.hivyo wapenzi wa umri sawa mf 24.mwanamke atakuwa na uwezo mkubwa wa kufikili kuliko mwanaume..hivyo inapendeza kama mwanaume akamzidi miaka kidoo mpenzi/mke wake ili uelewa wake ukue.
2.kimaumbile mwanaume anachelewa sana kuzeeka kuliko mwanamke.hasa baada ya kujifungua mwili wa mwanamke unachoka halaka..xo ili kuepusha utofauti wao ni vema mwanaume akamzidi kidogo mwanamke ili waweze kwenda sawa...
3.heshima..mwanamme akimzidi umri mwezake heshima inakuwepo kwani atakuwa na uelewa mkubwa sana wa jinsi ya kuiongoza familia yake.na mwanamke atamuheshimu..mtazamo tuuu..
 
Miss u much .....niaje jamni.
Mim mzima pitia home upate japo juice
Tufanye jumapili ukirudi kanisani kama kawaida yetu, leo itakuwa vigumu au sio wangu?!
 
ngoja waje waongee wengine, ila mimi mume wangu ni mkubwa kwangu kwa miaka 9 na sasa tuna miaka mitatu ya ndoa na tayari tuna watoto wawili wa kike(pacha) wana miezi 11, sijawahi kujuta na wala sijawa na wazo, jinsi anavyonilea nikifanya kitu utasikia no honey wewe bado mtoto acha nitafanya mimi kiukweli ni maelewano ya kwenda mbele, nilivyojifungua akaniambia miezi 9 uliyobeba mimba imekutosha sasa ni zamu yake kuhudumia watoto, na akitoka ofisini unaona masikio yamemsimama kama popo mgeni anawahi kufanya kazi nyumbani. kiukweli umri ni jambo la muhimu. nadhani ningekuwa na waumri wangu mambo yangekuwa mengine.

Your so lucky mamy! Jivunie kuwa nae
 
kwa mtazamo wangu umri unachukuliwa kama kigezo kutokana na ...
1.mwanamke anawai kupevuka sana kiakili kuliko mwanaume.hivyo wapenzi wa umri sawa mf 24.mwanamke atakuwa na uwezo mkubwa wa kufikili kuliko mwanaume..hivyo inapendeza kama mwanaume akamzidi miaka kidoo mpenzi/mke wake ili uelewa wake ukue.
2.kimaumbile mwanaume anachelewa sana kuzeeka kuliko mwanamke.hasa baada ya kujifungua mwili wa mwanamke unachoka halaka..xo ili kuepusha utofauti wao ni vema mwanaume akamzidi kidogo mwanamke ili waweze kwenda sawa...
3.heshima..mwanamme akimzidi umri mwezake heshima inakuwepo kwani atakuwa na uelewa mkubwa sana wa jinsi ya kuiongoza familia yake.na mwanamke atamuheshimu..mtazamo tuuu..

Nashukuru mkuu@byb sac
 
kwa mtazamo wangu umri unachukuliwa kama kigezo kutokana na ...
1.mwanamke anawai kupevuka sana kiakili kuliko mwanaume.hivyo wapenzi wa umri sawa mf 24.mwanamke atakuwa na uwezo mkubwa wa kufikili kuliko mwanaume..hivyo inapendeza kama mwanaume akamzidi miaka kidoo mpenzi/mke wake ili uelewa wake ukue.
2.kimaumbile mwanaume anachelewa sana kuzeeka kuliko mwanamke.hasa baada ya kujifungua mwili wa mwanamke unachoka halaka..xo ili kuepusha utofauti wao ni vema mwanaume akamzidi kidogo mwanamke ili waweze kwenda sawa...
3.heshima..mwanamme akimzidi umri mwezake heshima inakuwepo kwani atakuwa na uelewa mkubwa sana wa jinsi ya kuiongoza familia yake.na mwanamke atamuheshimu..mtazamo tuuu..

kuna kitu inaitwa IQ unaweza ukawa unamiaka 30 ukapitwa na chali wa miaka 20 kwa fikra na akili
 
Back
Top Bottom