Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
Mkuu wa nchi amekanusha vikali uvumi uliozagaa Bongo kwamba serikali yake imepiga bei kwa wamarekani eneo la Kigamboni.
Mkuu huyo alikanusha hayo jana wakati akizindua kivuko kipya cha MV Magogoni na kusema madai hayo kuwa hayana kichwa wala miguu.
"Kuna watu waongo wanasema kigambini imeuzwa kwa Wamarekani, uongo wao umeaminika zaidi,Huu ni uvumi na uongo wa mchana hauna kichwa wala miguu, Wamarekani waje hapa wanatafuta nini?Aliuliza.
Alisema anachofahamu yeye ni kwamba Jiji kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, wanampango wa kuboresha mazingira ya Kigamboni.
Alieleza kuwa kinachofanyika ni kwamba wataalamu wa upimaji wanapima na kupanga vizuri mji huo na kamwe wenyeji wa eneo hilo hawatahamishwa bali watapewa maeneo yaliyopimwa, yatakayobaki watagawiwa wengine.
Ikitokea watendaji wakakiuka ahadi ya kutoa kipaumbele kwa wakazi wa Kigamboni, nipewe taarifa na hapo ndipo malalamiko yaanzie na si vinginevyo,aliahidi Rais Kikwete.
Mkuu huyo alikanusha hayo jana wakati akizindua kivuko kipya cha MV Magogoni na kusema madai hayo kuwa hayana kichwa wala miguu.
"Kuna watu waongo wanasema kigambini imeuzwa kwa Wamarekani, uongo wao umeaminika zaidi,Huu ni uvumi na uongo wa mchana hauna kichwa wala miguu, Wamarekani waje hapa wanatafuta nini?Aliuliza.
Alisema anachofahamu yeye ni kwamba Jiji kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, wanampango wa kuboresha mazingira ya Kigamboni.
Alieleza kuwa kinachofanyika ni kwamba wataalamu wa upimaji wanapima na kupanga vizuri mji huo na kamwe wenyeji wa eneo hilo hawatahamishwa bali watapewa maeneo yaliyopimwa, yatakayobaki watagawiwa wengine.
Ikitokea watendaji wakakiuka ahadi ya kutoa kipaumbele kwa wakazi wa Kigamboni, nipewe taarifa na hapo ndipo malalamiko yaanzie na si vinginevyo,aliahidi Rais Kikwete.