Kifo cha Steven Kanumba na hatma ya Elizabeth Michael (Lulu)

huyo mtoto ni mdogo halafu amekuwa pound sasa hao wote wanachemka nae nadhani umenipata ..lulu hajamuua kanumba bali mungu alishamuandikia kanumba kifo chake lazima sababu awe lulu na pia huwezi ukambadilisha mungu
 
Roho nyeusi tu zinawasumbua, tatizo letu wabongo tunataka kila kukicha wanakuöa yuleyule, ukipiga hatua moja mbele inakua tabu.
 
Mi nahisi wengi itakuwa amepita wakitarajia atadumu sasa wanaumia kuskia alikw na wv kwa lulu inamaansha alipaki
 
Siyo hivyo kinachofanya watu wamchukie Lulu si kwa sababu eti alipendwa na marehemu la hasha bali life sytle yake ni mbovu na kutokana na hilo wanahisi labda ameweza kumfanyia Kanumba.
 
Unayosema ni kweli kabisa ila tatizo la watanzania wengi ni kutokubali ukweli na kupenda kupotoshana. Sheria is there for a reason and if Lulu akipewa sheria kweli wengi watalia. Msije kushangaa bongo movie industry yote ikafa kila mmoja akimuhusisha mwenzake.
 
Mh nilikuwa nasubiri mtu aanzishe huu uzi maana kwenye twitter nafasi ni fupi sana ya kupost.
We are all not sure kama Lulu ndiye alimuua Kanumba. kuwa nae chumbani haimaanishi kuwa ndo muuaji. Biology nilisoma kidogo ila sijawahi kusikia eti ukigonga kichwa kwa kitu kigumu kama ukuta basi unatoa mapovu. Mapovu yanahusiana na kula au kunywa (Drs wanaweza kusaidia hapa kwa technical terms).
Kuna maswali ya msingi hapa.
1. Lulu aliletwa na nani kwa Kanumba
2. Lulu alikuwa anaongea na nani kwenye simu iliyoleta huo ''ugomvi'' na Kanumba?
3. Alipokimbia aliondoka na usafiri gani wakati yeye ndo alimwambia mdogo wake kanumba kuwa kaka yako kaanguka?
4. Ray alikuwa na bifu na kanumba la mda mrefu na alimuahidi eti watamalizana kiume, na sasa ray anasema alipopigiwa simu alikuwa jirani na muhimbili. alipigiwa simu na nani na alipigiwa simu kama nani wakati hawakuwa marafiki wa karibu tena?

kwa nchi yetu ambayo haki ya mtu inaweza ikauzwa ili apewe mwingine, Lulu lazima apate msaada wa kisheria ili aweze kufunguka katika kumtafuta muuaji halali wa Kanumba. Kuwa nae ndani haimaanishi ndo muuaji ila kwa kuwa alikuwa eneo la tukio lazima aisaidie polisi mpaka ukweli ujulikane.
Zitto na Halima wamefanya vizuri na nawaomba mama Bisimba na Usu malya nao wamsaidie huyu mtoto.
Anahitaji msaada wa kisaikolojia maana kampoteza mpenzi wake na hili tukioo ni kubwa sana kwa umri wake na mazingira yalivyotokea.

With a fair trial to Lulu, the truth will be revealed and it may surprise us all


Unayosema ni kweli kabisa ila tatizo la watanzania wengi ni kutokubali ukweli na kupenda kupotoshana. Sheria is there for a reason and if Lulu akipewa sheria kweli wengi watalia. Msije kushangaa bongo movie industry yote ikafa kila mmoja akimuhusisha mwenzake.
 
Mnaomteteta huyu mtoto wote ni wapuuzi She deserves everything na kwanza natamani akae huko hata miaka miwili mitatu...Sio katoto kadogo kazi kuendekeza umalaya tu!
 
Mnaomteteta huyu mtoto wote ni wapuuzi She deserves everything na kwanza natamani akae huko hata miaka miwili mitatu...Sio katoto kadogo kazi kuendekeza umalaya tu!


Kuwa mpole mkuu na kila mtu anaweza kuongea anachotaka yeye, je una uwakika LULU ndio kamuuwa kanumba??Kuwa nae ndani sio ndio kwamba amemuuwa sasa hata mimi mpenzi wangu akinifia ndani ina maanisha kwamba nimemuuwa??inatokea tu na ni swala la kawaida na sio kuwaita watu wapuuzi
 
Steven Kanumba kama alivyofahamika, kwa sasa ni marehemu.

Kifo chake naweza kusema kuwa kimewagusa watu weengi ukizingatia alikuwa ktk fani ya maigizo, na ni mmoja kati ya waigizaji ktk runinga anayetajwa kuwa maarufu sana hapa nchini na nchi za jirani.

Hakuwa msanii mkongwe, lakini amekuwa na nyota ya kupendwa na kuvuta hisia za wengi kwa kipindi hiki kifupi alichojiunga ktk fani hiyo.

Kifo chake pia kimekuwa faraja kwa vyombo vya habari hasa Televisheni na Redio ambazo hazina vipindi vya kueleweka.
Pia hata Magazeti ambayo hayana ya maana ya kuandika, nayo pia yamejaza picha za marehemu na udaku wa hapa na pale.

Kifo cha kijana huyu pia kimeita hata viongozi wa ngazi mbalimbali za kisiasa hapa nchini.
kimemuita mpaka Rais wa nchi na kumlazimu aahirishe safari yake ambayo ilikuwa na manufaa kwa taifa na kuja kujumuika ktk msiba.

Kila kona ya wasio na kazi au wasio na ya maana ya kufanya basi habari imekuwa ni ya kifo cha Kanumba, kwenye basi kanumba, mahospitalini kanumba, stendi kanumba, bar Kanumba, wakristo nao hawaelezi tena kufa na kufufuka kwa Yesu kristo bali nao wameshikwa na kifo cha Kanumba, kila kona ni Kanumba, Kanumba, Kanumba.

wengine wamejaribu kukurupuka na kusema msiba huu ni wa kitaifa.
Wengine wamekuja na wazo eti mwili wa Kanumba ukaagwe ktk uwanja wa Taifa.
Wengine tumewasikia wakikaririwa wakisema kwa nini hakufa Ray badala ya Kanumba?
...Stupid

Binafsi najaribu kuuangalia uwezo wa Kanumba kikazi.
Ni wazi kuwa Kanumba alikuwa ni msanii wa kawaida tu ila nyota yake pamoja na yale aliyowahi kukaririwa Baba yake akiyasema ndiyo yamefanya kijana huyu aonekane ni mkali zaidi hapa nchini.

Kanumba movie zake nyingi ni za kawaida na tumeshashuhudia movie zake nyingi zikikosolewa sokoni na wapenzi wa sanaa hiyo.
Haya ni lazima yasemwe hata kama katangulia mbele ya haki.


kwa miezi ya karibuni uwezo wa uigizaji wa hawa mahasimu wawili yaani Ray na Kanumba umepata ushindani mkubwa toka kwa mtu ambaye anaaminika kuwa yuko ktk chati ya juu kwa sasa, akifahamika kama JB ama Jacob Steven.
Je nini kimefanya Ray na Kanumba waporomoke ktk chati ile na kumpisha bila hiana JB?

binafsi kuna mambo matatu yaliyonifanya nimshushe Kanumba na kumdharau.
1. kwa siku za karibuni Kanumba alikaririwa akisema yeye hana mchumba na wala hanywi Pombe, lakini kifo chake kimedhihirisha kuwa Kanumba alikuwa ni Mzinzi na mlevi pia.
Hivyo ni wazi kuwa Kanumba alikuwa ni msanii muongo mwennye kutaka kuonekana msafi machoni mwa watu


2. Pia Kanumba kwa siku za karibuni amesikika akidai kuwa Baba yake pamoja na mama yake wa kambo walimtesa sana pindi alipokuwa anaishi nao.
Wenye akili wakahoji je walikutesa vipi?
Lakini likaja jibu kuwa Kanumba alipokuwa kwao alikuwa anachunga Mbuzi na kuosha vyombo.
Hayo ndio mateso ambayo Kanumba aliamua kumuanika Baba yake na kupelekea kutoelewana kati yao.
Hapa dogo alikosea...


3.Pia jamii iliamini kuwa Lulu ana uwezo mkubwa wa kuigiza.
Hivyo ilimkabidhi Kanumba mtoto huyo ili akisimamie kipaji cha mtoto huyo lakini Kanumba hakufanya hivyo bali alimtumbukiza mtoto huyo kwenye dimbwi la ngono.


Sasa je kwa machache hayo Kanumba kaifunza nini jamii inayovutiwa na kazi zake za sanaa?
 
michael Jackson alivyokufa basi Obama aliendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa na wala hakukanyaga msibani.

Laiti kwamba Michael na umaarufu wake ule angekuwa ni mtanzania basi tarehe aliyokufa kwenye kalenda zetu tungewekewa kidubwasha chekundu.
Pia tungeenda kuuaga mwili wake ktk viwanja vya ikulu.
Tusingeenda kazini mpaka tumzike.
Na mkulu wetu nadhani angelia hadharani kwa kweli.
 
mimi naona labda katufundisha ngono,pombe na kutafuna kuku mishikaki na chips!
Hakuna kingine.
Ulimbukeni umetujaa tunashindwa hata kufanya kazi zetu za msingi,eti Kanumba Kanumba,Kanumba Kanumba,Kanumba Kanumba who was he?????????
 
michael Jackson alivyokufa basi Obama aliendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa na wala hakukanyaga msibani.

Laiti kwamba Michael na umaarufu wake ule angekuwa ni mtanzania basi tarehe aliyokufa kwenye kalenda zetu tungewekewa kidubwasha chekundu.
Pia tungeenda kuuaga mwili wake ktk viwanja vya ikulu.
Tusingeenda kazini mpaka tumzike.
Na mkulu wetu nadhani angelia hadharani kwa kweli.
Umeona ehee!
Ulimbukeni umetujaa!
Tena usije sikia tukawekewa Kanumba day!
 
mimi naona labda katufundisha ngono,pombe na kutafuna kuku mishikaki na chips!
Hakuna kingine.
Ulimbukeni umetujaa tunashindwa hata kufanya kazi zetu za msingi,eti Kanumba Kanumba,Kanumba Kanumba,Kanumba Kanumba who was he?????????

kweli kabisa...fanculo
 
michael Jackson alivyokufa basi Obama aliendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa na wala hakukanyaga msibani.

Laiti kwamba Michael na umaarufu wake ule angekuwa ni mtanzania basi tarehe aliyokufa kwenye kalenda zetu tungewekewa kidubwasha chekundu.
Pia tungeenda kuuaga mwili wake ktk viwanja vya ikulu.
Tusingeenda kazini mpaka tumzike.
Na mkulu wetu nadhani angelia hadharani kwa kweli.
Tena msafara wa kumzika michael jackson ulikua na gari3 tuu.
So vipi leader2 akausindikize?tena kwa kutumia kodi za wananchi walima nyanya wa mlali-morogoro?
 
madaktari waligoma then jamaa akakwea pipa na kusepa, ile hali huku nchini kuna wazalendo wanakufa tu bila kupatiwa huduma mahospitalini.

Eti kafa Kanumba jamaa na safari kaahirisha duh...
 
Namuomba M/mungu leo kuanzia saa2.30 ashushe mvua ya mawe ili asipatikane mtz yeyote barabarani,leo j,4 watu wote tunatakiwa kua kazini ala!
 
madaktari waligoma then jamaa akakwea pipa na kusepa, ile hali huku nchini kuna wazalendo wanakufa tu bila kupatiwa huduma mahospitalini.

Eti kafa Kanumba jamaa na safari kaahirisha duh...

Jamaa anawazimia sana wasanii na wanamichezo.We unashangaa hillo?
Jamaa alienda Jamaica, then kabla hajakutana na rais wa nchi au kiongozi yoyote wa juu serikalini ye alikutana na Hussain Bolt yule mtoka baruti bingwa wa mita 100.
 
madaktari waligoma then jamaa akakwea pipa na kusepa, ile hali huku nchini kuna wazalendo wanakufa tu bila kupatiwa huduma mahospitalini.

Eti kafa Kanumba jamaa na safari kaahirisha duh...
Tena si mnakumbuka juu ya mgomo wa madaktari kuna mwana jf mwenzetu alifiwa na mtoto wake?na tulicomment hapa juu ya upuuzi wa madaktari na serikali?mbona wahanga hawakupozwa chochote?na mkubwa akakwea zake pipa mamtoni???
 
Namuomba M/mungu leo kuanzia saa2.30 ashushe mvua ya mawe ili asipatikane mtz yeyote barabarani,leo j,4 watu wote tunatakiwa kua kazini ala!

Ebana we huwajui wabongo kwa kujishaua kujishughulisha na shughuli zisizo na msingi.
Tena wako radhi kujidumbukiza kwenye hiyo mvua ili mradi wafike na wamuage.
 
Ebana we huwajui wabongo kwa kujishaua kujishughulisha na shughuli zisizo na msingi.
Tena wako radhi kujidumbukiza kwenye hiyo mvua ili mradi wafike na wamuage.

Na atakayelowana sana atasifiwa.
Yaani bongo kuna watu kichwani sijui kuna mtindi?
 
Back
Top Bottom