Sina hakika lakini ,nimewaza tu na hawa wachache waliowaza Kama Mimi nkaona tuje tupate na ya humu
Je ni kweli Mama wa taifa alizimia na kujikuta yupo Muhimbili baada yakusikia Sita kafariki?
Kama ndiyo, ni kwanini iwe hivyo? Kwani ni ndugu? Inasemekana hata baba alivyoenda Masaki kumsabai Sita hakwenda na Mama.
Pili, Lowasa amekua akisifiwa kua na roho nzuri na ya kusamehe mahasimu wake, vipi ktk msiba wa mzee Sita asionekane popote? Si Masaki, Karimjee wala Bungeni.
Au nna kiherehere tu ,maana huenda leo akaibuka Urambo kumuaga Spika wake.
Asipotokea basi ule wema wake ni wa kaole.
Tatu, hivi mtoto wa mkulima baada ya kuenguliwa na mzee wa msoga kule Dodoma siku ile ndiyo ilikua basi tena? Au yalikua macho yangu kupoteza umakini maana na yy sijamuona Masaki, K, mjee wala Bungeni.
Angekua anatumia gari yake tungesema Katavi-Dar ni mbali, labda uchumi unambana. Anyway, huko kwao ni msimu wa kuandaa mashamba ,labda kathamini zaid shamba kuliko kumuaga Spika wake
Ni hayo tu