Kifo ni kifo tu kiwe ajali au kurogwa yes kuna mambo mengi ya msingi ya kuhoji iwe kabla ama baada ya kifo,mfano mzuri zaidi ni kwa vifo vivyotokana na ajali za barabarani ninavyoelewa ajali hizi nyingi. Kama si zote husababishwa na ama uwajibikaji wa moja kwa moja wa watendaji au watumiaji wa barabara ama chombo cha usafiri kilichohusika na ajali hiyo au kutowajibika kwa namna moja au ingine na pande hizo mbili. Watendaji kwa maana ya serikali,taasisi,na umma kwa ujumla wake,ikiwa ni case ya utengenezaji mbovu wa barabara,uingizwaji wa gurudumu hafifu au vyombo chakavu hapo ni lazima kundi hili likubali uhusika wa moja kwa moja kufanikisha ajali au kifo husika ila kama ni ubovu wa barabara kushindwa kudhibiti mwenendo wa vyombo vya usafiri,hapo kosa ni kushindwa kuwajibika ila hakuna unafiki unaofariji na kukutenga mbali na dhambi yako ama ya kuwajibika ama kutowajibika kama kumbebesha MUNGU kile ambacho kwa binaadamu kimeisha kuwa juu ya uwezo, MUNGU awarehemu wote waliopoteza uhai wao kwenye mzunguko huo ambao bado hatujui hatma yake