kama mtu anataka kuficha identity kwa tz sio kazi ngumu.. sim cards zinauzwa kama peremende na mtu anaweza kuwa na line ya simu akaitumia kwa kazi flani then akaitelekeza. ishu ya PRIVATE NUMBER inafanya kutilia mashaka ukweli wa hii habari
Wapendwa,
huwezi kutuma sms ikatokea private namba, never ever.Jaribu kutunga kitu kingine.
kama Zitto amesema hayo anayodaiwa kusema basi nimeanza kuwa na mashaka naye.
thanks.
Kwa ujumla habari hii ina maswali mengi kuliko majibu
Hapa kuna haja ya kufanya mambo matatu ama manne ili kujua nini kinaendelea.
1.kama ni kweli kuwaw kuna kiongozi aliwapigia simu waandishi wa habari asubuhi saa nne na kuwaambia kuwa kuna habari kubwa siku hiyo, na pia kama kiongozi huyo aliyepiga simu ni huyu huyu aliyempigia zitto basi kuna haja ya huyo kiongozi kujieleza alikuwa anamaanisha kitu gani.
2. inawezekana asiwe mlengwa ni zitto ila alikuwa sumaye kwani naye pia alikuwepo kwenye msafara ,kuna haja ya polisi kuchunguza jambo hili kwa kina na kulipatia majibu ya haraka kwaqni hii itakuwa ni hatari klwa viongozi wetu.
3.lazima mwanahalisi wawe tayari kuwataja waandishi husika ili kuweza kuupata ukweli wa mambo na kujua nini kilimuua waziri wetu ,huenda naye alikuwa ni mlengwa huyo naye alikuwa big news.
Ni lazima kuujua ukweli kwani habari hii ikiachwa inaweza kuleta hisia mbaya na pia kuwajenga watu kisaikolojia kuwa zitto anataka kuuwawa na hii ni hatari kwa taifa haswa ukizingatia hali halisi ya kisiasa kwa sasa.
Dereva ni lazima atafutwe akiwa hai ili kuweza kuieleza ,mahakama kiini cha ajali na pia ni lazima uongozi wa juu wa jeshi la polisi uwajibike kama unashindwa kumtafuta dereva aliyesababisha kifo cha waziri wa serikali , je?akisababisha kifo cha mlalahoi kama mimi atapatikana?
Usalama wa taifa lazima uingizwe matatani kwani kama habari hizi zina ukweli kuna kila sababu kuwa wanajua kinachoendelea kwenye taifa hili lazima wawajibike kueleza nini kinaendelea kimya kimya kwenye nchi hii.
Nami nitaanza uchunguzi wangu ili kujua nini kilitokea na hata kama ni kwenda hadi kwa familia ya dereva na kujua kama kabla ya siku ya ajali alikuwa amesafiri kwenda wapi na kama hali za maisha ya familia zilikuwa tofauti na siku nyingine ,na hapo nitauweka uchunguzi wangu wazi japo unaweza ukachukua muda mrefu kwani mimi sio mtaalamu wa masuala ya kiuchunguzi.
Apparently sikuwa nataka kumkosea heshima Mh Zitto vievile nataka aseme tu kwani domocracy is prevailing-na 'umaurufu'was not in my text!Atanaye,
Zitto alishakuwa maarufu toka kipindi kile tunasoma Mlimani,sasa kusema anatafuta umaarufu sasa ni kumkosea heshima.wewe unataka asiseme kwa sababu itamuongezea umaarufu??
the truth should be told..
Wana JF,
Nilizungumza na mwandishi wa MwanaHalisi na kumweleza ya kwamba siamini kama ajali ile ilipangwa. Ninaamini ni ajali kama ajali nyingine tu. Kuendekeza habari hizi ni hatari sana kwa utulivu wa nchi. Nilimwambia hivyo mwandishi. Ajali ikitokea na nikapoteza maisha, ni mipango ya mungu. Wala sitembei nikiogopa kuwa nitauwawa. Siogopi hata kidogo.
Ni kweli nilipigiwa simu na naibu waziri. Lakini haihusiani hata kidogo na ajali. Mimi kama kiongozi ninawasiliana na viongozi mbalimbali. Sasa kama kiongozi akinipigia simu halafu ikatokea ajali na nikasema yeye ndio kapanga, basi sitakuwa ninawasiliana na viongozi.
MwanaHalisi limekwenda out of the way. Na nimewasialiana na Mhariri wake juu ya hili.
Wana JF,
Nilizungumza na mwandishi wa MwanaHalisi na kumweleza ya kwamba siamini kama ajali ile ilipangwa. Ninaamini ni ajali kama ajali nyingine tu. Kuendekeza habari hizi ni hatari sana kwa utulivu wa nchi. Nilimwambia hivyo mwandishi. Ajali ikitokea na nikapoteza maisha, ni mipango ya mungu. Wala sitembei nikiogopa kuwa nitauwawa. Siogopi hata kidogo.
Ni kweli nilipigiwa simu na naibu waziri. Lakini haihusiani hata kidogo na ajali. Mimi kama kiongozi ninawasiliana na viongozi mbalimbali. Sasa kama kiongozi akinipigia simu halafu ikatokea ajali na nikasema yeye ndio kapanga, basi sitakuwa ninawasiliana na viongozi.
MwanaHalisi limekwenda out of the way. Na nimewasialiana na Mhariri wake juu ya hili.
ndio hiki kitu kinawezeakana,wewe ndio haufahamu nini cha kufanya..nenda karibu na huduma kwa wateja ya kampuni yoyote ya simu..