Kifo cha CHADEMA kimekuwa cha ajabu kweli!

Kifo cha CHADEMA kimekuwa cha ajabu kweli!

Mbuzimtu

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2013
Posts
355
Reaction score
178
Ndugu wanaJF,
Tumeshuhudia utabiri mwingi dhidi ya chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA), kuwa chama hiki kinakufa kwa kasi ya ajabu. Binafsi nimegundua jambo la ajabu sana kupitia kifo cha chama hiki. Kwa kadili kinavozidi kusemwa kuwa kinakufa ndivo kinavozidi kuitesa CCM. Sasa napata maswali mawili makubwa,

MOJA: Chadema kwa mwaka jana na mwaka huu, kimeonyesha kuwa kimeenea kila kona ya Tanzania. Kwamjibu wa wa wanaCCM (Nape) ni kwamba chadema kinakufa kwa kasi kila kona ya nchi?. je, nini maana ya chama cha siasa kufa kila kona ya nchi wakati huo huo kinapenya kila kona ya nchi ambako hakijawahi kufika?.

MBILI: Tangu mwaka 2010 mpaka leo, inaonyesha chadema kimezidi kupendwa na wananchi na zaidi sana tangu kuunda UKAWA watanzania wameongeza kupendana zaidi na wanaiona CCM kama shetani. Kwa hali iliyopo sasa watanzania wanakula CCM wanalala CHADEMA/CU/NCCR-Mageuzi. Tutarajie nini hapo October 2015.
 
Mkuu nadhani hii kauli ya Cdm itakufa,inakufa wahusika waasisi wake wanaijutia wanatatamani kuifuta kwa sababu imekuwa kama petrol na moto
 
Ndugu wanaJF,
Tumeshuhudia utabiri mwingi dhidi ya chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA), kuwa chama hiki kinakufa kwa kasi ya ajabu. Binafsi nimegundua jambo la ajabu sana kupitia kifo cha chama hiki. Kwa kadili kinavozidi kusemwa kuwa kinakufa ndivo kinavozidi kuitesa CCM. Sasa napata maswali mawili makubwa,

MOJA: Chadema kwa mwaka jana na mwaka huu, kimeonyesha kuwa kimeenea kila kona ya Tanzania. Kwamjibu wa wa wanaCCM (Nape) ni kwamba chadema kinakufa kwa kasi kila kona ya nchi?. je, nini maana ya chama cha siasa kufa kila kona ya nchi wakati huo huo kinapenya kila kona ya nchi ambako hakijawahi kufika?.

MBILI: Tangu mwaka 2010 mpaka leo, inaonyesha chadema kimezidi kupendwa na wananchi na zaidi sana tangu kuunda UKAWA watanzania wameongeza kupendana zaidi na wanaiona CCM kama shetani. Kwa hali iliyopo sasa watanzania wanakula CCM wanalala CHADEMA/CU/NCCR-Mageuzi. Tutarajie nini hapo October 2015.

Mkuu Mbuzimtu,
Mpaka sasa CCM wanaomba miezi iende taratibu ili hiyo October isifike mapema.Hizo mbwembwe za Nape kuwa CDM inakufa kwa kasi ni siasa za maji taka tu.Mfano tumeuona huko Sumbawanga kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa ambako kwa matarajio ya wengi tulidhani kuwa bado kuna uelewa mdogo juu ya mambo ya siasa lakini CCM wamenyooshwa kwelikweli.Ukweli unabaki mioyoni mwao tu juu ya nini kitatokea ifikapo October 2015.
 
hivi unajua chiz hatambui kuwa anaumwa ila kinachofanya aonekane chizi ni watu wanaona ama kuadhirika na vituko vya uchiz wake. Sasa watanzania wanaiona ccm na viongozi wake machiz tena wale wadampo walioshindikana mirembe! Ndo maana cdm/cuf/nccr zinaenea kwa kasi kama moto nyikani/ huku nld nayo ikianza kutajwa tajwa tofaut na zaman ilikuwa inatajwa kwenye uchaguz tu
 
Unasema tutarajie nini mwaka huu kwenye uchaguzi mkuu??

Aaaaah, we ndugu inawezekana uko mbali na nchi yako, Wenzako mpaka sasa wanabuni mbinu za kuahirisha uchaguzi mkuu hapa October achia mbali kura ya maoni hapo April 30. Sasa wameagiza Tume ya Uchaguzi iahirishe kuandikisha wapiga kura kwa njia ya Bvr Bali vitumike vitambulisho vya mwaka 2010 ambavyo walikwisha tutamgazia kwamba havina kazi tena!!

Chadema inakufa kwa kasi kubwa sana kama hutaki unaacha... Eboooooh!!!

BACK TANGANYIKA
 
Ni kweli kabisa CHADEMA inakufa:


Rukwa. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeigaragaza vibaya CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika juzi katika kata tatu za Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa ambazo hazikufanya uchaguzi Desemba 14, mwaka jana.

Uchaguzi katika kata hizo uliahirishwa kutokana na kasoro mbalimbali jambo lililosababisha mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, William Shimwela kusimamishwa kazi.

Msimamizi wa uchaguzi huo uliofanyika katika kata za Msua, Chanji na Kizwite na mitaa mingine miwili iliyorudia uchaguzi, Hamid Njovu alisema Chadema ilinyakua jumla ya mitaa 37 kati ya 44 na kuiacha CCM ikiambulia mitaa mitano.
 
Ndugu wanaJF,
Tumeshuhudia utabiri mwingi dhidi ya chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA), kuwa chama hiki kinakufa kwa kasi ya ajabu. Binafsi nimegundua jambo la ajabu sana kupitia kifo cha chama hiki. Kwa kadili kinavozidi kusemwa kuwa kinakufa ndivo kinavozidi kuitesa CCM. Sasa napata maswali mawili makubwa,

MOJA: Chadema kwa mwaka jana na mwaka huu, kimeonyesha kuwa kimeenea kila kona ya Tanzania. Kwamjibu wa wa wanaCCM (Nape) ni kwamba chadema kinakufa kwa kasi kila kona ya nchi?. je, nini maana ya chama cha siasa kufa kila kona ya nchi wakati huo huo kinapenya kila kona ya nchi ambako hakijawahi kufika?.

MBILI: Tangu mwaka 2010 mpaka leo, inaonyesha chadema kimezidi kupendwa na wananchi na zaidi sana tangu kuunda UKAWA watanzania wameongeza kupendana zaidi na wanaiona CCM kama shetani. Kwa hali iliyopo sasa watanzania wanakula CCM wanalala CHADEMA/CU/NCCR-Mageuzi. Tutarajie nini hapo October 2015.

Wewe kweli ndio upo dunia ya kusadikika
 
Itakufa kwanza ccm alafu Chadema itachukua nchi. Cdm haitakufa kabla ccm haijafa.
 
Baada ya ccm kumnunua Zitto waliamini hivyo vurugu kubwa kutokea ndani ya chama
 
Ni kweli kabisa CHADEMA inakufa:


Rukwa. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeigaragaza vibaya CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika juzi katika kata tatu za Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa ambazo hazikufanya uchaguzi Desemba 14, mwaka jana.

Uchaguzi katika kata hizo uliahirishwa kutokana na kasoro mbalimbali jambo lililosababisha mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, William Shimwela kusimamishwa kazi.

Msimamizi wa uchaguzi huo uliofanyika katika kata za Msua, Chanji na Kizwite na mitaa mingine miwili iliyorudia uchaguzi, Hamid Njovu alisema Chadema ilinyakua jumla ya mitaa 37 kati ya 44 na kuiacha CCM ikiambulia mitaa mitano.
Asante kamanda, umeiweka vizuri sana!
 
Naona matokeo ya serikali za mitaa bado yamewachanganya ndio maana mnaanzisha mada za ajabu. Matokeo kamili mtayapata mwezi Oktoba kwenye uchaguzi mkuu.ccm inaelekea kaburini.
 
Mkuu, hakuna mtu yeyote including hao mamburula wa Lumumba wanaokesha humu anayeweza kueleza precisely ni kwanini wanaiombea Chadema "kifo" au ni kwanini wanaichukia hivyo. Nape naye mapovu tu kila kukicha KUILAANI Chadema hebu aeleze ubaya wa Chadema ni upi sijui kama ataweza.
 
Mkuu, hakuna mtu yeyote including hao mamburula wa Lumumba wanaokesha humu anayeweza kueleza precisely ni kwanini wanaiombea Chadema "kifo" au ni kwanini wanaichukia hivyo. Nape naye mapovu tu kila kukicha KUILAANI Chadema hebu aeleze ubaya wa Chadema ni upi sijui kama ataweza.

Pia nape awaeleze watanzania ni lini wale waliogawana fedha za escrow pale bank kubwa watachukuliwa hatua
 
Siku zote anayekufa hawezi kujua kama anakufa ila daktari ndiyo anajua siri ya mgonjwa kuwa anakufa,

kwahiyo chadema kamwe hawatajua kama wamekufa au la!
 
Pia nape awaeleze watanzania ni lini wale waliogawana fedha za escrow pale bank kubwa watachukuliwa hatua
Hili swali anaweza kujibu mbowe na mabtia kwakuwa ni wanufaika wakubwa wa pesa hizo.
 
Mbuzimtu mkuu,

Hizo stori za chama kufa cdm hazijaanza leo, cha msingi ufahamu hizo ni porojo za kujaribu kuwaaminisha wananchi kuwa cdm inapotea.

Kwa ujumla mie naona hoja hiyo ni ya kiji0nga kwa sababu ukiwaambia watu kuwa hiki kitu kinakufa ndo watafanya juhudi kukiokoa,

Huwezi kumshawishi mtu aachane na chama pinzani, kwa hoja hizo na cm wanakosea hapo tu.
 
Chadema ipo hai sana, tena mioyoni mwa watu. Hii yote ni kwasababu wengi wanaoipenda na watakaoipigia kura ni wale ambao hawajitokezi kwenye mikutano yao.

Chadema wategemee kura nyingi sana kuliko wanavyodhania kwasababu CCM imechokwa na hata wafanya kazi wao ila wanaona wakisema hadharani kulinda ugali wao.

Cha muhimu wahakikishe wanawashawishi sana watu wajiandikishe kwenye daftari, watu wapige kura na watu wallinde kura.
 
Back
Top Bottom