Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

Acha kipotee tuu. Hawana maana hawa...

Ai nyiie, msiseme hivyo, kikipona kitabadilika. Niliwazuia watu wasikiite majina mabaya kama vile Escrow kwavile meneno huwa yanaumba. Baba zangu wadogo na mashangazi wanafahamu wazi kuwa chama chetu hakiponi ndiyo maana wanasisitiza eti kiandike wosia kabla ya 2015, kwa kufahamu kuwa hakiponi wamekazana kugawana na kujilimbikizia mali za mgonjwa kabla moyo na mafigo havijaacha kufanya kazi pia. Inshallah, wanaweza kupata aibu kubwa na kuumbuka kama mgonjwa akipatiwa matibabu mazuri na wahudumu wenye moyo, bidii, ujuzi, na huruma na kupona. Kwasasa tuko macho kuwabaini wale wote wenye tabia ya kunywa uji wa mgonjwa wetu kwa kuwa tunafahamu kuwa episode moja tu tena itasababisha mgonjwa apate degede, kuharisha na kutapika hadi kukata kamba. Hatukubali, kimetulea, kutusomesha na kutulinda. Yaliyopita si ndwele, kwani tunajua kuwa watu wetu watatusamehe haraka kwasababu niwepesi wa kusahau na wagumu wa kukumbuka yaliyopita.
 
ndugu yang nakushauri jiandae kisaikolojia, hamna namna mgonjwa wako anaweza poa, make kama mpaka mishipa ya ubongo ishaoza hata apone atafanya nin? pole na jikaze huo ndio ukubwa
 
CCM wakimbilia mahakamani kuogopa marudio ya uchaguzi, kata ya Makoko mtaa wa Zanzibar, na kata ya kitaji mtaa wa kitaji D.

Mkurugenzi wa manispaa ya musoma mjini ambaye ni msimamizi wa Uchaguzi ndugu Ahmed Sawa amekiri kuwepo kwa zuio Hilo la Mahakama.

Hivyo itapelekea uchaguzi huo kutofanyika siku ya jumapili kwa hujuma za CCM na mawakala wake mkoa wa mara.
 
miaka nenda miaka rudi ccm inakufa inakufa, ccm ni kiboko yenu.

kama kweli ccm ni kiboko je ni kwanini wamenyang'anywa mitaa 2600 waliyokuwa wanaiongoza?na ni kwanini wanaogopa kufanya uchaguzi wa huru na haki?
 
Kitendo cha kuzuia uchaguzi wa marudio kwa kutumia mahakama ni dalili za mwisho za Ccm
 
Back
Top Bottom