Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

R.I.P chama cha mafisadi
Mimi sielewi kwa nini watu hawaoni hata kilicho mbele yao.
Hivi kigezo chenu ni kipi? mkiangalia baadhi ya michango yangu kabla ya uchaguzi uliopita niliwaambia hamkunielewa sana sana ni kukashifu sana maan wengi wa vijana waliomo humu wana phd ya kukashifu.
Uchaguzi wa serikali za mitaa ambao umeisha hivi karibuni upinzani umepata asilimia ngapi?
Cha msingi hapa kuweni realistic mtambue udhaifu wa vyama vyenu na mjenge mikakati thabiti ya kujiuza kwa wenye nchi bila ya hivyo mtaishia kutukana tu na mwandawazimu akimtukana mwenye akili timamu hutabasamu ni kuelea na hamsini zake maana anafahamu huyo kiumbe mwenzake ni punguani.
 
Kwanza salam
nasema ccm si chama cha siasa tena kwa sababu kimeacha misingi yake na kuanza kufenya kazi kwa kutumia ile misingi aliyoikataa mwasisi wake baba wa taifa nikiangalia njia wanazotumia ccm kupata viongozi wake nakumbuka usemi aliowahi kuniambia mwalimu wangu kuwa kila mzazi anamwandaa mtoto wake ili aje awe mrithi wake kwa maana nyingine mkulima anamwandaa mtoto wake ili aje kuwa mkulima na kiongozi anamwandaa mtoto wake ili aje kuwa kiongozi nasema hivyo kwa sababu ya mfumo huu walioanza kuutumia ccm kuwa kila nafasi ya kiongozi itakayotokea itajazwa na mtoto wa kiongozi huu ni mfumo wa hatari sana na utakuja kuirudisha nchi hii kwenye mfumo wa kifalme na ninawaomba wananchi msikubali kushabikia mfumo huu ukizoeleka tutakuja kujutia hebu angalia viongozi wa ccm ulinganishe na viongozi wa vyaama vingine mfano Nape baba yake alikuwa Moses mnawie kiongozi wa ccm, Ali Kigoma baba yake alikuwa Kigoma Malima kiongizi wa , makongro Nyerere , vita Kawawa, Zainabu Kawawa, Zainabu Gama ,watoto wa sokoine,arusha tuliona alipofariki mbunge Sumari aliteuliwa mtoto wake Sioi sumari na kana sio wananchi wa arusha kukataa utawala wa kifalme leo angekuwa mbunge . Angalia kalenga amefariki mginwa ameteuliwa mtoto wake ANGALIA CHALINZE Ridhiwani kikwete ndie mgombea mfumo huu na wanaccm wanaushabikia hivi hakuna mwana ccm asie kiongozi mwenye mtoto anaeweza kuwa kiongozi?? mimi sijui lakini kwa maoni yangu huu ni mfumo mbaya usiotakiwa kushabikiwa na mtu eyyote na niwakupigwa vita kwa nguvu zote
 
Kijana rudi kijijini maisha ya mjini yatakupa uchizi
 
Kwanza salam
nasema ccm si chama cha siasa tena kwa sababu kimeacha misingi yake na kuanza kufenya kazi kwa kutumia ile misingi aliyoikataa mwasisi wake baba wa taifa nikiangalia njia wanazotumia ccm kupata viongozi wake nakumbuka usemi aliowahi kuniambia mwalimu wangu kuwa kila mzazi anamwandaa mtoto wake ili aje awe mrithi wake kwa maana nyingine mkulima anamwandaa mtoto wake ili aje kuwa mkulima na kiongozi anamwandaa mtoto wake ili aje kuwa kiongozi nasema hivyo kwa sababu ya mfumo huu walioanza kuutumia ccm kuwa kila nafasi ya kiongozi itakayotokea itajazwa na mtoto wa kiongozi huu ni mfumo wa hatari sana na utakuja kuirudisha nchi hii kwenye mfumo wa kifalme na ninawaomba wananchi msikubali kushabikia mfumo huu ukizoeleka tutakuja kujutia hebu angalia viongozi wa ccm ulinganishe na viongozi wa vyaama vingine mfano Nape baba yake alikuwa Moses mnawie kiongozi wa ccm, Ali Kigoma baba yake alikuwa Kigoma Malima kiongizi wa , makongro Nyerere , vita Kawawa, Zainabu Kawawa, Zainabu Gama ,watoto wa sokoine,arusha tuliona alipofariki mbunge Sumari aliteuliwa mtoto wake Sioi sumari na kana sio wananchi wa arusha kukataa utawala wa kifalme leo angekuwa mbunge . Angalia kalenga amefariki mginwa ameteuliwa mtoto wake ANGALIA CHALINZE Ridhiwani kikwete ndie mgombea mfumo huu na wanaccm wanaushabikia hivi hakuna mwana ccm asie kiongozi mwenye mtoto anaeweza kuwa kiongozi?? mimi sijui lakini kwa maoni yangu huu ni mfumo mbaya usiotakiwa kushabikiwa na mtu eyyote na niwakupigwa vita kwa nguvu zote
Mimi naona hamna kosa kabisa kwenye huu mfumo unasema wakurithishana.Labda sijakuelewa vzr wamerithishana vipi.mfn kalenga huyo mtt wa Mgimwa wamempigia kura Ridhiwani kapigiwa kura.Wewe unataka kuniambia katiba mpya tuweke kipengele SIO RUHUSA BABA YAKO AKIWA MBUNGE,MJUMBE WA MTAA,RAIS MTOTO KUGOMBEA NAFASI YAKE?Mawazo mgando hayo wewe kama humtaki mtu usimpigie kura basi.Kama mtu havunji katiba ya nchi yupo sahihi hamna ubaya.Nionalo kwako ni roho ya kwanini tuu.Nasema raia wa kawaida sina hata ndugu tuseme balozi lakini kwa hili unalosema unakuwa unaleta ubaguzi ambayo ni dhambi mbele za wanadamu wenzako na kwa MUNGU pia.
Najua utanikosoa ila ukweli ni ukweli tuu hata kama inauma.
 
Mimi naona hamna kosa kabisa kwenye huu mfumo unasema wakurithishana.Labda sijakuelewa vzr wamerithishana vipi.mfn kalenga huyo mtt wa Mgimwa wamempigia kura Ridhiwani kapigiwa kura.Wewe unataka kuniambia katiba mpya tuweke kipengele SIO RUHUSA BABA YAKO AKIWA MBUNGE,MJUMBE WA MTAA,RAIS MTOTO KUGOMBEA NAFASI YAKE?Mawazo mgando hayo wewe kama humtaki mtu usimpigie kura basi.Kama mtu havunji katiba ya nchi yupo sahihi hamna ubaya.Nionalo kwako ni roho ya kwanini tuu.Nasema raia wa kawaida sina hata ndugu tuseme balozi lakini kwa hili unalosema unakuwa unaleta ubaguzi ambayo ni dhambi mbele za wanadamu wenzako na kwa MUNGU pia.
Najua utanikosoa ila ukweli ni ukweli tuu hata kama inauma.

Nonsense!
 
Mimi naona hamna kosa kabisa kwenye huu mfumo unasema wakurithishana.Labda sijakuelewa vzr wamerithishana vipi.mfn kalenga huyo mtt wa Mgimwa wamempigia kura Ridhiwani kapigiwa kura.Wewe unataka kuniambia katiba mpya tuweke kipengele SIO RUHUSA BABA YAKO AKIWA MBUNGE,MJUMBE WA MTAA,RAIS MTOTO KUGOMBEA NAFASI YAKE?Mawazo mgando hayo wewe kama humtaki mtu usimpigie kura basi.Kama mtu havunji katiba ya nchi yupo sahihi hamna ubaya.Nionalo kwako ni roho ya kwanini tuu.Nasema raia wa kawaida sina hata ndugu tuseme balozi lakini kwa hili unalosema unakuwa unaleta ubaguzi ambayo ni dhambi mbele za wanadamu wenzako na kwa MUNGU pia.
Najua utanikosoa ila ukweli ni ukweli tuu hata kama inauma.

Unavyo andika unaonesha kabisa uwezo wako uko chini sana! Unajaribu kuelezea jambo ambalo kwakweli nigumu sana kulielezea,pole sana ndugu yangu kwa kuelezea jambo ambalo halielezeki!Unatakiwa kuangalia mambo kwa upana zaidi,jaribu kufikili nje ya box! ndiyo maana andiko lako ni senseless kabisa pole sana!
 
Unavyo andika unaonesha kabisa uwezo wako uko chini sana! Unajaribu kuelezea jambo ambalo kwakweli nigumu sana kulielezea,pole sana ndugu yangu kwa kuelezea jambo ambalo halielezeki!Unatakiwa kuangalia mambo kwa upana zaidi,jaribu kufikili nje ya box! ndiyo maana andiko lako ni senseless kabisa pole sana!
Najua umeona kama natetea ndio maana ukasema uwezo upo chini.Najua pia umetoa hii thread baada ya Ridhwani kupitishwa labda pia kalenga Mtoto wa Mgimwa kupitishwa.Nipe point yako kubwa kuliko ambapo kavunja katiba ya nchi au kanuni za uteuzi wa uchaguzi.Usitumie muda wako kuamini sana akili za kuambiwa.Wee lazima Chadema sasa ushapewa akili za kuambiwa sasa unajifanya unajua.Mbona Chadema mtoto wa Ndesamburo ni mbunge viti maalum au pale palichezwa rafu au walipima uwezo wao.Ngoja nikupe haki moja kikatiba mf ukitaka kugombea ubunge lazima uwe na miaka 21.Haikusema miaka 21 ila usiwe mtoto wa kiongozi wowote.
Nilijua unapoint kumbe walewale akili za kushikiwa ila kama ulivyosema uandishi wa mtu unaonesha mtu wa jinsi gani hata mimi nimegundua DHAMBI YA UBAGUZI IPO KWAKO KUONA KUNA WATU HAWARUHUSIWI KUFANYA HIVI.Ila tutakwenda ngoja katiba mpya itengenezwe vizuri ila tatizo wewe hujasoma katiba ya sasa usingepost hizo pumba zako.

ILA HUU NI MTAZAMO TUU NAJUA UMEKUNYWA MAJI YA BENDERA HUTANIELEWA.
 
Najua umeona kama natetea ndio maana ukasema uwezo upo chini.Najua pia umetoa hii thread baada ya Ridhwani kupitishwa labda pia kalenga Mtoto wa Mgimwa kupitishwa.Nipe point yako kubwa kuliko ambapo kavunja katiba ya nchi au kanuni za uteuzi wa uchaguzi.Usitumie muda wako kuamini sana akili za kuambiwa.Wee lazima Chadema sasa ushapewa akili za kuambiwa sasa unajifanya unajua.Mbona Chadema mtoto wa Ndesamburo ni mbunge viti maalum au pale palichezwa rafu au walipima uwezo wao.Ngoja nikupe haki moja kikatiba mf ukitaka kugombea ubunge lazima uwe na miaka 21.Haikusema miaka 21 ila usiwe mtoto wa kiongozi wowote.
Nilijua unapoint kumbe walewale akili za kushikiwa ila kama ulivyosema uandishi wa mtu unaonesha mtu wa jinsi gani hata mimi nimegundua DHAMBI YA UBAGUZI IPO KWAKO KUONA KUNA WATU HAWARUHUSIWI KUFANYA HIVI.Ila tutakwenda ngoja katiba mpya itengenezwe vizuri ila tatizo wewe hujasoma katiba ya sasa usingepost hizo pumba zako.

ILA HUU NI MTAZAMO TUU NAJUA UMEKUNYWA MAJI YA BENDERA HUTANIELEWA.

Du naona sasa umeisha nibatiza uchadema na hilo ndiyo tatizo linalowasumbua watanzania wengi sana,hamjui kwamba kuna watu free na wala si washabiki wa chadema wala CCM.Mimi siyo chadema wala CCM ila ni mpinga maovu ktk nchi yangu ya Tanzania na wala siungi mkono hata akina Ndesambulo na kina Lissu kuweka Dada zao Bungeni na watoto wao! hayo ni mambo ya ajabu kabisa na huo pia ni ugonjwa mkubwa wa CCM na ndiyo maana nimekuambia fikili na nje ya Box.Unaniambia kuhusu Ridhiwan wala mimi siko interested hiyo ni juu ya hao wanaokubali kuchezewa namna hiyo! unadhani ingekua ninakotoka mimi ujinga kama huo tusingekubali hata siku moja.

CCM inamtaji wa wajinga ndiyo maana itaendelea kutesa sana baadhi maeneo ya nchi hii!swala hapo siyo kuvunja katiba lakini kwa akili ya kawaida unadhani kwa maeneo yenu hayo kuna mtu atathubutu kumpinga? hahahahha thubutu siyo nyie nawajua sana!nenda sehemu za wanaoelewa mambo uone kama utawachezea na mambo hayo! kama unabisha kamuulize Mramba,pamoja na kuweka lami lakini alikataliwa na warombo! wengine hatuabudu majina bwana.
 
Ikiwa ni muda mrefu umepita,tokea watanzania tupate uhuru, tukiwa chini ya utawala wa TANU, hatimaye CCM bado mabadiliko makubwa hayajafanyika kuonesha malengo ya kulipatia taifa letu maendeleo. Awamu ya kwanza ilianza vyema, lakini mawazo ya Mwalimu JK Nyerere yalipoanza kukiukwa katika awamu ya pili, ya tatu na hatimaye ya nne ndio sasa watanzania tunaona tuko katika jehanamu iliyojaa chuki,njama,ufisadi, na umaskini uliokithiri.

Ni ukweli usiofichika CCCM na uongozi wake wote imeshindwa kutatua matatizo yanayotukabili, na niseme imekuwa ikituongezea tabu kila kukicha. Nianze na MGOMO WA MADAKTARI, AJALI ZA ZANZIBAR, SUALA LA MUUNGANO,KILIMO n.k vyote vinatabiri kifo cha CCM, kwa kuzingatia kuongezeka kwa machafuko nchini.

Watanzania walio wengi wenye akili timamu na hekima nadhani tayari wameshajiandaa kufanya mabadiliko makubwa 2015 ,na namini itakuwa ndio mwisho wa utawala wa kidhalimuna dhaifu wa CCM!

NA HICHO NDICHO KIFO CHA CCM 2015!

-------------------------------


mkuu good

this ndio post ambazo nilizoea kuziona jamii forum
 
Huu ndio ukweli usio pingika kuwa hizi ni saa za mwisho za chama cha mapinduzi kuwepo madarakani, na sababu zake ni kama zifuatazo.

1. Wamekiuka miiko ya chama iliyoachwa na waasisi wa taifa hili Nyerere,Kawawa,jaji Warioba na wengineo.
Chama siyo cha mkulima na mfanyakazi,bali ni cha mabwanyenye na wala rushwa wakubwa mfano: EPA,Green Dip,mikataba ya IPTL, rada,richmond,merermeta na mengineyo mengi tu!

2. Watanzania wameichoka CCM, mfano ni kwenye mikutano na maadhimisho mbalimbali bila kuweka kivutio kama vyakula ,vinywaji na kuwapatia watu usafiri hiyo sherehe au maadhimisho yatahudhuriwa na watu wachache sana tofauti na miaka ya 80,90 na mwanzo wa 2000 -2005 hivi watu walikuwa wanajaa sana.

3. Ongezeko la vijana wengi wenye uelewa na wasiodanganyika ambao wana maliza shule za sekondari za kata na nyinginezo kwa wingi. Hawa vijana wanaushawishi mkubwa kwa jamii na hawadanganyiki kirahisi ,kinachotakiwa ni kuwaelmisha ili wajiandikishe kwenye daftari kwa kila mmoja.

4. Kurithishana madaraka.
 
5. Kuna wengi wanaoutaka urais kupitia kwao, hawatapaacha salama wasipopitishwa. 6. Katiba mpya na muumdo utakaotokana nayo utaiacha ccm hoi.
 
Yote ni mawazo feki kama ccm ikianguka unafikiri nani aliyekamili ataongoza taifa hili. CDm ni saccos hujui? Mbulula we yaani hata Leo najua we ni mshika pembe tu
 
Ni mchungu kwa wnaccm wachumia tumbo na mambulula, itabidi waukubali tu, maana huwezi kushindana na upepo wa mabadiliko, ccm wanaojitambua hawana shida, hili wanalielewa, ndio maana mweyekiti wao taifa, aliwaambia wajindae kisaikolojia, tunataka kuking'oa chama kinachokumbatia mafisadi wakiongozwa na Lowasa anayeutafuta urais kwa nguvu, ccm safari imeiva, mtake msitake, tumeamua iwe hivyo.
 
Ccm sio chama cha wakulima na wafanyakazi, bali ni genge la wahujumu maslahi ya wa watanganyika na watanzania! Cheki kwenye kuelekea kupata katiba mpya ccm imekuwa kikwazo!
 
Yote ni mawazo feki kama ccm ikianguka unafikiri nani aliyekamili ataongoza taifa hili. CDm ni saccos hujui? Mbulula we yaani hata Leo najua we ni mshika pembe tu

yaanai wewe hata muda wa kufikiri nadhani huna kutokana na mhemko. hivi unadhani chama mbadala ni CDM tu?? mwaka huu lazima CDM iwape pressure. mbona kuna CUF na NCCR mpaka ACT wapo lakini unakomaa na CDM tu? tulia ila mabadiliko lazima yawepo hata kama sio 2015.
 
Back
Top Bottom