Transistor
JF-Expert Member
- Aug 8, 2013
- 1,061
- 1,639
SECURITY MASTER CIRCUIT
Top view ya circuit inaonekana hivi
Bottom view inaonekana hivi
KAZI AMBAZO INAWEZA KUZIFANYA
1.Kutambua mabomu na siraha zozote za chuma mfano bunduki.
kifaa hiki kikifungwa mlangoni,au sehemu yeyote watu wanapo ingilia kitasaidia kugundua ubebaji wa siraha hizo hata kama zipo ndani ya mabegi au masanduku.
Vilevile kifaa hiki kinaweza kutengenezewa kigari kidogo(toy car) ambacho kitakua kinabeba sakiti hii ili kukagua mabomu maeneo ambako kunahisiwa bomu lipo,.
Hii itasaidia kupunguza hatari kwa mkaguzi binadamu kusogea eneo la hatari,hivyo badala ya binadamu kusogea eneo la hatari kifaa hiki kitapakiwa katika kijigari kinacho endeshwa na remote na kupelekwa eneo hilo linalohisiwa kuwa na bomu.
Endapo kifaa hiki kitagundua uwepo wa bomu kitatuma ujumbe kwa njia ya sms pia kitawasha king'ora kuashiria uwepo wa kitu cha hatari.
2.Unaweza kuitumia kama Door security guard.
Kazi nyingine inayoweza kufanywa na kifaa hiki ni kama door security ambapo kinafungwa katika mlango wako.
Mlango wa (gari,nyumba au chochote) utakapo funguliwa au kuvunjwa bila idhini yako,ndani ya sekunde 30 utapata ujumbe kwenye simu yako(Ujumbe huu utakutaarifu kuwa mlango wako umefunguliwa).Popote pale utakapokuwa.
Baada ya kukutumia ujumbe kifaa hiki kitaanza kupiga ALARM au KING'ORA chenye sauti kali ili kuwataarifu wale watakao kuwa jirani kuhusu uvamizi huo.
Unaweza kuitumia sakiti hii vilevile katika sehemu yeyote unayo hifadhi vitu vyako vya thamani ambapo usingependa pafunguliwe na mtu mwingine bila idhini yako.
NB
Ufanyaji wake wa kazi wa skiti hii unaweza ku-design-iwa katika hali tofauti tofauti kulingana na mahitaji ya mteja.
(The design is not fixed)
3.Unaweza kuitumia kama Object ditecting.
Kifaa hiki unaweza ukakitumia kutambua kizuizi chochote ambacho kitakua kinasogelea mlango wako,dirisha lako aukuta wako n.k
Mfano kama mtu atakua anasogelea mlango wako kabla hajaufikia kifaa hiki kitagundua uwepo wake na kufanya maamuzi kutegemeana na wewe unataka kifanye nini kinapo hisi kizuizi.
Mfano;-
unaweza ukataka kikihisi kizuizi kiwashe taa(mfano ni usiku huna haja ya kuwasha security lamps muda wote taa zitajiwasha tu pale mtu au kitu chochote kinaposogelea nyumba yako.hii inasaidia kupunguza bili ya umeme).
Vile vile reaction za kifaa siyo fixed utapendekeza wewe unataka kifaa kifanye nini kinapo hisi kizuizi.
4.Touch detector
Pia kifaa hiki unweza ukakitumia kutambua mtu anapo gusa,kitasa cha mlango wako;reaction yake itategemeana na wewe utataka nini kifanyike pale mtu anapogusa kitasa cha mlango wako wa gari,nyumba n.k
Kazi hizi na nyingine nyingi zinaweza kufanywa na sakiti hii!
Kama utataka u-design-iwe kitu chocho te cha electronics wasiliana nasi tutajitahidi kadri tuwezavyo ili wazo lako liwe kitu harisi.
Tazama ufanyaji wake wa kazi YOUTUBE part 1 and YOUTUBE part 2
Kwa wale wanaopenda kujifunza design za electronics darasa limeanza tayari ingia HAPA
"IT IS ALWAYS IMPOSSIBLE UNTILL IT IS DONE "