Kifaa cha kutafsiri lugha

Kifaa cha kutafsiri lugha

Kwa ufupi ni kwamba unachagua lugha yako katika lugha ambazo zimrtayarishwa unabonteza,unakuta mfasiri yupo live
Hata kama mpo watu 20 lugha tofauti,basi watawekwa wafasiri 20 tofauti ili kukidhi haja za wageni
thanks kiongozi kwa good comment!
 
Siyo kweli kile kifaa kina uwezo wa kutranslate Chenyewe, na kina fanya kazi kwa Lugha wazo feed kwenye kifaa hicho. Sasa akiwa anatafsiri mtu, kama kuna watu watatu wasio elewe Lugha inayongewa alafu wakalimani watafsiri si itakua fojo.
umenikera sana aisee daah
 
Skype software ya Microsoft ambayo watu wanaotumia kufanya video call inauwezo wa kutafsiri real time, sema sio lugha zote, Kuna Lugha kubwa tu Duniani Kama Kingereza, Kichina, kifaransa etc

Angalia demo Yao Hapa
 
Kwenye mikutano inaweza kua kuna watafsiri wapo lakini kwa technology ya leo hata Google wana application ya kutafsili lugha pia Amazon wana kifaa kinaitwa Alexa unawepiga nae hata story.
 
Kama vipo ngoja nikakinunue niache kung'ang'ana na kupoteza muda kujifunza kichina na kispain
 
Siyo kweli kile kifaa kina uwezo wa kutranslate Chenyewe, na kina fanya kazi kwa Lugha wazo feed kwenye kifaa hicho. Sasa akiwa anatafsiri mtu, kama kuna watu watatu wasio elewe Lugha inayongewa alafu wakalimani watafsiri si itakua fojo.
Kipindi cha mwanzo walikuwa wanatafsiri watu kabisa, mwalimu wangu wa advance ndio ilikuwa kazi yake kufanya tafsiri na ukalimani kwenye mikutano mikubwa ya viongozi ingawa siku hizi machine ndio inafanya hiyo kazi, ingawa ina changomoto nyingi kwenye kufanya tafsiri na kukalimani
 
Acha kubisha busha vitu usivyo vijua, natumia free basics nashindwa kuattach picha Tena ya juzi mkutano wa sadc nikuonyeshe, acha ujuaji!
Very true kuna translation butty wako watu ndio hutafsi kwa lugha za hadhira iliyopo ila huyu hataki kuelewa kaleta swali na majibu yake ukweli wapo watu hutafsiri hawaonekani sababu wao ni sehemu ya mitambo
 
Ngoja nijaribu kuchangia kwa kuanza kuweka sawa, maana ya tafsiri na ukalimani. Hizi dhana zinachanganywa sana;

Tafsiri (Translation) ni hali ya kuhaulisha (kubadilisha) mawazo yaliyopo katika maandishi kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine. Hivyo, tafsiri uhusisha lugha ya maandishi.

Ukalimani (Interpretation) ni hali ya kuhaulisha mawazo yaliyopo katika lugha ya mazungumzo, kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine. Hivyo, ukalimani uhusisha lugha ya mazungumzo.

Zipo kampuni ambazo zimetengeneza software mbalimbali, zinazoweza kutafsiri au kukalimani (Machine translation or interpretation), lakini si lugha zote zimeingizwa katika mfumo. Fahamu, kompyuta inafanya kazi kama ilivyoprogamiwa. Kompyuta inaelekezwa na binadamu nini cha kufanya.

Kuhusu Kiswahili na Jiwe; sina uhakika lakini kuna asilimia kubwa, huwa kuna binadamu (humani interpreters), wanaofanya ukalimani wakiwa ndani ya vyumba maalumu ambavyo havipitishi sauti ( Sound proof).

Kuna sababu za msingi kwa nini binadamu ataendelea kufanya ukalimanj au tafsiri;

Lugha humu duniani hutofautiana katika vipengele mbalimbali, hivyo kuifanya wakati mwingine mashine kushindwa au kupotosha ujumbe.

Kwa mfano, mashine inaweza kushindwa kutoa ujumbe sahihi pindi unapozungumza au kuchapa Kiswahili cha mtaani, kukosea matamshi, au miundo ya sentensi.

Binadamu ataendelea kukalimani vikao muhimu, mfano AU, SADC, UN etc.
 
Skype software ya Microsoft ambayo watu wanaotumia kufanya video call inauwezo wa kutafsiri real time, sema sio lugha zote, Kuna Lugha kubwa tu Duniani Kama Kingereza, Kichina, kifaransa etc

Angalia demo Yao Hapa
Hii inapoteza ladha ya mkutano imekaa kama VAR.
 
Siyo kweli kile kifaa kina uwezo wa kutranslate Chenyewe, na kina fanya kazi kwa Lugha wazo feed kwenye kifaa hicho. Sasa akiwa anatafsiri mtu, kama kuna watu watatu wasio elewe Lugha inayongewa alafu wakalimani watafsiri si itakua fojo.
inno.jpg


Huyu ni Innocent Mungy, afisa habari muandamizi, na hapa alikua katika majukumu yake hivi karibuni katika vikao vya SADC,hapa alikua akitafsiri ! sasa hiyo machine inayo tafsiri automatically ali invent baba yako? we jamaa mpuuzi sana
 
Back
Top Bottom