Mchano juu ya Mkutano wa CUF & Speech Prof. Lipumba
1.Mkutano wa CUF leo Jangwani ulihudhuriawa na watu wengi na Prof. Lipumba alitoa hotuba.
2. Makamu wa Mwenyekiti CUF alisema kuwa kwa vile CCM & CHADEMA wanasema kuwa CUF ni chama cha Waislam basi Waislam wote Tanzania jiungeni na CUF. Pamoja na kwamba usemi huu unaweza kuwa ulitolewa as sarcasm hauna mashiko kwani ingetosha kusema nyote Wakristo kwa Waislam mnakaribishwa CUF. Kiongozi kakosa hekima kwa ku- reinforce kinatuhumiwa. Hii ni kama vile mtu aseme "kwa vile huwa nasingiziwa kuwa natembea na mke wa Fulani, sasa nasema nafanya kweli, Mrs. Fulani tuonane!
3. Prof. Lipumba kaongea issue za maana za kumpunguzia umaskini Mtz lakini ukweli hajatumia fursa ya sasa ya mabadiliko ya Katiba katika kuhamasisha wanachama chake juu ya mambo mengi muhimu yatakayo leta mabadiliko. Kaongea moja tu kuhusu kuwepo kipengelele kinachotamka Wananchi kufaidika moja kwa moja na rasilimali za nchi. Aidha haitoshi kuiombea roho ya marehemu Mwandishi wa habari na kisha mwishoni unamaliza kwa kusema tu kuwa Polisi mmeona sisi CUF tunapokutana hatuna fujo na tunakwenda Arusha kupeleka sera sio fujo / magomvi wala matusi.
Hii kauli imeshusha shule yake babu kubwa ya Uprofesa wa kweli katika uchumi aliyokuwa ameitoa katika kunyanyua uchumi wa nchi maana by implication alikuwa anasema tafuatayo: " SISI CUF SI KAMA CHADEMA WALETA FUJO WANAOSABABISHA POLISI KUTUMIA NGUVU HADI MAUAJI"
Mark my words!
Nimalizie kwa kusema kuwa VYAMA VYA UPINZANI VINAPOPATA NAFASI MBELE YA WANANCHI NA WAKAJIKITA KATIKA KUPIGANA VIJEMBE WAO KWA WAO, hakika mimi binafsi siwachukulii serious, ni kichefuchefu na mnaonekana vichekesho. Na ukweli ni kwamba unless mkubali kuunganisha nguvu au Katiba ibadilike na kukataa a simple majority Government; CCM itaendelea kuwatawala kwa muda mrefu ujao.
1.Mkutano wa CUF leo Jangwani ulihudhuriawa na watu wengi na Prof. Lipumba alitoa hotuba.
2. Makamu wa Mwenyekiti CUF alisema kuwa kwa vile CCM & CHADEMA wanasema kuwa CUF ni chama cha Waislam basi Waislam wote Tanzania jiungeni na CUF. Pamoja na kwamba usemi huu unaweza kuwa ulitolewa as sarcasm hauna mashiko kwani ingetosha kusema nyote Wakristo kwa Waislam mnakaribishwa CUF. Kiongozi kakosa hekima kwa ku- reinforce kinatuhumiwa. Hii ni kama vile mtu aseme "kwa vile huwa nasingiziwa kuwa natembea na mke wa Fulani, sasa nasema nafanya kweli, Mrs. Fulani tuonane!
3. Prof. Lipumba kaongea issue za maana za kumpunguzia umaskini Mtz lakini ukweli hajatumia fursa ya sasa ya mabadiliko ya Katiba katika kuhamasisha wanachama chake juu ya mambo mengi muhimu yatakayo leta mabadiliko. Kaongea moja tu kuhusu kuwepo kipengelele kinachotamka Wananchi kufaidika moja kwa moja na rasilimali za nchi. Aidha haitoshi kuiombea roho ya marehemu Mwandishi wa habari na kisha mwishoni unamaliza kwa kusema tu kuwa Polisi mmeona sisi CUF tunapokutana hatuna fujo na tunakwenda Arusha kupeleka sera sio fujo / magomvi wala matusi.
Hii kauli imeshusha shule yake babu kubwa ya Uprofesa wa kweli katika uchumi aliyokuwa ameitoa katika kunyanyua uchumi wa nchi maana by implication alikuwa anasema tafuatayo: " SISI CUF SI KAMA CHADEMA WALETA FUJO WANAOSABABISHA POLISI KUTUMIA NGUVU HADI MAUAJI"
Mark my words!
Nimalizie kwa kusema kuwa VYAMA VYA UPINZANI VINAPOPATA NAFASI MBELE YA WANANCHI NA WAKAJIKITA KATIKA KUPIGANA VIJEMBE WAO KWA WAO, hakika mimi binafsi siwachukulii serious, ni kichefuchefu na mnaonekana vichekesho. Na ukweli ni kwamba unless mkubali kuunganisha nguvu au Katiba ibadilike na kukataa a simple majority Government; CCM itaendelea kuwatawala kwa muda mrefu ujao.
​Historia inabainisha kuwa ukombozi wa Taifa letu ulianzia Dar-es-salaam na ukamalizikia Dar-es-salaam
Mitandao na maongezi ya watu mitaani yalikuwa yanabainisha na kututaka tuamini kuwa CUF haiko tena hai Tanzania bara.
Mkutano wa leo Jang'wani umetoa kitendawili kipya katika jamii na hasa watu wanaofuatilia siasa za Tanzania. katika hali ya kawaida kwa sasa ni vigumu kukitengua.
Ninadiriki kusema, wafuasi na wapenzi wengi wa vyama vingine vya kisiasa hasa CHADEMA kabla ya mkutano wa leo jang'wani waliamini kama CUF haiko tena Tanzania bara. Mkutano wa leo umewapa taswira mpya na wengi wao mpaka muda huu hawaamini wanachokiona katika television na picha mpaka wanadiriki kusema picha zimechakachuliwa.
Marumbano kwa sasa ni kati ya wapenzi na wanachama wa CUF na CHADEMA kutaka kuiaminisha jamii kipi ni chama chenye wafuasi wengi nchini.
CCM wanafurahia sana haya marumbano na ninaamini wanapenda yaendelee milele kwa vile kwao ni mtaji wa kisiasa. Kwa sasa wako kimya wakiangalia kwa mbali.
Waswahili walisema, vita vya panzi, furaha ya Kunguru na siasa za Tanzania siyo kama tuzijuavyo.
Kwa watu tusiowapenzi na wafuasi wa chama chochote cha kisiasa Tanzania tunazifurahia changamoto kama hizi kwa sababu ni kichocheo chanya cha maendeleo nchini.
Haya ni maoni yangu.
Leo Profesa katamka vitu sikutegemea kabisa, hizo ni kauli za watu kama Mtatiro, Kambaya na wengine. Hivi anaamini kabisa kwamba CDM, na siyo polisi ndiyo husababisha vifo kwenye mikutano? Au hii anasema kwa CDM tu na si chama chake?
Anasahau kijiji cha Shumba Mjini huko Zanzibar mwaka 1993 wakati polisi walipomuuwa mwanaCUF aliyekuwa akipandisha bendera ya chama chake katika ufunguzi wa tawi?
Anasahau January 2001 pale makumi ya wanaCUF walipouawa na risasi za polisi huko Pemba katika maandamano ya amani?
Kufuatana na kauli ya Prof leo -- ina maana matukio hayo yote mawili yalitokana na CUF kufanya fujo?
Anasahau alivyovunjwa mkono na polisi wakati anaresist kukamatwa katika kampeni za mwaka 2000? Bahati hakukutokea maafa, lakini ni CUF ndiyo walifanya fujo?
Inakuwaje leo hii Profesa anawaona polisi hawana hatia wakati vifo vinatokea mikutanoni, hatia ni vyama?
Nilikuwa naona kwamba Prof ni only a reasonable person amebakia katika CUF, kumbe sasa nina mashaka sana, naye ameanza kusombwa na siasa za kihovyo hovyo tu.