Kibwana Dachi tuombe radhi Wakatoliki

Kibwana Dachi tuombe radhi Wakatoliki

ustaadh Dach anaujua ukatoliki kuliko wakatoliki wenyewe
 
Last edited by a moderator:
chakufia nini

Mkuu nimekuelewa sana Na haujakosea.
Shaka langu halipo kwa watu waliokomaa kiimani, wao hayo Maneno kwao ni bure kabisa.

Lkn upande wa Pili kwa watu tunaokua kiroho, ambao bado tunapigana vita vya kiroho hii no shida.

Fikiria Mtu aliyeamua kumfuata YESU kwa sababu ya kuchoshwa Na ushirikina mtaani kwake kisha anaambia HAO ULIOJIAMBATANISHA NAO NI WASHIRIKINA, bila shaka hii roho itapotea kabisa.

Mwisho kabisa huyu Kidachi alichomaanisha ni zaidi ya ukatoliki, KAMA KUMUAMINI YESU NI USHIRIKINA BASI ALICHOMAANISHA NI KUWA UFUASI WA YESU NI USHIRIKINA
 
Last edited by a moderator:
Lakini mimi naona zoezi la uchaguzi wa Papa limekaa kishirikina vile.
 
Hua siyo msemaji sana humu jamvini japo ni mwanajamvi hili. Kiukweli sijapata nafasi ya kusikiliza hii radio kwa leo. Ila kama ni kweli kayasema haya basi atuombe radhi mara moja wakotoliki si tu kwa Tanzania bali kwa ulimwengu wa kikatoliki. Catholic church means 'universal Church'. Asipofanya hivyo tutaweka mambo hadharani kuhusu maisha na historia ya Muddy pamwe na kitabu chao. Subrini mone muda si mrefu.


Kamwaga sumu hata akiomba radhi yawezekana hiyo radhi isitoke moyoni, hivyo bora asamehewe.
 
NDUGU ZANGU DINI SI MANENO MENGI DINI SI MATANGAZO KM YA HAO NDUGU ZT DINI NI IMANI DINI NI MATENDO. Wasameheni, hawajui watendalo.
 
Wakatoliki ni watu waelewa hawana visasi hivyo mada km hizo hakuna haja ya kutuumiza wakatoliki nawaomba wakatoliki wote jivunieni ukristo wenu.
 
Inasikitisha sana kuona vijana tena wanaojiita wasomi wanaamka asubuhi nakuanza kushabikia udini usio na tija humu! Yaani mishipa imewasimama kabisa bila hata ya aibu! Huu si muda wakujadili udini humu hata kama wengi wetu tunadini kama unaona imekuuma sana chukua hatua stahiki ili kumuwajibisha nasi kutuletea fujo humu!Sasa unafikiri hata ukimtusi yy au dini yake utapata faida gani zaidi yakueneza udini?
Akhasante Mkuu Na Tupo Pamoja.
 
Hebu weka Audio na sisi tusikie kabla ya kutoa maoni yetu
 
Mara nyingi mtu akianza kukusema vibaya anakupenda anatafuta namna ya kuwa na wewe, mkaribisheni kwa upendo maana upendo ndio tunda la roho.
 
Dachi naona amevurugwa! Atuwache wakatoliki hatunaga bla bla kama za wengine, na ushasamehewa bwana dachi!
 
Wakatoliki huwa hawana visasi! Mfano mzuri ni Kardinali Pengo; hakulipa kisasi kwa Gwajima!
Akhsante Mkuu Na NASISITIZA Tena Hakusema Kuwa Wakristo Duniani Wanaamini USHIRIKINA Bali Nimemsikia Mwenyewe Kwa Masikio Yangu Mazima Na Akili Zangu Timamu Mtangazaji Kibwana Dachi Akisema Kuwa Dhehebu La WAKATOLIKI LINAAMINI SANA USHIRIKINA Na Naomba Kama Mimi GENTAMYCINE Nimemsingizia Huyu MTANGAZAJI Basi Naomba ISIFIKE Hata Saa 6 Mchana NILAANIKE au NIPATWE Na JAMBO Baya. Najiamini 100% Kwa NILICHOKIWASILISHA Hapa Kwenu.
 
chakufia nini

Nachelea kukubaliana na Mkatoliki wewe, ambaye huoni athari ya maneno aliyoyatoa huyo mtangazaji, mfano endapo mwanao angekuwa ni mmoja wa waliosikiliza kipindi hicho na akaaminishwa kwa kusikia kuwa unaofanyika Rome ni uchawi, na hana nafasi ya kumuuliza huyo aliyetamka, huoni kuwa ataamini hilo?

Je, ni nani ambaye atakanusha kama sio kweli kuwa ule ni ushirikina? Maadhara ya kuaminishwa kuwa Kanisa Katoliki ni washirikina wakubwa huoni athari yake? Kesho mkiwa kwenye jumuiya mnasali, akija mtu kuwaita nyie ni wachawi chekelea tu maana imani yako inakukataza na unafurahia kutukanwa
 
Last edited by a moderator:
Huo ukomavu unaoutaka wakuja kurusha ngumi na matusi humu jf utakusaidianini?
chakufia nini;

Tumsifu Yesu Kristo!;

Nina Hakika Huwezi ukamzidi Yesu Upendo! Umeona Upendo Aliowapa wale waliokuwa wanatukanisha Nyumba ya Baba yake?? Ni bakora tu...Yesu hakuwa legelege Mkuu!; ndilo Tatizo kubwa tulilo nalo Wafuasi wake, tunapenda Ufufuko lakini Msalaba tunatafuta sababu...
 
Last edited by a moderator:
Kuamini kwamba uchawi upo ni TOFAUTI kabisa na kuamini katika uchawi. Hoja hapa ni kwamba mleta mada amemsikia mtangazaji mmoja akisema kwamba RC wanaamini uchawi. Na kama nia yake ingekuwa kusema 'wanaamini kuwa kuna uchawi', basi ingekuwa wakristu wote au watu wote wanaotumia biblia, lakini yeye amesikika akisema Roman Catholic

Nadhani ni kiswahili tu,
sidhani kwamba walikua wanasema Nyie mnaloga!
 
Back
Top Bottom