Kibwana Dachi tuombe radhi Wakatoliki

Kibwana Dachi tuombe radhi Wakatoliki

Nachelea kukubaliana na Mkatoliki wewe, ambaye huoni athari ya maneno aliyoyatoa huyo mtangazaji, mfano endapo mwanao angekuwa ni mmoja wa waliosikiliza kipindi hicho na akaaminishwa kwa kusikia kuwa unaofanyika Rome ni uchawi, na hana nafasi ya kumuuliza huyo aliyetamka, huoni kuwa ataamini hilo?

Je, ni nani ambaye atakanusha kama sio kweli kuwa ule ni ushirikina? Maadhara ya kuaminishwa kuwa Kanisa Katoliki ni washirikina wakubwa huoni athari yake? Kesho mkiwa kwenye jumuiya mnasali, akija mtu kuwaita nyie ni wachawi chekelea tu maana imani yako inakukataza na unafurahia kutukanwa

Hayo yote yaliyosemwa hayajabadilisha imani ya Kanisa Katoliki wala imani ya Wakatoliki. Hebu angalia mfano wa kiongozi wetu Pengo. Mbona alifanyiwa udhalilishaji mkubwa sana na Gwajma? Uliona alichojibu? Hakumtaka hata Gwajma aombe radhi zaidi ya kutamka amemsamehe. Hivi unadhani angeanzisha ligi na Gwajma angekuwa anatetea imani? Lile la Gwajma halikuwa zaidi ya hili?
 
Utulivu ni silaha kubwa sana unaposhambuliwa na adui wa nje na hata wa ndani. Shambulizi likitoke nje, usitoe nafasi kwa nafsi yako kujumuika na adui kwenye kivuli cha kisasi kukupatia adha kubwa zaidi.

Kanisa Katoliki ni taasisi kubwa kuliko zote hapa ulimwenguni. Iwe ni kwa idadi ya watu au hata resources. Ili uonekane na ww upo, kulishmbulia kanisa katoliki ni hatua ya kwanza. Lkn ukweli ni kwamba litendelea kuwepo regardless f that.

Juzi juzi hapa aliibuka the so called 'Nabii' na kuongea maneno ya hovyo hovyo juu ya kiongozi wa Kanisa Katoliki nchini, tena ni ya kukera hasa. Kanisa halikushugulika naye kabisa, aliachwa kwa kuwa 'he is so low to be discussed by the CC of Tanzania'. Niwakumbushe kuwa, watu ambao wangepaswa kumjadili 'mfufua watu' huwa wako bize na uratibu washughuli za maendeleo ya jamii (shule, zahanati, vuo vya ufundi n.k)

Kibwana Dachi asamehewe kwa hitilafu zake za kifikra na chuki. Kama alivyoumbuka 'Nabii Mfufuaji' katika unabii wake wa mwisho aliufanya kwa CCM kwenye siasa kumuinua 'Joshua' wa kuivusha Tanzania kwenda nchi ya ahadi, na huyu ataumbuka kwa yake.
 
chakufia nini;

Hoja na majibu safi kabisa.

Mkatoliki gani kafundishwa kulipa kisasi au kutosamehe? Hawa ndio wale wanaochafua amani kwa sababu tu ya kusaka haki ya "kuchinja". Kama una hasira, itakuwaje ukisikiliza mihadhara pale Manzese?

Wakatoliki wala hawahangaishwi na mambo madogo.
 
Kama hii ndio mada yake ya maana basi cpati picha hizo nyingine zipoje!!!!
Angalia, katika Kiswahili hakuna neno "DHEHEBU", badala yake kuna "MADHEHEBU". Liwe moja, ni madhehebu. Yawe mawili au 100 ni madhehebu tu. Aaache Wakatoliki waendelee kuishi na ndugu zao wote -wa madhehebu yote kwa amani na utulivu. Uvumilivu ni sifa mama ya mwamini wa kweli.
 
Sio kosa lenu Bali ni ile kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa.. Niwaulize, hasa mnaokazania msamaha!; Hivi mnaelewa nini Yesu aliposema Muwe wapole kama huwa lakini werevu kama nyoka!? Unaona msamaha alio-utoa Yohana Mbatizaji kwa kumkemea Herodi kwamba ni mzinzi aache uzinzi wake...Yohana akakatwa kichwa!

Umeona Yohana alivyobeba Msalaba wake na kumfuata Yesu? Wee upo humu umebakia samehe, samehe! Hata Hujainuka kukemea uongo aliotamka kwa kinywa chake!; tusijipe moyo Kama hatujui umemuangamiza yeye na wewe pia!...
 
kwani wewe umetumwa na kanisa katoliki?

au wewe ni kanisa katoliki? huoni kama unafanya makosa kama aliyoyafanya kibwana coz hata kibwana hakutumwa na watu wadini yake mimi naona tusubirie tamko la kanisa katoliki kuliko sisi kujichukulia hatua ya kutoa matamko haya coz yanaweza ya kuendeleza chuki ya mtu mmoja dhidi ya mwingine.
 
Sio kosa lenu Bali ni ile kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa.. Niwaulize, hasa mnaokazania msamaha!; Hivi mnaelewa nini Yesu aliposema Muwe wapole kama huwa lakini werevu kama nyoka!? Unaona msamaha alio-utoa Yohana Mbatizaji kwa kumkemea Herodi kwamba ni mzinzi aache uzinzi wake...Yohana akakatwa kichwa!

Umeona Yohana alivyobeba Msalaba wake na kumfuata Yesu? Wee upo humu umebakia samehe, samehe! Hata Hujainuka kukemea uongo aliotamka kwa kinywa chake!; tusijipe moyo Kama hatujui umemuangamiza yeye na wewe pia!...

Jitazame ni mambo yapi yanakushughulisha kisha utagundua kuwa huna sababu ya kuwa kama 'wao'. Tungelilelewa kwa chuki na kulipizana visasi, tusingekuwa taasisi kubwa. Sisemi kwamba alichoongea ni kizuri au kimenifurahisha, ila ni wazi hakinisumbui kwa kuwa kimesemwa na yeye.

Kama kauli hiyo ingetolewa na Askofu wa Kanisa Katoliki, ningelikuwa concerned. Be cool!
 
Kama ameyasema kweli weledi umempungua. Tukiacha udini pembeni nadhani tasnia ya habari ina utaratibu wa kiungwana sana pale mtu anapopotoka. KUOMBA RADHI.
 
Huo ukomavu unaoutaka wakuja kurusha ngumi na matusi humu jf utakusaidianini?

Matusi na ngumi gani wewe? Hivi mwizi kumwmbia wewe ni mwizi unaona unamtupia ngumi na kumtukana!? Unachekesha sana...Usiiwekee mipaka Injili Mkuu, hata humu viumbe wa Mungu wamo inatupasa tuwafanye Wana wa Mungu...
 
Chief, naona Ukatoliki wako ni wa kimwili zaidi. Ukatoliki haufundishi hivi....jipange tena kiimani chief.

ni mimi Mkatoliki mwenzio.

 
Chief, naona Ukatoliki wako ni wa kimwili zaidi. Ukatoliki haufundishi hivi....jipange tena kiimani chief.

ni mimi Mkatoliki mwenzio.


Utakuwa muoga tu huna lolote! Huyu jamaa hajakosea lolote, la msingi huyo Kibwana aombe radhi tu! Huyo mtu ana dini yake, nini kimemtuma kuja kusema yale asiyoyajua! Huo moshi mweupe na mweusi ndio kaona uchawi?! Yaliyoko ndani ya dini yake hayamtoshi?
 
Hayo yote yaliyosemwa hayajabadilisha imani ya Kanisa Katoliki wala imani ya Wakatoliki. Hebu angalia mfano wa kiongozi wetu Pengo. Mbona alifanyiwa udhalilishaji mkubwa sana na Gwajma? Uliona alichojibu? Hakumtaka hata Gwajma aombe radhi zaidi ya kutamka amemsamehe. Hivi unadhani angeanzisha ligi na Gwajma angekuwa anatetea imani? Lile la Gwajma halikuwa zaidi ya hili?
Issue ya Gwajima kwa Pengo hailingani na hii, utaratibu wa kumchagua papa ni hatua ya juu ya Kanisa na waumini husali na kufunga hadi papa apatikane, sasa leo tuamini ule ni ushirikina? Jambo hili halipaswi kudhihakiwa.
 
Ile post ya Ninth Circle ya Dr. Kevin D. Anett, alipost nani humu jukwaani? somebody Nyerere eeeh!!! nikidhani tu kama Kibwana Dachi anasema kile ambacho duniani kinasemwa na hata humu jukwaani kinasemwa pia.
 
Issue ya Gwajima kwa Pengo hailingani na hii, utaratibu wa kumchagua papa ni hatua ya juu ya Kanisa na waumini husali na kufunga hadi papa apatikane, sasa leo tuamini ule ni ushirikina? Jambo hili halipaswi kudhihakiwa

Tutetee imani na sio dhehebu.
 
Back
Top Bottom