Kiboko ya Lowassa Afariki Dunia

Jamani, Madaha ha"kupambana" kama nionavyo hizo post hapo juu, mtowa mada anasema Serenge alipambana. Sasa mtowa mada hebu tuweke sawa hapa, ulikurupuka? au hawa wachangiaji wengine wanaongea issue tofauti?
 
Sielewi kwa nini huyo mkuu aliyefariki alikuwa ni kiboko cha Lowasa. Mimi naona alikuwa ni mnyonge wa Lowasa.
 
Mbona sioni dalili ya hayo mapambano zaidi ya hiyo post inayoonesha kanali madaha alichemsha
 
Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza Luteni Kanali Mstaafu Serenge Mrengo amefariki Dunia.
Source; Habari Leo:hug:
Bibikuku ebu tuambie ni vipi huyu bwana alikuwa kiboko ya Lowasa?
Habari yako imekuja na utata!
 
Kikwete bwana, yeye anakwenda kunywa dawa Loliondo Wakuu wa Wilaya anawapereka India!! huu sio unyama kweli?
 
Bibikuku,

Kama kumbukumbu zangu zinanipa vizuri kauli hiyo ilitolewa na Col Madaha aliyekuwa DC wa Nymagana wakati huo. Siyo Serenge(RIP).

Pengine mwenye uhakika 100% atusaidie.

ndivyo hivyo alikuwa kanali mstaafu madaha,na sasa ni DC mstaafu.
 
Jamani, Madaha ha"kupambana" kama nionavyo hizo post hapo juu, mtowa mada anasema Serenge alipambana. Sasa mtowa mada hebu tuweke sawa hapa, ulikurupuka? au hawa wachangiaji wengine wanaongea issue tofauti?

Mkuu ni Madaha, Kapotolo hapo juu ame-confirm hili kwa kuweka na source kabisa ya Daily News; Friday,September 28, 2007 @00:02 na mwandishi ni JOHN KULEKANA.
 
Bibikuku,

Kama kumbukumbu zangu zinanipa vizuri kauli hiyo ilitolewa na Col Madaha aliyekuwa DC wa Nymagana wakati huo. Siyo Serenge(RIP).

Pengine mwenye uhakika 100% atusaidie.

Aliyem-blast lowassa hadharani ni Mhe. Madaha. Mimi nilishuhudia tukio hilo. It was kindumbwendumbwe. Tena basi wakati huo lowassa alikuwa ametokea mkoani Kigoma kwenye ziara ya kiserikali ambapo aliwabana mbavu maDC wengi mbele ya wananchi. Ndipo alipofika Mwanza akakumbana na kisiki cha mpingo Mzee Madaha. Lowassa alitamani ardhi ipasuke azame na kuficha uso wake kwa aibu.

Kilichotokea ni kwamba lowassa alikataa ripoti ya Mzee Madaha kwa maelezo kuwa ni ripoti mbaya sana na imejaa uwongo. Aliiponda ripoti kwa hasira mbele ya wananchi. Mzee Madaha baada ya kuona amedharirishwa nae alijibu mapigo kwa kumweleza lowassa kamba hawezi kumfundisha kazi. Yeye ni mzoefu kuliko lowassa na amekuwa DC tangu lowassa akiwa mwanafunzi miaka 24 iliyopita na miaka yote alikuwa akiandika ripoti zake hivyo hivyo''. Wakati anaongea maneno hayo, wananchi walikuwa wanamshangilia.

Huyo mwandishi wa Daily News alichakachua hiyo habari ili kulinda heshima ya waziri mkuu.
 
DC ampinga Lowassa hadharani

Friday, 28 September 2007 08:26


na Sitta Tumma, Mwanza
KATIKA hali isiyo ya kawaida, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, jijini Mwanza, Kanali Peter Madaha, ameonyesha jeuri ya kumpinga waziwazi Waziri Mkuu, Edward Lowassa, baada ya kuikataa taarifa ya wilaya hiyo.
Mkuu huyo wa wilaya alilazimika kumjibu Lowassa hadharani na papo hapo, baada ya kuikataa taarifa hiyo ya wilaya na kisha akamweleza mkuu huyo wa wilaya kuwa uongozi wake ni dhaifu.
Malumbano hayo yaliyozua gumzo kwa viongozi na watendaji wa serikali yalitokea jana, saa 3:45 asubuhi, Ikulu ndogo jijini hapa wakati mkuu huyo wa wilaya akitoa taarifa ya maendeleo ya wilaya hiyo.
Katika taarifa hiyo, Lowassa alionekana kutoridhishwa nayo hususan katika sekta ya elimu na kilimo, ambayo ilielezwa kuwa na udanganyifu mkubwa hata waziri mkuu kulazimika kuikataa na kusema mkuu huyo wa wilaya hana uongozi thabiti katika wilaya yake.
“Huwezi ukaniambia mimi sina uongozi imara...mimi ni kiongozi na nina miaka 24 nikiwa kama kiongozi wa Serikali ya Tanzania. Mimi ni kiongozi, tena mzuri sana,” alisema DC huyo kwa kujiamini na kwa sauti ya juu.
Katika hali hiyo, Lowassa hakuweza kubishana naye wala kumjibu lolote, isipokuwa alisisitiza kuikataa taarifa hiyo ya wilaya na kuonyesha kusikitishwa na kushangazwa na kauli ya DC huyo.

Source: Tanzania Daima: Friday, 28 September 2007 08:26
 
Angalieni hiyo news imeandikwa na Gazeti gani!!
Kumbukumbu zangu zinaonyesha Kanali Madaha Alimwambia EL kuwa amefanya utumishi ulotukuka kipindi cha Nyerere Mwinyi na Mkapa. EL anastahili kujifunza toka kwake na si yeyeMadaha ajfunze toka kwa EL. kwa hivyo EL hana haki hata moja ya kumkosoa zaidi ya kusikiliza kisha kuendelea na kampeni zake za urais. Baada ya Kumtoa nishai , Mzee madaha alijaa na kufanya wote walokuwa ukumbini kupigwa na butwaa kama dk 10 hivi wasiamini kilichosemwa na madaha hadi meya alipoahirisha kikao ilhali kulikuwa na m/kiti [meya hakuwa mwenyekiti bali mjumbe alekaa high table]
 
Back
Top Bottom