Kibiblia: Namna wanaojiita manabii, mitume, makuhani wanavyopotosha watu

Swahili AI

JF-Expert Member
Mar 2, 2016
6,212
46,836
Leo nataka niwaonyeshe namna ambavyo wakujiita manabii, makuhani, mitume na wengineo wanavyo walaghai wakristo.
Nitafafanua kibiblia kabisa.

Kwanza chanzo cha upotoshaji wa waaumini umetajwa katika Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa;
Ni kweli kabisa, wanaangamia kiuchumi, kifikra na kwa kila namna.

Sasa kwanini nayasema haya?
Kitabu cha Matayo 10, Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka mengi na tofauti {soma, nitaweka kwa uchache hapa}. Moja ya agizo alilowapa kuanzia mstari wa 7 ni: Na mnapokwenda, hubirini mkisema, ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia;

Agizo namba 1 ni juu ya kurudi kwake kitu ambacho hawafanyi wakiwa kwenye majukwaa yao zaidi ya kuhubiri mafanikio ambapo ni kinyume na andiko
Mathayo 6:33
"Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa." Sina maana tusufanye kazi.

Kisha neno likaendelea kusema:
8 Waponyeni wagonjwa, wafufueni wafu, watakaseni wenye ukoma, wafukuzeni pepo. Mmepokea bure, toeni bure. 9 Msichukue dhahabu, wala fedha wala sarafu za shaba katika mikanda yenu.
Tena akasisitiza kwamba wasichukue mali kutoka kwa hao watu kwa maana wamepewa bure.

Sasa inakuaje mnapangiwa mpaka viwango vya kutoa sadaka ili uonane na huyo nabii/mtume/mchungaji? Au kuuziwa bidhaa fulani ili ukapate uponyaji?

Amkeni wandugu. Biblia imeweka wazi kila kitu ila kwakuwa watu hawasomi wanasubiri kupata miujiza, mtaendelea kupigwa na kupigwa kila siku.
 
Rheinard Bonnke ndo alileta hii kitu afrika. Imagine alifanya waafrika zaidi ya 70M kuokoka.

Halafu nilifatilia mission zake za tz naona alizifanyia mbeya, itakua ndo maana mbeya ipo hivi ilivyo.

Kuna kina mwakasege, geordavie wamejifunzia kutoka nje, ila huyo mzungu nadhani ndo alichochea mambo.
 

Hes 12:6​

Kisha akawaambia, Sikizeni basi maneno yangu; Akiwapo nabii kati yenu, Mimi, BWANA, nitajifunua kwake katika maono, Nitasema naye katika ndoto.

Manabii wa kweli na watumishi wengine kama mitume, wachungaji, walimu et al wapo, ila kumbuka;

1 Yoh 4:1-2​

Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu.
 
Kisha neno likaendelea kusema:
8 Waponyeni wagonjwa, wafufueni wafu, watakaseni wenye ukoma, wafukuzeni pepo. Mmepokea bure, toeni bure. 9 Msichukue dhahabu, wala fedha wala sarafu za shaba katika mikanda yenu. Tena akasisitiza kwamba wasichukue mali kutoka kwa hao watu kwa maana wamepewa bure.
Naomba kutajiwa majina ya watumishi wa Mungu kutoka kwenye biblia na nje ya biblia waliowahi kuwafufua wafu.
 
Leo nataka niwaonyeshe namna ambavyo wakujiita manabii, makuhani, mitume na wengineo wanavyo walaghai wakristo.
Nitafafanua kibiblia kabisa.

Kwanza chanzo cha upotoshaji wa waaumini umetajwa katika Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa;
Ni kweli kabisa, wanaangamia kiuchumi, kifikra na kwa kila namna.

Sasa kwanini nayasema haya?
Kitabu cha Matayo 10, Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka mengi na tofauti {soma, nitaweka kwa uchache hapa}. Moja ya agizo alilowapa kuanzia mstari wa 7 ni: Na mnapokwenda, hubirini mkisema, ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia;

Agizo namba 1 ni juu ya kurudi kwake kitu ambacho hawafanyi wakiwa kwenye majukwaa yao zaidi ya kuhubiri mafanikio ambapo ni kinyume na andiko
Mathayo 6:33
"Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa." Sina maana tusufanye kazi.

Kisha neno likaendelea kusema:
8 Waponyeni wagonjwa, wafufueni wafu, watakaseni wenye ukoma, wafukuzeni pepo. Mmepokea bure, toeni bure. 9 Msichukue dhahabu, wala fedha wala sarafu za shaba katika mikanda yenu.
Tena akasisitiza kwamba wasichukue mali kutoka kwa hao watu kwa maana wamepewa bure.

Sasa inakuaje mnapangiwa mpaka viwango vya kutoa sadaka ili uonane na huyo nabii/mtume/mchungaji? Au kuuziwa bidhaa fulani ili ukapate uponyaji?

Amkeni wandugu. Biblia imeweka wazi kila kitu ila kwakuwa watu hawasomi wanasubiri kupata miujiza, mtaendelea kupigwa na kupigwa kila siku.
MK254 Yale mambo yetu Shakahola
 
Rheinard Bonnke ndo alileta hii kitu afrika. Imagine alifanya waafrika zaidi ya 70M kuokoka.

Halafu nilifatilia mission zake za tz naona alizifanyia mbeya, itakua ndo maana mbeya ipo hivi ilivyo.

Kuna kina mwakasege, geordavie wamejifunzia kutoka nje, ila huyo mzungu nadhani ndo alichochea mambo.
Mkuu humjui Bonnke vizuri, huwezi kumweka Bonnke kwenye kapu moja na Geordavie.

Halafu kihistoria uamsho wa kipentekoste Tanzania ambao ulianzia Mbeya haukuletwa na Bonnke. Japo aliwahi kuhubiri Mbeya.
 
Mkuu humjui Bonnke vizuri, huwezi kumweka Bonnke kwenye kapu moja na Geordavie.

Halafu kihistoria uamsho wa kipentekoste Tanzania ambao ulianzia Mbeya haukuletwa na Bonnke. Japo aliwahi kuhubiri Mbeya.
Asante 🤝
Yaani gordave nae umuweke na Bonke,u must be kidding 🤣
Eti Mwakasege na gordave uwaweke kapu Moja🤔😀
No thank you!
Watu hawajui historia za uamsho kabisa
 
Wamekazania sana mafundisho ya sadaka kama jambo muhimu sana wakati sadaka ilikuwa na umuhimu kabla ya Yesu Kristo ambapo watu walitakiwa kutoa ndege, mnyama au nafaka kwa makuhani kwa ajili ya sadaka ya kuteketeza ili wapate kusamehewa madhambi.

Je, kusisitiza utoaji wa sadaka hata baada ya Yesu mwenyewe kujitoa sadaka, ni jambo sahihi?

Mimi naona badala ya kuita sadaka wangeiita michango kwa ajili ya kuendesha huduma, kwa sababu maana ya sadaka ni kafara inayotolewa kwa ajili ya kupata msamaha. Sasa baada ya sadaka ya Yesu msalabani, ni sadaka ipi tena ambayo bado ina nguvu?​
 
Back
Top Bottom