Kibanda: Naliona anguko la Zitto Kabwe!

Kibanda: Naliona anguko la Zitto Kabwe!

Status
Not open for further replies.
maamuzi aliyoyafanya zitto mwaka 2009 yakuamua kujitoa ndiyo yanayomgharimu leo hii,nadhani huu ni wakati wakuruhusu demokrasia iamue ndani ya vyama vyetu vya siasa.bila shaka zitto hayuko tayari kurudia makosa aliyokwisha yafanya.lets democracy decide.

Yani lazima niwe mjumbe wa mkutano mkuu wa CHADEMA ili huyu mnafiki asipate ata kura 5.
 
maamuzi aliyoyafanya zitto mwaka 2009 yakuamua kujitoa ndiyo yanayomgharimu leo hii,nadhani huu ni wakati wakuruhusu demokrasia iamue ndani ya vyama vyetu vya siasa.bila shaka zitto hayuko tayari kurudia makosa aliyokwisha yafanya.lets democracy decide.
If I were you, I would have never opened my big mouth any more and spit anything out more that what I have vomited kwenye kadamnasi ya jf, mpaka baada ya vikao vyenu vya nidhamu vya ndani!.

Kwa ushauri tuu, bora ujinyamazie dada yangu, utatunza heshima yako hiyo kidogo iliyobakia!, hapo ulipo, tayari umebaki na nguo ya ndani ya chini tuu, naomba ujisetiri kwa kujikalia kimya, ili na hiyo usije ukavuliwa ukabaki ...wa mnyama!. Mwangalie mwenzako ZZK, kajinyamazia kimya!. Hata vuvuzela saa8 naye kimya!. Bora jikalie kimya kwanza ujue hatma yako ndipo uendeleze uhuru wako wa kutumia your freedom of expression!, kwa sasa Chadema inajitahidi kuwapunguza the "Lukosi type!", najua mko wengi, ila anayeondoka kimya kimya, ndiye anayeondoka kwa heshima, kuliko kupiga kelele ili kuny.a kambi ndipo atimke!.

Ni ushauri tuu!.

Pasco.
 
JK hajawahi kuwa naibu katibu mkuu wa CCM katika umri wake wote achilia mbali miaka 25! Pia hakupata unaibu waziri akiwa na umri wa miaka33 kwani katika umri huo alikuwa hajawa hata mbunge, amekuwa naibu waziri mwaka 1987 akiwa na miaka 37 hivyo wewe nakuchukulia kama mwongo tu na wtu wakujue hivyo basi
Kibanda kwenye makala hii umekuwa upande mmoja wa Mbowe,unasema kuwa Zitto ni kijana na unakubali amesimamia mambo makubwa ya kisiasa nchini, pia amekuwa naibu Katibu mkuu kwanini ashindwe kusimamia kazi ya uenyekiti wakati Mtendaji mkuu wa chama ni katibu mkuu? Zitto awe na subira kwani hujui kuwa muda uliopo ndio wako na muda ujao si wako? una maana vijana ni taifa la Kesho? JK amekuwa naibu Katibu mkuu wa CCM akiwa na miaka 25.

amekuwa naibu waziri kwenye wizara nzito ya nishati akiwa na miaka 33.kama ZITTO ana SHINE bungeni kwanini ashindwe uenyekiti wa Chadema?
 
Ahsante mkuu Pasco,

Niseme tu kwamba hakuna kijana aliweza kuvutia wengi ktk miaka ya hiv karibuni kama Zitto, binafsi bado sijaona Zitto alikosa nini CHADEMA mpaka aanze kubadilika, kipindi kile mzee wetu Edwin Mtei aliposema kwamba "WE CAN NO CHOOSE A MAN FROM NO WHERE"( if am not mistaken).

alikuwa amemaanisha kwani anajua changamoto za kiuongozi sasa hebu fikiri leo hii Zitto ndio angekuwa mwenyekiti wa CHADEMA na tabia zake hizi sijui chama kingekuwa wapi.

Zitto jua kwamba mpaka muda huu umekwisha poteza imani mbele ya watu wote makini hapa nchini.

Shardcole@Tabora1

zitto ana kadi moja atapotezaje imani kwa wananchi?
 
Zitto katubu zambi zako kwa viongozi wako na uache unafiki sasa..
Vilevile wahenga wetu walisema, mtu makini hujifunza kutokana na makosa yake. Ni vyema wote walioteleza waombe radhi na kutorudia makosa.
 
Last edited by a moderator:
Naona unaendelea kumvua nguo zitto kwa utetezi wa namna hii tena kwa kutumia hoja ya card!

Hebu tuthibitishie pasi na shaka kuwa mtu akiwa na card ya chama kimoja hawezi kuwa msaliti? Let me tell you card inaweza ikawa si hoja kabisa bali matendo ya mtu binafsi yanaweza yakawa hukumu tosha!

Nakushauri Juliana Shonza ni bora unyamaze maana hata kumtetea zitto huwezi maana una kuja na hoja dhaifu sana:

Na hapa ni ushahidi mwingine kuwa hoja ya card imetoka wapi!

Hakika wewe binti ni mweupe sana upstair!

Pole sana unazidi kuchimba shimo badala ya kufukia!

zitto ana kadi moja atapotezaje imani kwa wananchi?
 
Last edited by a moderator:
Pasco, huu ni ushauri mzuri sana, kuna kipindi ambapo watu wanafanya "re-organisation and re-construction", ni bora Juliana Shonza akae kimya na wajipande upya, ZZK ni mjanja sana, lazima atakuja na single ya kujiweka sawa ndani ya CDM, only time will tell, let us wait and see!
 
Du, kuna watu humu tumetoka mbali na ZZK!, nikukukmbuka nilivyomfagilia hapa, na hizi tuhuma zinazoelekezwa kwake saa hizi, naamini ni za uongo, na nitaendelea kusimama nae!.
Mpaka sasa bado huamini?
You have passed beyond Thomas's unbelieved threshold.
Hata siku Zitto akiri au kutubu huenda bado hautaamini.

Kwani na wewe alipelekwa kwa mganga kuapishwa ili usimsaliti Zitto au unaogopa panya wa kwenu kufa?
 
naungana kabisa na Bw Kibanda. Zito ingawa katiba inakuruhusu pasi na shaka lakini wewe bado kabisa kukomaa kisiasa anahitaji takriban miaka mitano zaidi ya kujijenga kisiasa kabla ya kuamua kugombea uongozi wa juu kabisa wa chama.

Zito kama kweli unataka uongozi wa juu kabisa katika siasa unahitaji upate uzoefu zaidi. uwe na subra.
lakini ukiangalia kwa upande mwingine inaweza ikawa ni ujanja wa kisiasa wa chadema kuonyesha kuwa Mbowe nae kapata mpinzani.

uchaguzi uliopita alipotaka kumtest mbowe kwenye position hii hii wazee wa chama walimwambia hayo maneno unayomwambia wewe leo,sasa atakua mtu wa kusubiri mpaka lini?mnyonge mnyongeni...mi naona tatizo la zitto ni dini yake na mahali atokako-kigoma
 
mti wenye matunda ndio unaopigwa mawe.
Binti bado hujachelewa msamaha bado upo, nenda katubu kwa viongozi wako usamehewe.

Wenzako kadhaa wameshaanza kutubu makosa yao na wanaelekea kusamehewa.

Kwani na wewe uliapishwa kwa mganga ili usimsaliti?

Kwani una ndoto za uFirst Lady? jamaa anao mademu kibao tena wakali ile mbaya, sidhani kama wewe ni mkali kuwapita wale wenzako.

Try to think big and broader!!!
 
uchaguzi uliopita alipotaka kumtest mbowe kwenye position hii hii wazee wa chama walimwambia hayo maneno unayomwambia wewe leo,sasa atakua mtu wa kusubiri mpaka lini?mnyonge mnyongeni...mi naona tatizo la zitto ni dini yake na mahali atokako-kigoma
Kwanini anang'ang'ania huko Chadema kama anahisi hawamtaki kwa sababu ya dini yake na mkoa wake?

Yeye ni mtu maarufu, ana uwezo wa kisiasa mkubwa sana, anapendwa na watu wengi sana ikiwemo WanaCCM, sasa kwanini asianzishe chama chake na kisha kufanikisha malengo yake anayoyataka kisiasa?
 
Jee kama hao wanao sadikiwa kwamba wametumiwa na zito ...na wao iwe wametumiwa waseme waliyo yasema ili kulinda masklahi ya wengine...hapa kuna tuhuma...ingekuwa vema CDM wakaunda tume kuchunguza malumbano haya...tume ya watu huru.....lakini haya yanayo tokea CDM yametokea hata Cuf...na wao waliunda kamati kuchunguza mfano wakati wa Nyaruba, mapalala, na hata mgombea maarufu wa Temeke ..Hiza...waliwachunguza wakaitwa wajieleze wakashindwa wakafukuzwa kwenye chama
na hivi karibuni Mh Hamad Rashid naye alikuwa na tuhuma...walimwita ajieleze kwenye kamati ya maadili ya chama chao akagoma kwenda walimpa muda wa kuomba radhi alishindwa kufanya hivyo..akafikuzwa CUF
Sasa haya ya Zito tunayassikia zaidi hapa jamii forum na wakati mwengine kutoka na vijana wa chama hicho,,,,Taarifa ya juzi ya Mbowe alikanusha kuwepo mgogoro wa uongozi....lakini hapa ukisoma karibu kila siku kuna topic mpya inamhusu zito...jee kunani?
inawezekana kuna makundi tayari ndani ya CDM ....na ndio haya yakupigana vijembe na kupondana humu forum....sisi wengine tunaona haya ya ajabu vijana wa chama kupigana vijembe nje ya vikao huu si mwelekeo mzuri...kaeni na ongeeni kama kuna sintofahamu imalizeni..hata kama ni kufukuza kila anaeleta fitina...kufanya hivyo ndio mnaimarisha chama ...ila kulea fitina hizi ...mwisha wake ni mgawanyiko...
Macos

Naheshimu mawazo na mtazamo wako. Hofu yangu ni kuwa kama umekuja kumtetea sidhani kama umefaulu maana mtu mwenye akili akisoma maneno yako vizuri ataona unamwangamiza Zitto kwa utetezi huu.
Unazidi kuthibitisha tuhuma ambazo hazipo katika tuhuma zinazozunguka sasa. So sad!

Pasco, nadhani bandiko la kibanda lilihitimisha vizuri tu. Wengi tumekuwa tukimsihi kuwa na subira, apunguze jazba na awe more professional. Kwa bahati mbaya hasikii wala haoni.

Kwa tuhuma hizi za uhujumu, anguko lake kisiasa ni dhahiri kama halipo njiani.
Tuhuma zinazomkabili zinamuondolea sehemu kubwa sana ya sifa za uongozi hata kama ni kiongozi kwa mwonekano.

Nafasi aliyo nayo ya kujirudi au kuzuia uharibu ''damage control'' ni yeye kujitoa kimaso maso bila msaada wa vijana ambao kisiasa ni wachanga na kifikra ni weupe sana.

Zitto anapaswa kuachia ngazi katika uongozi kwa sasa ikiwa ni hatua ya kuwajibika na ku-reset the button.

Jitihada zake za kutaka kuona nyumba inaunguka kwa msemo wa 'namwaga mboga mwaga ugali'' zinaweza zizifanikiwe kwasababu washirika wake hawaonekani kuwa watu makini.

Ningemshauri Zitto awaase vijana wake wasimwage mpunga kwenye kuku wengi na kukaa kimya ni busara na msaada kwake

The only window of opportunity ni yeye kuachia ngazi katika uongozi.

Aachie ngazi kwa sababu amedhihirisha betrayal, amepoteza trust na moral authority yake imekuwa severely compromized. Hizi jitihada za kuwatumia immature political gangs kumsafisha zitahitimisha safari yake mapema sana.

Kiwango na umaarufu aliofikia Zitto halafu uangalie timu aliyokuwa anafanya nayo kazi kichini chini ni ushahidi kuwa pamoja na vision na mission anazoonekane kuwa nazo, politically ni immature na ameonyesha poor judgement kama kiongozi. Zitto anahitaji muda akomae kisiasa na hili litabaki kuwa donda ndugu.

Zitto, kama unakipenda chama chako na unapenda ustawi wa taifa hili, ni wakati muafaka kabisa uweke masilahi yako pembeni kwa kuachia uongozi ili uwe mfano wa vijana shupavu wanaokubali kuwajibika.

Kwasasa huna moral ya kumyooshea kidole Mizengo Pinda ajiuzulu kwa kutowawajibisha mawaziri maana wewe hujafanya hivyo.
 
maamuzi aliyoyafanya zitto mwaka 2009 yakuamua kujitoa ndiyo yanayomgharimu leo hii,nadhani huu ni wakati wakuruhusu demokrasia iamue ndani ya vyama vyetu vya siasa.bila shaka zitto hayuko tayari kurudia makosa aliyokwisha yafanya.lets democracy decide.

Juliana wewe ni nyoka wa mdimu
 
Kibanda jitolee kumshauri Zitto, nahisi bado ananafasi nyingine, he is still young and strong anachotakiwa akubali yaishe
 
mti wenye matunda ndio unaopigwa mawe.

Wewe dada nakushauri nikiwa kama kakio haya mambo yaache kaa pembeni jifunze. Zitto is too far and you just prepare to start yaani hata hujaanza. Mtafute Fatuma Maghimbi ujifunze yaliyomkuta. Usijiharibie maisha mapema dogo
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom