Kete ya mwisho ya Maalim Seif ni kuunda chama kipya cha Siasa!

Hivi Mbowe alipo pokea mlungula wa Lowassa, aliwatoa?. Au mnapiga propaganda free kwa kua nyie hamjui matumizi ya pesa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ok tukubali kuwa cdm imempokea fisadi mmoja yaani lowasa ,ccm wamebaki wafisadi wangapi? Cdm ndiyo pekee inatakiwa kuwa watakatifu? Nyie ccm mnapoteza muda kuwadanganya watz, mnafikiri tumesahau list of shame?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu mgogoro unaofukuta ndani ya CUF kwa ugomvi kati ya Katibu Mkuu halali wa CUF Mhe. Maalimu Seifu na Mwenyekiti fake Prof(njaa) Haruna Lipumba umelenga kuimaliza CUF kisiasa.
Kwa msaada wa Serikali na vyombo vya ulinzi na Usalama CUF halali lazima iangamie ili isiendelee kuisumbua CCM ya Serikali ya Awamu ya 5. Figisu zote zinazoendelea lengo ni Maalimu Seifu na lazima amalizwe kisiasa kabla ya 2020!!

Serikali wanajua kabisa kuwa Uchaguzi Mkuu wa 2015 Maalimu Seifu alishinda kwa kishindo na kama Uhuru,Haki na Demokrasia ya kweli vingetamalaki na kuzingatiwa na ZEC hivi leo Maalimu Seifu angelikuwa yuko Ikulu ya Zanzibar akiongoza Visiwa vya Marashi ya Pemba.

Kwa hali inavyoelekea imebakia kete moja tu kwa Maalimu Seifu ambayo itamwokoa kisiasa nayo ni KUANZISHA CHAMA KIPYA CHA SIASA. Lazima CUF halali wajifunze kwa Wapinzani Kenya kina Raila Odinga, William Ruto, Uhuru Kenyata na wengineo. Kwamba jina la Chama sio hoja. Leo hakuna KANU tena wala ODM badala yake tuna JUBILEE na NASA na siasa zinakwenda! Jambo la msingi hapa ni WATU au UMMA ulio nyuma yako. Nina hakika kama Maalimu ataondoka leo na kuachana na CUF ambayo Lipumba ameamua kuisambaratisha na kuunda Chama kingine kwa Jina lolote kwa ajili ya kuwakomboa Wazanzibari na Wazanzibara toka utawala kandamizi wa CCM umma wote utakuwa nyuma yake.

Kwa kufanya hivo Wabunge wote wa Kuchaguliwa CUF watakuwa wamepoteza uanachama wa CUF kama wale wa kuteuliwa(Special Seats) walivyopoteza juzi baada ya kutimuliwa na CUF ya Lipumba. Kitakachofuata ni Tume ya Uchaguzi kuitisha Uchaguzi na Wabunge wote wa Kuchaguliwa CUF watarudi Bungeni kwa jina la Chama kipya na ushindi mkubwa. Kwa mtaji huo CUF ya Lipumba watakuwa hawana Wabunge wa Kuchaguliwa na kwa mantiki hiyo hawatakuwa na Wabunge wa Viti Maalumu na hawatakuwa na RUZUKU tena.CUF watabaki na Lipumba na Sakaya na ndiyo itakuwa hitima ya CUF Tanzania.

Huu mtego wa CCM wa kumpa presha Seif aunde chama kipya ama kuhamia chama kingine (na kinatajwa CHADEMA hasahasa), eti tu kumkimbia Prof mjinga asiejielewa ni wa kitoto na kila mtu mwenye zake akili timamu anauelewa na kuona kabisa haiwezekani !!

Kwangu mimi labda ninaweza kukuelewa wewe mleta mada kama ungesema, hili la kuunda ama kuhama chama, Bwana Maalim Seif alifanye siku chache kabla ya uchaguzi mkuu wa 2020 na ni iwapo tu yeye mwenyewe atakiri kuwa kashindwa kuipata haki yake ya ushindi wa uchaguzi mkuu wa oktoba 2015!!
 
Wateule,
Umechangia kwa umakini kiasi kwamba umenishawishi nikubaliane na wewe kwa Maalimu kujiunga na CHADEMA.
My question is: Je, Maalimu Seifu na Waunguja na Wapemba watakuwa tayari kuhamia CHADEMA? Lakini pia tusisahu kuna sumu au dhana moja potofu sana ilishajengwa kuhusu Udini kwenye vyama vya siasa!!. Kwamba CHADEMA ni chama cha Kikristo na CUF ni chama cha Kiislamu. Sasa kwa watu ambao hawasomi katikati ya mistari kwa ndugu zetu wa Visiwani wakisikia Ukristo basi wanajua ni kuingilia imani zao na hii inawatoa nje!

Itakuwa ni wakti mwafaka sasa kwa Viongozi wakuu wa CHADEMA kukaa na Maalimu, kina Salim Mwalimu kuwaelimisha Wazalendo wote walioko Visiwani ili waelewe hilo somo na wajue adui yao ni nani. Ukristo ni just DINI wala haina issue kwenye Politics. Adui namba 1 wa Wazanzibar ni CCM na huyu ndo anatakiwa ashambuliwe toka kona zote ili kumsambaratisha kama KANU ya Moi ilivyopotea huko Kenya!!!

Kwahiyo ccm ni chama cha dini gani ? Haya wakate kujiunga chadema watawaliwe na ccm katoliki.

Siasa zinabadilika watambue hilo ,hata wakisusia uchaguzi watawapa ccm tu maushindi ya burebure
 
Mzalendo 2015,
Wapo kweli namba ya Wazanzibari wanaoamini hivyo. Lakini, hizi propaganda za udini (na pacha wake "amani") zinakuzwa zaidi na CCM ili kuwapunguzia CUF na upinzani kwa ujumla nguvu ya kuwapa wafuasi.

Kama Seif, atahamia CHADEMA kama tulivyoshauri hapa, basi nina imani kabisa hizo propaganda za udini hazitofua dafu, na Wazanzibari watakuwa tayari kumuunga mkono Seif kwa maslahi ya nchi yao ambayo imegeuzwa koloni la CCM (wala sio la Tanganyika kama inavyoaminika).

Wazanzibari wa Pemba na wengi wa Unguja kama matokeo ya 2015 yalivyoonyesha, wameshajua adui yao mkubwa ni CCM na wala sio kingine chochote. Watakuwa pamoja na CHADEMA na maalim. Bado haitokuwa rahisi kuitoa CCM madarakani kutokana na hila zake za kila aina, lakini itakuwa kwenye wakati mgumu sana, na uwezekano wa kuizika kama KANU utakuwa ni mkubwa.

Asante.
Acheni kuwapotosha wana CUF kwa janja janja. Infact hiki kitu ndo CDM miaka yote wanaomba kitokee ili wajijenge Kisiasa Zanzibar sehemu ambayo hawakubaliki hata na panya. Kwa maalim kujiunga na CDM ni kujimaliza kabisa kisiasa na kuipa nguvu mpya CDM. Kwa ushawishi alionao maalim ni mara mia akaunda chama chake kuliko kujitumbukiza kwenye genge la wafanyabishara wanaowaza kuongeza ruzuku kila siku.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maalimu hawezi kuhamia chadema, kwa sababu zifuatazo. Mosi, sera za chadema na Cuf zinatofautiana, ataacha sera alizopigania kwa miaka yote hiyo na aanze kupigania sera za Cdm? Haiwezekani, mpaka sasa najua maalimu anaichukia cdm kwani asili ya mgogoro wa cuf ni cdm kupitia ukawa, najua hili mtalipinga ila lina ukweli, kwani tafsiri yake ni kuwa tangu mwanzo nia ya cdm ilikuwa ni kuiua cuf. Cuf ina kaunasaba ka dini ya Kiislamu zanzibar na bara, cdm ina kaunasaba ka kiruthel tangu kauli ile ya ni zamu yetu, hivyo maalimu kujiunga na cdm ni sawa na kubatizwa, hivyo hatakubali pamoja na wafuasi wake, mi naona hana jingine ila tu kuanzisha chama kingine, japo hakitakiki. Ila itanailaani sana cdm kwa kuivuruga cuf

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maalimu hawezi kuhamia chadema, kwa sababu zifuatazo. Mosi, sera za chadema na Cuf zinatofautiana, ataacha sera alizopigania kwa miaka yote hiyo na aanze kupigania sera za Cdm? Haiwezekani, mpaka sasa najua maalimu anaichukia cdm kwani asili ya mgogoro wa cuf ni cdm kupitia ukawa, najua hili mtalipinga ila lina ukweli, kwani tafsiri yake ni kuwa tangu mwanzo nia ya cdm ilikuwa ni kuiua cuf. Cuf ina kaunasaba ka dini ya Kiislamu zanzibar na bara, cdm ina kaunasaba ka kiruthel tangu kauli ile ya ni zamu yetu, hivyo maalimu kujiunga na cdm ni sawa na kubatizwa, hivyo hatakubali pamoja na wafuasi wake, mi naona hana jingine ila tu kuanzisha chama kingine, japo hakitakiki. Ila itanailaani sana cdm kwa kuivuruga cuf

Sent using Jamii Forums mobile app

umumbati,
Nikuambia ule msemo wa Bashite mwenzio RC Dar. Kwamba wewe ni moja ya VICHAA TUNAOHANGAIKA NAO!
Wewe hakika utakuwa ni kichaa. Hivi mpaka sasa anayetaka kuua CUF ni Prof. Lipumba au CHADEMA?? Najua wewe ni CCM na kwako wewe kuwagombanisha CUF na CHADEMA au CUF na LIPUMBA kwako ni tija na mtaji!!!
Najua CCM hamtaki kuiona CUF, hamtaki kuiona CHADEMA wala hamtaki kuona UKAWA na upinzani wa aina yoyote Tanzania. Any Great Thinker knows that for sure.
 
Kwahiyo ccm ni chama cha dini gani ? Haya wakate kujiunga chadema watawaliwe na ccm katoliki.

Siasa zinabadilika watambue hilo ,hata wakisusia uchaguzi watawapa ccm tu maushindi ya burebure

CCM ni chama cha MASHETANI, ni chama cha MAGAIDI. Shetani hana dini anaingia popote iwe kanisani(katoliki,lutheri,anglikana,sabato n.k), msikitini(shia,sunni,bohra n.k.) lakini pia kwenye tunguli CCM ni twende kazi.
 
Hata maji Marefu ni Profesa. Yaani Lipumba ni dola kumtumia ndiko kunakomfanya aonekane na watu kama nyie kumuona ni Profesa na siyo "Pro-pesa" lakini yeye mwenyewe akiachwa na Maalim ni mwepesi kuliko unyoya wa kuku.

Na lengo la CCM kumtumia Lipumba sidhani kama litafanikiwa kwani ni yeye mwisho wa siku ndiye atakayedharauliwa!
Mkuu,Sefu anatafunwa na karma ya kumpora Mapalala CUF, usihangaike.
 
Maalimu hawezi kuhamia chadema, kwa sababu zifuatazo. Mosi, sera za chadema na Cuf zinatofautiana, ataacha sera alizopigania kwa miaka yote hiyo na aanze kupigania sera za Cdm? Haiwezekani, mpaka sasa najua maalimu anaichukia cdm kwani asili ya mgogoro wa cuf ni cdm kupitia ukawa, najua hili mtalipinga ila lina ukweli, kwani tafsiri yake ni kuwa tangu mwanzo nia ya cdm ilikuwa ni kuiua cuf. Cuf ina kaunasaba ka dini ya Kiislamu zanzibar na bara, cdm ina kaunasaba ka kiruthel tangu kauli ile ya ni zamu yetu, hivyo maalimu kujiunga na cdm ni sawa na kubatizwa, hivyo hatakubali pamoja na wafuasi wake, mi naona hana jingine ila tu kuanzisha chama kingine, japo hakitakiki. Ila itanailaani sana cdm kwa kuivuruga cuf

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaonekana una hofu baada kutambua kuwa mnaweza kuua CUF, lakini sio mitazamo ya kimaendeleo ya kina Maalim Seif. Upinzani sasa ndo utaongezeka nguvu. Hila na mabavu ya ccmserikali vitasaidia kujenga upinzani makini zaidi, kama ilivyokuwa kwa ANC wakati wa Afrika ya kusini ya makaburu.
 
Ushauri wa bure kwa Maalim na Chadema (Wakifanya mapema kabla ya 2019 ni bora zaidi).

1. Maalim akiondoka CUF kwa staili nzuri "definetly" Cuf itakufilia mbali. Wenyewe kule pemba wanasema "kafu nmaalim na Maalim nkafu".
2. Maalim kuhamia Chadema sio karata mbaya lakini hapa lazima "win-win situation" itumike. Kuna mambo lazima wakubaliane hasa ya kikatiba.
3. Kutokana na "mentality" ya wafuasi wa Cuf ni vyema, ikiwa Maalim atahamia Chadema ni vyema kukazaliwa JINA jipya la chama. Hii itaziba midomo ya wote wenye "akili ndogo".
4. Maalim afanye "referendum" wanachama wanaomuunga mkono wapige kura, ikishindikana hata mkutano mkubwa wa hadhara kwaajili ya kuomba ridhaa kwa wanachama wake kuhamia Chadema. Hii itafanya kuhamia kwake kuwe kumeridhiwa na wafuasi wake.
5. Ikiwa atakubali kuhamia, basi iwe shughuli kubwa ya kitaifa (ifanyike Airtime ya kutosha).

Maalim "Focus" iwe 2020, hizi story za kuwa sijui utapewa Uraisi kabla ya lini Sijui achana nazo, zinakupotezea muda wa kufanya mambo muhimu.
 
Huu mgogoro unaofukuta ndani ya CUF kwa ugomvi kati ya Katibu Mkuu halali wa CUF Mhe. Maalimu Seifu na Mwenyekiti fake Prof(njaa) Haruna Lipumba umelenga kuimaliza CUF kisiasa.
Kwa msaada wa Serikali na vyombo vya ulinzi na Usalama CUF halali lazima iangamie ili isiendelee kuisumbua CCM ya Serikali ya Awamu ya 5. Figisu zote zinazoendelea lengo ni Maalimu Seifu na lazima amalizwe kisiasa kabla ya 2020!!

Serikali wanajua kabisa kuwa Uchaguzi Mkuu wa 2015 Maalimu Seifu alishinda kwa kishindo na kama Uhuru,Haki na Demokrasia ya kweli vingetamalaki na kuzingatiwa na ZEC hivi leo Maalimu Seifu angelikuwa yuko Ikulu ya Zanzibar akiongoza Visiwa vya Marashi ya Pemba.

Kwa hali inavyoelekea imebakia kete moja tu kwa Maalimu Seifu ambayo itamwokoa kisiasa nayo ni KUANZISHA CHAMA KIPYA CHA SIASA. Lazima CUF halali wajifunze kwa Wapinzani Kenya kina Raila Odinga, William Ruto, Uhuru Kenyata na wengineo. Kwamba jina la Chama sio hoja. Leo hakuna KANU tena wala ODM badala yake tuna JUBILEE na NASA na siasa zinakwenda! Jambo la msingi hapa ni WATU au UMMA ulio nyuma yako. Nina hakika kama Maalimu ataondoka leo na kuachana na CUF ambayo Lipumba ameamua kuisambaratisha na kuunda Chama kingine kwa Jina lolote kwa ajili ya kuwakomboa Wazanzibari na Wazanzibara toka utawala kandamizi wa CCM umma wote utakuwa nyuma yake.

Kwa kufanya hivo Wabunge wote wa Kuchaguliwa CUF watakuwa wamepoteza uanachama wa CUF kama wale wa kuteuliwa(Special Seats) walivyopoteza juzi baada ya kutimuliwa na CUF ya Lipumba. Kitakachofuata ni Tume ya Uchaguzi kuitisha Uchaguzi na Wabunge wote wa Kuchaguliwa CUF watarudi Bungeni kwa jina la Chama kipya na ushindi mkubwa. Kwa mtaji huo CUF ya Lipumba watakuwa hawana Wabunge wa Kuchaguliwa na kwa mantiki hiyo hawatakuwa na Wabunge wa Viti Maalumu na hawatakuwa na RUZUKU tena.CUF watabaki na Lipumba na Sakaya na ndiyo itakuwa hitima ya CUF Tanzania.
Kweli kabisa umenena vyema 100%.
 
Seif sharrif hamad nafikiri hii ss ni zamu yake.anachofanyiwa ni kile aliwafanyia wenzie ambao ni waanzilishi wa cuf.mzee mapalala alifanyiwa mbovu na hamad.msobi mageni hamad rashid profesa safari.orodha ni ndeefu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usitake kupotosha wala kuchanganya mambo hapa. Hiyo 2015 cuf na cdm zilishiriki uchaguzi huo ndani ya ukawa na huko visiwani cdm waliachiwa nadhani jimbo moja alilokuwa Salim Mwalimu basi. Na mgombea wa urais kwa tiketi ya muungano huko visiwani alikuwa ni Lowassa na yeye alipata kura nyingi kuliko hata Magu. Kwa sasa iwapo Cuf waligoma kushiriki uchaguzi wa marudio ni wazi wameshapoteza sana, hivyo wamuache Lipumba atambe kupitia mgongo wa serekali kwa muda mfupi sana. Inafahamika Cuf ya Seif ndio yenye nguvu kwa wananchi hivyo uchaguzi ujao Lipumba atabaki na ofisi tu kwani uwezo wa kupata kura hana, na hilo analifahamu. Hata haya mapendekezo ya Seif kuhamia cdm wanaccm hawayapendi maana wanajua Lipumba hana watu, na iwapo Seif atahamia cdm sasa itaimarika zaidi kwani itakuwa na nguvu bara na visiwani.

mkuu ilikuwaje ccm ikapata wabunge wengi ili hali alishinda lowassa?
 
Back
Top Bottom