Kete ya mwisho ya Maalim Seif ni kuunda chama kipya cha Siasa!

Mzalendo2015

JF-Expert Member
Aug 14, 2012
6,697
9,048
Huu mgogoro unaofukuta ndani ya CUF kwa ugomvi kati ya Katibu Mkuu halali wa CUF Mhe. Maalimu Seifu na Mwenyekiti fake Prof(njaa) Haruna Lipumba umelenga kuimaliza CUF kisiasa.
Kwa msaada wa Serikali na vyombo vya ulinzi na Usalama CUF halali lazima iangamie ili isiendelee kuisumbua CCM ya Serikali ya Awamu ya 5. Figisu zote zinazoendelea lengo ni Maalimu Seifu na lazima amalizwe kisiasa kabla ya 2020!!

Serikali wanajua kabisa kuwa Uchaguzi Mkuu wa 2015 Maalimu Seifu alishinda kwa kishindo na kama Uhuru,Haki na Demokrasia ya kweli vingetamalaki na kuzingatiwa na ZEC hivi leo Maalimu Seifu angelikuwa yuko Ikulu ya Zanzibar akiongoza Visiwa vya Marashi ya Pemba.

Kwa hali inavyoelekea imebakia kete moja tu kwa Maalimu Seifu ambayo itamwokoa kisiasa nayo ni KUANZISHA CHAMA KIPYA CHA SIASA. Lazima CUF halali wajifunze kwa Wapinzani Kenya kina Raila Odinga, William Ruto, Uhuru Kenyata na wengineo. Kwamba jina la Chama sio hoja. Leo hakuna KANU tena wala ODM badala yake tuna JUBILEE na NASA na siasa zinakwenda! Jambo la msingi hapa ni WATU au UMMA ulio nyuma yako. Nina hakika kama Maalimu ataondoka leo na kuachana na CUF ambayo Lipumba ameamua kuisambaratisha na kuunda Chama kingine kwa Jina lolote kwa ajili ya kuwakomboa Wazanzibari na Wazanzibara toka utawala kandamizi wa CCM umma wote utakuwa nyuma yake.

Kwa kufanya hivo Wabunge wote wa Kuchaguliwa CUF watakuwa wamepoteza uanachama wa CUF kama wale wa kuteuliwa(Special Seats) walivyopoteza juzi baada ya kutimuliwa na CUF ya Lipumba. Kitakachofuata ni Tume ya Uchaguzi kuitisha Uchaguzi na Wabunge wote wa Kuchaguliwa CUF watarudi Bungeni kwa jina la Chama kipya na ushindi mkubwa. Kwa mtaji huo CUF ya Lipumba watakuwa hawana Wabunge wa Kuchaguliwa na kwa mantiki hiyo hawatakuwa na Wabunge wa Viti Maalumu na hawatakuwa na RUZUKU tena.CUF watabaki na Lipumba na Sakaya na ndiyo itakuwa hitima ya CUF Tanzania.
 
Mtamuelewa Lipumba kwa nini kaitwa Profesa
Hata maji Marefu ni Profesa. Yaani Lipumba ni dola kumtumia ndiko kunakomfanya aonekane na watu kama nyie kumuona ni Profesa na siyo "Pro-pesa" lakini yeye mwenyewe akiachwa na Maalim ni mwepesi kuliko unyoya wa kuku.

Na lengo la CCM kumtumia Lipumba sidhani kama litafanikiwa kwani ni yeye mwisho wa siku ndiye atakayedharauliwa!
 
Huu mgogoro unaofukuta ndani ya CUF kwa ugomvi kati ya Katibu Mkuu halali wa CUF Mhe. Maalimu Seifu na Mwenyekiti fake Prof(njaa) Haruna Lipumba umelenga kuimaliza CUF kisiasa.
Kwa msaada wa Serikali na vyombo vya ulinzi na Usalama CUF halali lazima iangamie ili isiendelee kuisumbua CCM ya Serikali ya Awamu ya 5. Figisu zote zinazoendelea lengo ni Maalimu Seifu na lazima amalizwe kisiasa kabla ya 2020!!

Serikali wanajua kabisa kuwa Uchaguzi Mkuu wa 2015 Maalimu Seifu alishinda kwa kishindo na kama Uhuru,Haki na Demokrasia ya kweli vingetamalaki na kuzingatiwa na ZEC hivi leo Maalimu Seifu angelikuwa yuko Ikulu ya Zanzibar akiongoza Visiwa vya Marashi ya Pemba.

Kwa hali inavyoelekea imebakia kete moja tu kwa Maalimu Seifu ambayo itamwokoa kisiasa nayo ni KUANZISHA CHAMA KIPYA CHA SIASA. Lazima CUF halali wajifunze kwa Wapinzani Kenya kina Raila Odinga, William Ruto, Uhuru Kenyata na wengineo. Kwamba jina la Chama sio hoja. Leo hakuna KANU tena wala ODM badala yake tuna JUBILEE na NASA na siasa zinakwenda! Jambo la msingi hapa ni WATU au UMMA ulio nyuma yako. Nina hakika kama Maalimu ataondoka leo na kuachana na CUF ambayo Lipumba ameamua kuisambaratisha na kuunda Chama kingine kwa Jina lolote kwa ajili ya kuwakomboa Wazanzibari na Wazanzibara toka utawala kandamizi wa CCM umma wote utakuwa nyuma yake.

Kwa kufanya hivo Wabunge wote wa Kuchaguliwa CUF watakuwa wamepoteza uanachama wa CUF kama wale wa kuteuliwa(Special Seats) walivyopoteza juzi baada ya kutimuliwa na CUF ya Lipumba. Kitakachofuata ni Tume ya Uchaguzi kuitisha Uchaguzi na Wabunge wote wa Kuchaguliwa CUF watarudi Bungeni kwa jina la Chama kipya na ushindi mkubwa. Kwa mtaji huo CUF ya Lipumba watakuwa hawana Wabunge wa Kuchaguliwa na kwa mantiki hiyo hawatakuwa na Wabunge wa Viti Maalumu na hawatakuwa na RUZUKU tena.CUF watabaki na Lipumba na Sakaya na ndiyo itakuwa hitima ya CUF Tanzania.
Mwezi jan 2017 alisema hautapita Mwezi atakuwa amekabidhiwa utawala Zanzibar. Mbona kimya??
 
Mwezi jan 2017 alisema hautapita Mwezi atakuwa amekabidhiwa utawala Zanzibar. Mbona kimya??

That is a joke!
Nani unategemea amkabidhi Utawala ilhali CCM waliompora ushindi kwa hila bado wameng'ang'ania Ikulu kama luba?
 
Nia ya serekali ya CCM ni kutaka kuvinyonga vyama vyote vya upinzani lakini katika harakati zake za kutaka kuviua vyama vya upinzani,itajikuta ina ibua chama kimoja cha upinzani chenye nguvu kubwa zaidi ya hivi vilivyopo, kwa kuwa sio wote watakao kubali kujiunga na CCM baada ya vyama vyao kuuawa,wataamua kujiunga na Chama kimoja cha upinzani ambacho kitakuwa na nguvu kubwa na kumaliza utitiri mkubwa wa vyama vya upinzani vilivyopo hivi sasa.
 
To be frank, kwa siasa za Visiwani ni ngumu sana kwa CHADEMA kumbeba Maalim Seifu.
Ushahidi wa hili ni Uchaguzi wa 2015, angalia CUF alipata majibo mangapi na CHADEMA walipata majimbo mangapi under UKAWA.

Hiyo ni kwasababu CUF bado ilikuwepo na mgombea wake alikuwa Maalim Seif kwa upande wa ZNZ. Ingawa alikuwa anawakilisha UKAWA kama mgombea, chama chake kilikuwa bado ni CUF na Wazanzibar walijua hivyo. Leo akiamua kuiacha CUF iliyonajisiwa na Lipumba, na kuhamia CHADEMA, basi huo utakuwa ni mwanzo wa safari mpya ya kisiasa yenye nguvu mara dufu ya 2015 kwa Seif. Wazanzibar watakuwa wamepata sababu ya wazi ya kuiunga mkono CHADEMA visiwani humo bila shaka.

Itakuwa imekula kwa Lipumba na mfadhili wake CCM, kwani itakuwa ngumu sana kuanzisha njama mpya za kumuangamiza kisiasa ili asidai haki yake ya 2015 kule ZNZ.

Mimi sio mwanachama wala shabiki wa CHADEMA. Lakini, kwa kuzingatia kwamba CHADEMA ndio chama kikuu cha upinzani Tanzania bara kwasasa, naunga mkono kwa Seif kuhamia huko ili kuendeleza mapambano dhidi ya CCM. Kuhamia kwa Seif CHADEMA, UKAWA ya ukweli (isiyokuwa na vizingiti vya kisheria kama ile ya uchaguzi wa 2015, ambayo ilimlazimu Duni Haji kujiunga CHADEMA ili awe mgombea mwenza wa Lowassa) itakuwa imezaliwa rasmi.
 
Ninavyoona Option kwa Maalim Seif sa hvi
1. Asubir 2018/2019 Ajiunge na Chadema ili abebwe na vugu vugu la Uchaguz kipind hicho Asijiunge sasa maana thaman yake by 2019 itakuwa imeshuka
2. Atengenze chama chake kingine with the Plans for 2025 maana figisu figisu mpka za kusajiliwa kwa 2020 hataweza, Ila option 2 umri itakuwa kikwazo kwake.
 
Hiyo ni kwasababu CUF bado ilikuwepo na mgombea wake alikuwa Maalim Seif kwa upande wa ZNZ. Ingawa alikuwa anawakilisha UKAWA kama mgombea, chama chake kilikuwa bado ni CUF na Wazanzibar walijua hivyo. Leo akiamua kuiacha CUF iliyonajisiwa na Lipumba, na kuhamia CHADEMA, basi huo utakuwa ni mwanzo wa safari mpya ya kisiasa yenye nguvu mara dufu ya 2015 kwa Seif. Wazanzibar watakuwa wamepata sababu ya wazi ya kuiunga mkono CHADEMA visiwani humo bila shaka.

Itakuwa imekula kwa Lipumba na mfadhili wake CCM, kwani itakuwa ngumu sana kuanzisha njama mpya za kumuangamiza kisiasa ili asidai haki yake ya 2015 kule ZNZ.

Mimi sio mwanachama wala shabiki wa CHADEMA. Lakini, kwa kuzingatia kwamba CHADEMA ndio chama kikuu cha upinzani Tanzania bara kwasasa, naunga mkono kwa Seif kuhamia huko ili kuendeleza mapambano dhidi ya CCM. Kuhamia kwa Seif CHADEMA, UKAWA ya ukweli (isiyokuwa na vizingiti vya kisheria kama ile ya uchaguzi wa 2015, ambayo ilimlazimu Duni Haji kujiunga CHADEMA ili awe mgombea mwenza wa Lowassa) itakuwa imezaliwa rasmi.

Wateule,
Umechangia kwa umakini kiasi kwamba umenishawishi nikubaliane na wewe kwa Maalimu kujiunga na CHADEMA.
My question is: Je, Maalimu Seifu na Waunguja na Wapemba watakuwa tayari kuhamia CHADEMA? Lakini pia tusisahu kuna sumu au dhana moja potofu sana ilishajengwa kuhusu Udini kwenye vyama vya siasa!!. Kwamba CHADEMA ni chama cha Kikristo na CUF ni chama cha Kiislamu. Sasa kwa watu ambao hawasomi katikati ya mistari kwa ndugu zetu wa Visiwani wakisikia Ukristo basi wanajua ni kuingilia imani zao na hii inawatoa nje!

Itakuwa ni wakti mwafaka sasa kwa Viongozi wakuu wa CHADEMA kukaa na Maalimu, kina Salim Mwalimu kuwaelimisha Wazalendo wote walioko Visiwani ili waelewe hilo somo na wajue adui yao ni nani. Ukristo ni just DINI wala haina issue kwenye Politics. Adui namba 1 wa Wazanzibar ni CCM na huyu ndo anatakiwa ashambuliwe toka kona zote ili kumsambaratisha kama KANU ya Moi ilivyopotea huko Kenya!!!
 
Huu mgogoro unaofukuta ndani ya CUF kwa ugomvi kati ya Katibu Mkuu halali wa CUF Mhe. Maalimu Seifu na Mwenyekiti fake Prof(njaa) Haruna Lipumba umelenga kuimaliza CUF kisiasa.
Kwa msaada wa Serikali na vyombo vya ulinzi na Usalama CUF halali lazima iangamie ili isiendelee kuisumbua CCM ya Serikali ya Awamu ya 5. Figisu zote zinazoendelea lengo ni Maalimu Seifu na lazima amalizwe kisiasa kabla ya 2020!!

Serikali wanajua kabisa kuwa Uchaguzi Mkuu wa 2015 Maalimu Seifu alishinda kwa kishindo na kama Uhuru,Haki na Demokrasia ya kweli vingetamalaki na kuzingatiwa na ZEC hivi leo Maalimu Seifu angelikuwa yuko Ikulu ya Zanzibar akiongoza Visiwa vya Marashi ya Pemba.

Kwa hali inavyoelekea imebakia kete moja tu kwa Maalimu Seifu ambayo itamwokoa kisiasa nayo ni KUANZISHA CHAMA KIPYA CHA SIASA. Lazima CUF halali wajifunze kwa Wapinzani Kenya kina Raila Odinga, William Ruto, Uhuru Kenyata na wengineo. Kwamba jina la Chama sio hoja. Leo hakuna KANU tena wala ODM badala yake tuna JUBILEE na NASA na siasa zinakwenda! Jambo la msingi hapa ni WATU au UMMA ulio nyuma yako. Nina hakika kama Maalimu ataondoka leo na kuachana na CUF ambayo Lipumba ameamua kuisambaratisha na kuunda Chama kingine kwa Jina lolote kwa ajili ya kuwakomboa Wazanzibari na Wazanzibara toka utawala kandamizi wa CCM umma wote utakuwa nyuma yake.

Kwa kufanya hivo Wabunge wote wa Kuchaguliwa CUF watakuwa wamepoteza uanachama wa CUF kama wale wa kuteuliwa(Special Seats) walivyopoteza juzi baada ya kutimuliwa na CUF ya Lipumba. Kitakachofuata ni Tume ya Uchaguzi kuitisha Uchaguzi na Wabunge wote wa Kuchaguliwa CUF watarudi Bungeni kwa jina la Chama kipya na ushindi mkubwa. Kwa mtaji huo CUF ya Lipumba watakuwa hawana Wabunge wa Kuchaguliwa na kwa mantiki hiyo hawatakuwa na Wabunge wa Viti Maalumu na hawatakuwa na RUZUKU tena.CUF watabaki na Lipumba na Sakaya na ndiyo itakuwa hitima ya CUF Tanzania.
maalim alizooea kudoea vyama vya wenzie
 
Wateule,
Umechangia kwa umakini kiasi kwamba umenishawishi nikubaliane na wewe kwa Maalimu kujiunga na CHADEMA.
My question is: Je, Maalimu Seifu na Waunguja na Wapemba watakuwa tayari kuhamia CHADEMA? Lakini pia tusisahu kuna sumu au dhana moja potofu sana ilishajengwa kuhusu Udini kwenye vyama vya siasa!!. Kwamba CHADEMA ni chama cha Kikristo na CUF ni chama cha Kiislamu. Sasa kwa watu ambao hawasomi katikati ya mistari kwa ndugu zetu wa Visiwani wakisikia Ukristo basi wanajua ni kuingilia imani zao na hii inawatoa nje!

Itakuwa ni wakti mwafaka sasa kwa Viongozi wakuu wa CHADEMA kukaa na Maalimu, kina Salim Mwalimu kuwaelimisha Wazalendo wote walioko Visiwani ili waelewe hilo somo na wajue adui yao ni nani. Ukristo ni just DINI wala haina issue kwenye Politics. Adui namba 1 wa Wazanzibar ni CCM na huyu ndo anatakiwa ashambuliwe toka kona zote ili kumsambaratisha kama KANU ya Moi ilivyopotea huko Kenya!!!
Wateule,
Umechangia kwa umakini kiasi kwamba umenishawishi nikubaliane na wewe kwa Maalimu kujiunga na CHADEMA.
My question is: Je, Maalimu Seifu na Waunguja na Wapemba watakuwa tayari kuhamia CHADEMA? Lakini pia tusisahu kuna sumu au dhana moja potofu sana ilishajengwa kuhusu Udini kwenye vyama vya siasa!!. Kwamba CHADEMA ni chama cha Kikristo na CUF ni chama cha Kiislamu. Sasa kwa watu ambao hawasomi katikati ya mistari kwa ndugu zetu wa Visiwani wakisikia Ukristo basi wanajua ni kuingilia imani zao na hii inawatoa nje!

Itakuwa ni wakti mwafaka sasa kwa Viongozi wakuu wa CHADEMA kukaa na Maalimu, kina Salim Mwalimu kuwaelimisha Wazalendo wote walioko Visiwani ili waelewe hilo somo na wajue adui yao ni nani. Ukristo ni just DINI wala haina issue kwenye Politics. Adui namba 1 wa Wazanzibar ni CCM na huyu ndo anatakiwa ashambuliwe toka kona zote ili kumsambaratisha kama KANU ya Moi ilivyopotea huko Kenya!!!

Mzalendo 2015,
Wapo kweli namba ya Wazanzibari wanaoamini hivyo. Lakini, hizi propaganda za udini (na pacha wake "amani") zinakuzwa zaidi na CCM ili kuwapunguzia CUF na upinzani kwa ujumla nguvu ya kuwapa wafuasi.

Kama Seif, atahamia CHADEMA kama tulivyoshauri hapa, basi nina imani kabisa hizo propaganda za udini hazitofua dafu, na Wazanzibari watakuwa tayari kumuunga mkono Seif kwa maslahi ya nchi yao ambayo imegeuzwa koloni la CCM (wala sio la Tanganyika kama inavyoaminika).

Wazanzibari wa Pemba na wengi wa Unguja kama matokeo ya 2015 yalivyoonyesha, wameshajua adui yao mkubwa ni CCM na wala sio kingine chochote. Watakuwa pamoja na CHADEMA na maalim. Bado haitokuwa rahisi kuitoa CCM madarakani kutokana na hila zake za kila aina, lakini itakuwa kwenye wakati mgumu sana, na uwezekano wa kuizika kama KANU utakuwa ni mkubwa.

Asante.
 
Hata maji Marefu ni Profesa. Yaani Lipumba ni dola kumtumia ndiko kunakomfanya aonekane na watu kama nyie kumuona ni Profesa na siyo "Pro-pesa" lakini yeye mwenyewe akiachwa na Maalim ni mwepesi kuliko unyoya wa kuku.

Na lengo la CCM kumtumia Lipumba sidhani kama litafanikiwa kwani ni yeye mwisho wa siku ndiye atakayedharauliwa!
Unataka kulinginisha Ziro na Profesa!?
 
Back
Top Bottom