Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,409
- 31,394
Kesi ya ugaidi ya Mwenyekiti wa Chadema Mbowe na Wenzake imeondolewa mahakamani
Si sahihi kusema kesi imekwisha, Mahakama inaonyesha 'kuna kesi ya kujibu''
Si sahihi kusema kesi imekwisha, hatukusikia utetezi
Ni makosa kusema 'kuna msamaha' hakuna hatia au hukumu iliyosomwa popote pale
Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi kulikuwa na ushahidi wa kutosha kuthibitisha ugaidi
Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka walikuwepo mashahidi wa kumtia hatiani Mbowe na Wenzake
Kwa mujibu wa Mahakama, Mbowe na wenzake walikuwa na kesi ya kujibu.
Mwisho wa yote kesi imeondolewa mahakamani bila hitimisho
Kuna mengi ya kujiuliza, kuhoji au kushangaa yatokanayo na kesi
1. Kesi iliendeshwajwe bila kujiridhisha ikiwa kuna tatizo la uhalifu !
Jeshi la Polisi lilieleza umma uwepo wa ushahidi wa kutosha dhidi ya Watuhumiwa.
Mwendesha mashtaka na jeshi walifikisha kesi Mahakamani, wameiondoa , ilikuwaje ikafika ilipofikia.
2. Je, sheria zetu zinalinda umma au zinatumika vibaya na waliopewa dhamana!
Tuhuma za ugaidi ni nzito kitaifa na kimataifa. Sheria ya makosa ya ugaidi ni kutopewa dhamana na vifungo virefu.
Kwa haya ya kuondoa kesi bila hitimisho, je, sheria ilitumiwa kama ilivyokusudiwa?
Wanaohisi sheria imetumika kisiasa watakuwa wamekose wapi kwa dhana hiyo
3. Nani anawajibika kwa gharama za kesi
Kwa uzito wa kesi gharama zilizotumika ni pamoja na zile za mahakamani kwa ujumla wake
Kwavile hakuna matokeo ya kesi kwa hukumu , nani anabeba gharama za kesi ?
Ikiwa ni Wananchi, yapi ni maelezo ya kutosha kuhusu matumizi ya kodi zao!
4. Nani anawajibika kwa ''gharama'' za uharibifu wa taswira ya nchi!
Kesi imekuwa na ''gharama' za taswira ya nchi. Kwa kukosa hitimisho, nchi inabaki na tasiwra gani kuhusu utwala wa sheria
Je, wanaodhani kuna mfumo kandamizi dhidi ya Wananchi wamekosea wapi na utetezi wa hapana ni upi.
Kwa upande wa ndani ya nchi, kipindi cha kesi mambo mengi mazuri yanayofanywa na serikali yamefunikwa na kesi
Nani anawajibika kwa ''gharama'' ya kesi hii katika mtazamo huo!
5. Nani anawafidia waathirika
Kwa kukaa ndani miezi au mwaka na kwa ushahidi wa 'kuteswa' nani anawajibika kuwalipa gharama
Kumnyima mtu uhuru ni kosa,kwa mtazamo wa kesi kuondolewa tu mahakamani nani atawalipa waathirika.
Kumkamata mtu ni haki, kumfikisha mahakamani ni haki, na kumpa nafasi ya utetezi ni haki na haki kubwa ni kumpa hukumu
Kwa vile watuhumiwa hawakupewa nafasi ya kujitetea au kuhukumiwa, haki yao ipo wapi
6. Ni ipi taswira ya mahakama katika jicho la kutoa haki bila hiyana au upendeleo
Mwenendo wa kesi uliiacha mahakama ikitazamwa kwa jicho la shaka sana
Maamuzi yalishangaza hata wanasheria, lakini kubwa, kwa vile kulikuwa na kesi ya kujibu na shtaka likaomdolewa wapi 'kesi hii inaacha image' ya mahakama katika kutoa haki? Je, hakuna uharibifu wa integrity and credibility ya mfumo wa kutoa haki nchini!
Kesi imeondolewa lakini si bila 'athari' kwa washtakiwa, serikali na Chadema.
Kwa Washtakiwa, kunyimwa haki ya kujitetea wakiwa wametuhumiwa kwa miezi na mwaka inaacha taswira zao pabaya sana
Mfano, Mbowe ni mfanyabiasha ndani na nje ya nchi. Nani atakayemsafisha na tuhuma za ugaidi ikiwa haikutokea mahakamani?
Kwa upande wa serikali, je, mifumo na taasisi zetu zinalinda haki za wananchi au ni vyombo vinavyotumiwa tu kwa malengo nje ya yaliyokusudiwa. Ni kwa vipi wananchi wataamini tena ikitokea tuhuma kama hizo kwa kiongozi mwingine mathalani wa siasa ?
Na je, serikali iliyohakikisha lipo 'jambo' ilikubali vipi watuhumiwa wa ugaidi kuonana na mkuu wa nchi?
Kwa upande wa Chadema, kesi ya Mbowe iliwunganisha kuliko wakati mwingine. Kesi ilitoa nafasi ya kuonyesha kwanini kuna uhitaji mifumo mipya ya nchi kwa kutumia katiba mpya . Kesi imeonyesha matumizi mabaya ya sheria za nchi na kuthibitishia dunia uonevu unaozungumziwa na chama hicho. Kesi imeonyesha mshikamano wa hali ya juu kwa hali na mali kwa nyakati ngumu
Kwa ujumla kesi imekijenga Chadema badala ya kukidhoofisha na kuhakikisha umma kuwa Chadema ni taasisi bila kutegemea mtu
Lakini pia hitimisho la kesi limeacha kovu ndani ya Chadema. Kesi ''imeisha' kwa hamasa na msisimko mkuwa.
Kitendo cha Mwenyekiti Mbowe kuonana na Rais SHH siku alipofunguliwa kimezua mjadala mpana na kumwaga 'maji baridi katika moto mkali''. Je, Mwenyekiti Mbowe alichukua uamuzi sahihi kwa wakati sahihi na mahali sahihi?
Je, maliziko la kesi na hotuba ya Mbowe imejibu ''ubaridi' aliousababisha kwa kwenda Ikulu haraka ?
Hayo tunayajadili bandiko linalofuata
Si sahihi kusema kesi imekwisha, Mahakama inaonyesha 'kuna kesi ya kujibu''
Si sahihi kusema kesi imekwisha, hatukusikia utetezi
Ni makosa kusema 'kuna msamaha' hakuna hatia au hukumu iliyosomwa popote pale
Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi kulikuwa na ushahidi wa kutosha kuthibitisha ugaidi
Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka walikuwepo mashahidi wa kumtia hatiani Mbowe na Wenzake
Kwa mujibu wa Mahakama, Mbowe na wenzake walikuwa na kesi ya kujibu.
Mwisho wa yote kesi imeondolewa mahakamani bila hitimisho
Kuna mengi ya kujiuliza, kuhoji au kushangaa yatokanayo na kesi
1. Kesi iliendeshwajwe bila kujiridhisha ikiwa kuna tatizo la uhalifu !
Jeshi la Polisi lilieleza umma uwepo wa ushahidi wa kutosha dhidi ya Watuhumiwa.
Mwendesha mashtaka na jeshi walifikisha kesi Mahakamani, wameiondoa , ilikuwaje ikafika ilipofikia.
2. Je, sheria zetu zinalinda umma au zinatumika vibaya na waliopewa dhamana!
Tuhuma za ugaidi ni nzito kitaifa na kimataifa. Sheria ya makosa ya ugaidi ni kutopewa dhamana na vifungo virefu.
Kwa haya ya kuondoa kesi bila hitimisho, je, sheria ilitumiwa kama ilivyokusudiwa?
Wanaohisi sheria imetumika kisiasa watakuwa wamekose wapi kwa dhana hiyo
3. Nani anawajibika kwa gharama za kesi
Kwa uzito wa kesi gharama zilizotumika ni pamoja na zile za mahakamani kwa ujumla wake
Kwavile hakuna matokeo ya kesi kwa hukumu , nani anabeba gharama za kesi ?
Ikiwa ni Wananchi, yapi ni maelezo ya kutosha kuhusu matumizi ya kodi zao!
4. Nani anawajibika kwa ''gharama'' za uharibifu wa taswira ya nchi!
Kesi imekuwa na ''gharama' za taswira ya nchi. Kwa kukosa hitimisho, nchi inabaki na tasiwra gani kuhusu utwala wa sheria
Je, wanaodhani kuna mfumo kandamizi dhidi ya Wananchi wamekosea wapi na utetezi wa hapana ni upi.
Kwa upande wa ndani ya nchi, kipindi cha kesi mambo mengi mazuri yanayofanywa na serikali yamefunikwa na kesi
Nani anawajibika kwa ''gharama'' ya kesi hii katika mtazamo huo!
5. Nani anawafidia waathirika
Kwa kukaa ndani miezi au mwaka na kwa ushahidi wa 'kuteswa' nani anawajibika kuwalipa gharama
Kumnyima mtu uhuru ni kosa,kwa mtazamo wa kesi kuondolewa tu mahakamani nani atawalipa waathirika.
Kumkamata mtu ni haki, kumfikisha mahakamani ni haki, na kumpa nafasi ya utetezi ni haki na haki kubwa ni kumpa hukumu
Kwa vile watuhumiwa hawakupewa nafasi ya kujitetea au kuhukumiwa, haki yao ipo wapi
6. Ni ipi taswira ya mahakama katika jicho la kutoa haki bila hiyana au upendeleo
Mwenendo wa kesi uliiacha mahakama ikitazamwa kwa jicho la shaka sana
Maamuzi yalishangaza hata wanasheria, lakini kubwa, kwa vile kulikuwa na kesi ya kujibu na shtaka likaomdolewa wapi 'kesi hii inaacha image' ya mahakama katika kutoa haki? Je, hakuna uharibifu wa integrity and credibility ya mfumo wa kutoa haki nchini!
Kesi imeondolewa lakini si bila 'athari' kwa washtakiwa, serikali na Chadema.
Kwa Washtakiwa, kunyimwa haki ya kujitetea wakiwa wametuhumiwa kwa miezi na mwaka inaacha taswira zao pabaya sana
Mfano, Mbowe ni mfanyabiasha ndani na nje ya nchi. Nani atakayemsafisha na tuhuma za ugaidi ikiwa haikutokea mahakamani?
Kwa upande wa serikali, je, mifumo na taasisi zetu zinalinda haki za wananchi au ni vyombo vinavyotumiwa tu kwa malengo nje ya yaliyokusudiwa. Ni kwa vipi wananchi wataamini tena ikitokea tuhuma kama hizo kwa kiongozi mwingine mathalani wa siasa ?
Na je, serikali iliyohakikisha lipo 'jambo' ilikubali vipi watuhumiwa wa ugaidi kuonana na mkuu wa nchi?
Kwa upande wa Chadema, kesi ya Mbowe iliwunganisha kuliko wakati mwingine. Kesi ilitoa nafasi ya kuonyesha kwanini kuna uhitaji mifumo mipya ya nchi kwa kutumia katiba mpya . Kesi imeonyesha matumizi mabaya ya sheria za nchi na kuthibitishia dunia uonevu unaozungumziwa na chama hicho. Kesi imeonyesha mshikamano wa hali ya juu kwa hali na mali kwa nyakati ngumu
Kwa ujumla kesi imekijenga Chadema badala ya kukidhoofisha na kuhakikisha umma kuwa Chadema ni taasisi bila kutegemea mtu
Lakini pia hitimisho la kesi limeacha kovu ndani ya Chadema. Kesi ''imeisha' kwa hamasa na msisimko mkuwa.
Kitendo cha Mwenyekiti Mbowe kuonana na Rais SHH siku alipofunguliwa kimezua mjadala mpana na kumwaga 'maji baridi katika moto mkali''. Je, Mwenyekiti Mbowe alichukua uamuzi sahihi kwa wakati sahihi na mahali sahihi?
Je, maliziko la kesi na hotuba ya Mbowe imejibu ''ubaridi' aliousababisha kwa kwenda Ikulu haraka ?
Hayo tunayajadili bandiko linalofuata