Kesi ya Ridhiwan against Dr. Slaa na Mtikila

kinepi_nepi

JF-Expert Member
Aug 16, 2007
869
235
Nataka kujua kesi ya utajiri wa mwana wa mkuu wa kaya Rizone imefikia wapi, baada ya magazeti kuandika kuwa ameifungua.

Kipindi hiki ambacho wauza mafuta wamesitisha kutuuzia mafuta wakita faida nono na tetesi zikisema kijana huyu tajari huenda naye ni muuza mafuta na msafirishaji wa haya mafuta.

Swali kwa nini agope kuitwa tajiri kama anabiashara na kipato halali.

Dr. Slaa aliuza swali kuhoji utajiri wa Rizone ameupata vipi, ilikuwa rahisi kwa rizone kusema anavyopata fedha kama ni mkopo au urithi au baba alimsaidia. Ila kijana alisema hata kichehche anachoendesha ni cha bei rahisi, mengine ni mambo ya kimjini mjini.

Ni kawaida kwa watoto wa viongozi wa Afrika kujitajirisha kwa mgongo wa vyeo vya baba zao.

Raisi wa wa zamani wa Misri Hosni Mubarak ana kesi yeye na wanaye wawili kwa kosa la rushwa na kuwaibia wananchi wa Misri.

Raisi wa Libya Muamar Gaddaf anatuhumiwa yeye na wanaye kuwauwa wananchi wa Libya na kuwaibia fedha za nchi yao.

Rais Saddam Hussein wa Iraq alishirikiana na wanaye kuwatesa wananchi wa Iraq kwa kuwafunga na kujilimbikizia mali.

Rais wa zamani wa Zaire Mobutu seseko alishiriki yeye na wanaye kuifilisi Zaire.

Tuhuma hizi zinasikisha sana na kufedhehesha, nilitegemea kijana huyu kusema kuwa ni kweli ana biashara na aeleze wapi alipata mtaji. Kuwa na gari la thamani sio utajiri yeye kama msomi na mwajiriwa anaweza kununua gari au kuwa na nyumba ya kuishi. Kitendo cha kukataa kila kitu kimeleta maswali mengi sana.

Nategemea kesi hii itasaidia sio watawala wa leo tu na familia zao bali watawala wajao na waleo.

Wito: Kama kesi iko mahakamani watanzania wenye mapenzi mema, mliopo popote duniani shirikini kujenga kesi hii ili kuujua ukweli na kukomesha tabia hii kama kweli imeingia Tanzania.

Sina matatizo na utajiri wa mtu yeyote kama ameupata kwa njia halali. Ila tatizo ni kama kuna matumizi mabaya ya kodi za wananchi kunufaisha wachache. Hakuna sababu kuogopa fedha zako kama ni za halali.

Twende kazi.

Nategemea mahakama itatenda haki kwa pande zote.
 
Ridhiwan haogopi mtu. Anachofanya ni kuvuta muda kwasababu ana vitu vingi anataka kulipua. Kama hamna taarifa ulizeni.
 
jamani tumechoka maandamano, tufanye kazi kwa maendeleo ya taifa letu changa. Kila siku kuandamana tu, halafu nchi ikidumaa mnaanza kuitupia lawama CCM
 
Magwanda wakikosa la kusema huwa wanatia huruma. Kwanza kajibuni kesi ya madiwani, halafu wakili wenu wa Arusha ndio kama tulivyosikia.
 
Riz1 aliufyata mkia na hataki hata kugusia hilo tena
Sio riz tu hata hawo walomtaja wamekaa kimya...walituambia wana ushahidi kamili......Riz hana wasiwasi bado anapeta na kama ni kweli ni bilionea basi atazidi kupaa.....

siasa uchwara za bongo wote kitu kimoja wantuchezea kiini macho walala hoi
 
Ridhiwan haogopi mtu. Anachofanya ni kuvuta muda kwasababu ana vitu vingi anataka kulipua. Kama hamna taarifa ulizeni.

mabomu ya kujilipua yeye na baa'ake ambao ni mafisadi nyota katika historia ya nchi hii tangia tupate uhuru miaka 50 iliyopita..............
 
Sio riz tu hata hawo walomtaja wamekaa kimya...walituambia wana ushahidi kamili......Riz hana wasiwasi bado anapeta na kama ni kweli ni bilionea basi atazidi kupaa.....

ALWAYS not usually the GUILTY ARE AFRAID........very afraid........................
 
Magwanda wakikosa la kusema huwa wanatia huruma. Kwanza kajibuni kesi ya madiwani, halafu wakili wenu wa Arusha ndio kama tulivyosikia.

huyu wakili ana kadi ya ccm........
 
jamani tumechoka maandamano, tufanye kazi kwa maendeleo ya taifa letu changa. Kila siku kuandamana tu, halafu nchi ikidumaa mnaanza kuitupia lawama CCM

utachokaje maandamano wakati hata siku moja hatujakuona mtaani ukijumulika nasi...............................tangia tupate uhuru tumekuwa tukihimizwa tufanye kazi kwa biddi lakini tumegundua uchumi wetu unashambuliwa na vijirusi vyenye rangi ya kijani na manjano.............mwanzoni tulifikiria ni ile timu ya Jangwani..................lakini kumbe ni hawa mchwa wanaojiita chama cha mafisadi.........
 
Sio riz tu hata hawo walomtaja wamekaa kimya...walituambia wana ushahidi kamili......Riz hana wasiwasi bado anapeta na kama ni kweli ni bilionea basi atazidi kupaa.....

siasa uchwara za bongo wote kitu kimoja wantuchezea kiini macho walala hoi

Jamani siku nyingine someni magazeti ya Kiingereza. Mbona Ridhuani alishafungua kesi mahakamani ya madai dhidi ya Dr. Slaa na Rev. Mtikila kama wiki tatu zimepita sasa. The Citizen iliandika hii habari.
 
jamani tumechoka maandamano, tufanye kazi kwa maendeleo ya taifa letu changa. Kila siku kuandamana tu, halafu nchi ikidumaa mnaanza kuitupia lawama CCM

TAIFA CHANGA? Miaka 50
ya uhuru bado taifa changa? Halafu wewe kwa kuitetea ccm unapata nin? Maji taabu,umeme hakuna,mafuta taabu,bei ya bidhaa juu! Au nyinyi ndio wale mnaotumiwa na vigogo wa ccm halafu wanawapa kidogokidogo? Eti maandamano kila siku' tangu yafanyike Iringa yamefanyika lin? Ni ujinga kung'ang'ania ccm wakati hata viongozi wa juu wanapingana!
 
jamani tumechoka maandamano, tufanye kazi kwa maendeleo ya taifa letu changa. Kila siku kuandamana tu, halafu nchi ikidumaa mnaanza kuitupia lawama CCM
sio lazima uchangie i think haujui unachochangia it better ukasoma wenzako wanachangia nini,mafuta hakuna ,umeme hakuna,madini yetu wanauza,polisi inaua raia democrasia hakuna,njaa nayo hiyo, viongozi watu kila siku wapo hewani wanakula bata kwa kodi zetu ,nipe sababu za msingi kwanini tusiandamane kudai haki zetu za msingi ?tujenge taifa changa ?unauhakika taifa letu ni changa miaka hamsini ya uhuru bado ni taifa changa ,watu wanauza hadi mahakama kama sio uchu wa mali nini ?
 
Jamani siku nyingine someni magazeti ya Kiingereza. Mbona Ridhuani alishafungua kesi mahakamani ya madai dhidi ya Dr. Slaa na Rev. Mtikila kama wiki tatu zimepita sasa. The Citizen iliandika hii habari.
Mkuu tunashukuru kwa ushauri, tulikuwa tunafuatilia habari hii kwenye Sani, Kiu na Ijumaa wkienda
 
Back
Top Bottom