kinepi_nepi
JF-Expert Member
- Aug 16, 2007
- 869
- 235
Nataka kujua kesi ya utajiri wa mwana wa mkuu wa kaya Rizone imefikia wapi, baada ya magazeti kuandika kuwa ameifungua.
Kipindi hiki ambacho wauza mafuta wamesitisha kutuuzia mafuta wakita faida nono na tetesi zikisema kijana huyu tajari huenda naye ni muuza mafuta na msafirishaji wa haya mafuta.
Swali kwa nini agope kuitwa tajiri kama anabiashara na kipato halali.
Dr. Slaa aliuza swali kuhoji utajiri wa Rizone ameupata vipi, ilikuwa rahisi kwa rizone kusema anavyopata fedha kama ni mkopo au urithi au baba alimsaidia. Ila kijana alisema hata kichehche anachoendesha ni cha bei rahisi, mengine ni mambo ya kimjini mjini.
Ni kawaida kwa watoto wa viongozi wa Afrika kujitajirisha kwa mgongo wa vyeo vya baba zao.
Raisi wa wa zamani wa Misri Hosni Mubarak ana kesi yeye na wanaye wawili kwa kosa la rushwa na kuwaibia wananchi wa Misri.
Raisi wa Libya Muamar Gaddaf anatuhumiwa yeye na wanaye kuwauwa wananchi wa Libya na kuwaibia fedha za nchi yao.
Rais Saddam Hussein wa Iraq alishirikiana na wanaye kuwatesa wananchi wa Iraq kwa kuwafunga na kujilimbikizia mali.
Rais wa zamani wa Zaire Mobutu seseko alishiriki yeye na wanaye kuifilisi Zaire.
Tuhuma hizi zinasikisha sana na kufedhehesha, nilitegemea kijana huyu kusema kuwa ni kweli ana biashara na aeleze wapi alipata mtaji. Kuwa na gari la thamani sio utajiri yeye kama msomi na mwajiriwa anaweza kununua gari au kuwa na nyumba ya kuishi. Kitendo cha kukataa kila kitu kimeleta maswali mengi sana.
Nategemea kesi hii itasaidia sio watawala wa leo tu na familia zao bali watawala wajao na waleo.
Wito: Kama kesi iko mahakamani watanzania wenye mapenzi mema, mliopo popote duniani shirikini kujenga kesi hii ili kuujua ukweli na kukomesha tabia hii kama kweli imeingia Tanzania.
Sina matatizo na utajiri wa mtu yeyote kama ameupata kwa njia halali. Ila tatizo ni kama kuna matumizi mabaya ya kodi za wananchi kunufaisha wachache. Hakuna sababu kuogopa fedha zako kama ni za halali.
Twende kazi.
Nategemea mahakama itatenda haki kwa pande zote.
Kipindi hiki ambacho wauza mafuta wamesitisha kutuuzia mafuta wakita faida nono na tetesi zikisema kijana huyu tajari huenda naye ni muuza mafuta na msafirishaji wa haya mafuta.
Swali kwa nini agope kuitwa tajiri kama anabiashara na kipato halali.
Dr. Slaa aliuza swali kuhoji utajiri wa Rizone ameupata vipi, ilikuwa rahisi kwa rizone kusema anavyopata fedha kama ni mkopo au urithi au baba alimsaidia. Ila kijana alisema hata kichehche anachoendesha ni cha bei rahisi, mengine ni mambo ya kimjini mjini.
Ni kawaida kwa watoto wa viongozi wa Afrika kujitajirisha kwa mgongo wa vyeo vya baba zao.
Raisi wa wa zamani wa Misri Hosni Mubarak ana kesi yeye na wanaye wawili kwa kosa la rushwa na kuwaibia wananchi wa Misri.
Raisi wa Libya Muamar Gaddaf anatuhumiwa yeye na wanaye kuwauwa wananchi wa Libya na kuwaibia fedha za nchi yao.
Rais Saddam Hussein wa Iraq alishirikiana na wanaye kuwatesa wananchi wa Iraq kwa kuwafunga na kujilimbikizia mali.
Rais wa zamani wa Zaire Mobutu seseko alishiriki yeye na wanaye kuifilisi Zaire.
Tuhuma hizi zinasikisha sana na kufedhehesha, nilitegemea kijana huyu kusema kuwa ni kweli ana biashara na aeleze wapi alipata mtaji. Kuwa na gari la thamani sio utajiri yeye kama msomi na mwajiriwa anaweza kununua gari au kuwa na nyumba ya kuishi. Kitendo cha kukataa kila kitu kimeleta maswali mengi sana.
Nategemea kesi hii itasaidia sio watawala wa leo tu na familia zao bali watawala wajao na waleo.
Wito: Kama kesi iko mahakamani watanzania wenye mapenzi mema, mliopo popote duniani shirikini kujenga kesi hii ili kuujua ukweli na kukomesha tabia hii kama kweli imeingia Tanzania.
Sina matatizo na utajiri wa mtu yeyote kama ameupata kwa njia halali. Ila tatizo ni kama kuna matumizi mabaya ya kodi za wananchi kunufaisha wachache. Hakuna sababu kuogopa fedha zako kama ni za halali.
Twende kazi.
Nategemea mahakama itatenda haki kwa pande zote.