Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Chama cha ACT kimesema Waandishi wa Habari wanakaribishwa Kuhudhuria.
============================
Mahakama Kuu Masjala Kuu Dodoma, leo Jumatatu, Septemba 8, 2025 inahitimisha usikilizaji shauri la kuenguliwa kwa mgombea urais aliyeteuliwa na Chama cha ACT-Wazalendo kupeperusha bendera yake katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, utakaofanyika Oktoba 29.
Awali Mahakama hiyo ilielekeza shauri hilo lisikilizwe kwa njia ya maandishi na mawakili wa pande zote waliwawasilisha hoja zao kwa tarehe walizopangiwa.
Hata hivyo mahakama hiyo, inahitimisha usikilizaji wa shauri hilo leo kwa njia ya mdomo, ambapo mawakili wa pande zote watafika mahakamani kwa ajili ya ufafanuzi wa baadhi ya hoja zao za maandishi.
Shauri hilo limefunguliwa na Bodi ya Wadhamini waliosajiliwa wa ACT-Wazalendo na mgombea urais aliyeteuliwa na chama hicho, Luhaga Mpina; dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).
Chama hicho kilichukua hatua hiyo kufuatia uamuzi wa Msajili wa Vyama vya Siasa kubatilisha uteuzi wa Mpina kuomba kuteuliwa na INEC kuwa mgombea urais wa chama hicho, na wa INEC kumzuia kurejesha fomu yake ya kuomba uteuzi aliyokabidhiwa awali kuijaza.
Katika shauri hilo namba 21692 la mwaka 2025 lililofunguliwa chini ya hati ya dharura sana, chama hicho pamoja na mambo mengine kinapinga uamuzi wa INEC kumuengua mgombea wao huyo katika orodha ya wagombea wa vyama mbalimbali walioomba uteuzi wake.