DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Tundu Lissu imehairishwa leo, Ijumaa Oktoba 24.2025 hadi Novemba 03.2025
Kesi hiyo imehairishwa kufuatia ombi la Jamhuri lililowasilishwa Mahakamani hapo likieleza kuwa, leo ilitakiwa wamlete shahidi wa Nne (4) aanze kutoa ushahidi wake baada ya yule wa Tatu (3) kukamilisha hapo jana, lakini wameshindwa kuleta shahidi hii leo kutokana na kwamba wameshindwa kumsafirisha kwa wakati na mashahidi wao hitajika nje ya Dar es Salaam (wapo mikoani)
Lissu alionekana kupinga vikali hoja hiyo akidai kwamba hiyo ni janjajanja ya Jamhuri kutaka aendelee kukaa gerezani hadi Uchaguzi Mkuu umalizike hivyo kuiomba Mahakama kuilazimisha Jamhuri kuendelea na kesi leo au Mahakama impatie dhamana aende nyumbani
Katika uamuzi wake, Mahakama kupitia jopo la Mawakili watatu (3) wanaosikiliza kesi hiyo wamesema kesi inayomkabili haina dhamana, na kwamba suala la kuomba hairisho kutokana na changamoto la mashahidi linakubalika kisheria na ikizingatiwa kuwa tangu kesi hiyo ianze hakuna siku ambayo Jamhuri imeshindwa kumleta shahidi
Hivyo kesi hiyo imehairishwa sasa hadi Novemba 03.2025 ambapo shahidi wa Nne (4) wa Jamhuri ataanza kutoa ushahidi wake.
Soma Pia: Kesi ya Lissu kuendelea leo Oktoba 24, shahidi wa nne wa jamhuri asubiriwa kwa hamu
Kesi hiyo imehairishwa kufuatia ombi la Jamhuri lililowasilishwa Mahakamani hapo likieleza kuwa, leo ilitakiwa wamlete shahidi wa Nne (4) aanze kutoa ushahidi wake baada ya yule wa Tatu (3) kukamilisha hapo jana, lakini wameshindwa kuleta shahidi hii leo kutokana na kwamba wameshindwa kumsafirisha kwa wakati na mashahidi wao hitajika nje ya Dar es Salaam (wapo mikoani)
Lissu alionekana kupinga vikali hoja hiyo akidai kwamba hiyo ni janjajanja ya Jamhuri kutaka aendelee kukaa gerezani hadi Uchaguzi Mkuu umalizike hivyo kuiomba Mahakama kuilazimisha Jamhuri kuendelea na kesi leo au Mahakama impatie dhamana aende nyumbani
Katika uamuzi wake, Mahakama kupitia jopo la Mawakili watatu (3) wanaosikiliza kesi hiyo wamesema kesi inayomkabili haina dhamana, na kwamba suala la kuomba hairisho kutokana na changamoto la mashahidi linakubalika kisheria na ikizingatiwa kuwa tangu kesi hiyo ianze hakuna siku ambayo Jamhuri imeshindwa kumleta shahidi
Hivyo kesi hiyo imehairishwa sasa hadi Novemba 03.2025 ambapo shahidi wa Nne (4) wa Jamhuri ataanza kutoa ushahidi wake.
Soma Pia: Kesi ya Lissu kuendelea leo Oktoba 24, shahidi wa nne wa jamhuri asubiriwa kwa hamu