Kesho madereva watagoma tena nchi nzima

Kesho madereva watagoma tena nchi nzima

Status
Not open for further replies.
tunataka mikataba,na suala la kusoma kila baada ya miaka mitatu hatutaki ni wizi na unyonyaji'basi na madaktali wakasome pia kila baada miaka mitatu.na walimu nao wakasome kila ufaulu unapokuwa duni

Mkajifunze pia customer care na sio kuweka gia tu. Akili za madereva uwa sizielewi kabisa, mfano anatoka kariakoo au ubungo anakuta wasafiri kibao stand anaweza asipakie au anaweza kusema hapakii anawacheka abiria kidogo then ndo anapakia, au analiweka gari pembeni kwanza watu wanapanda baadae anadai haendi ila wakikuta kituoni abiria wa kugombea wanapiga debe mpaka koo linakauka, madereva hasa wa daladala wana akili ndogo pamoja na makondakta wao.
 
Kufa kufaana, kesho wenue usafiri wao binafsi wanateleza tu, hamna foleni!
 
tahadhari kwa watumiaji wa vyombo vya usafiri vya umma.

kuna kila dalili kwa mgomo mwingine wa dala dala kutokana na madai ya wasafirishaji kwamba barabara ya kuingia na kutoka stand ya makumbusho ni mbovu na inaharibu magari yao.

wahusika wamedai kwamba kituo kimejaa matope; barabara pia za kuingia na kutoka kituoni zina mahandaki na zinajaza maji na matope; wanashindwa kufanya kazi katika hali nzuri tofauti na hali ilivyokua kipindi kile kituo cha mwenge.

hali hii imekua ikiendelea kwa muda sasa; ukizingatia jitihada mbali mbali walizofanya wahusika hao kuomba barabara zitengenezwe bila mafanikio; wakati ushuru unakusanywa kila siku.

Kutokana na wahusika kuziba masikio; wasafirishaji wameona wagome kushinikiza kukarabatisa kwa barabara hizo; au watakaidi kukitumia kituo kushushia ndani mpaka watakapo sikilizwa.

ni pigo jingine tena kwa watumiaji wa usafiri wa uma.
 
TBC1 kuna Mkuu wa mkoa wa DSM na kamanda Kova wanaongelea swala la mgomo kesho.
Kesho kutakuwa na mkutano kati ya Waziri mkuu na madereva. Mkuu wa mkoa amesema kuwa madereva wasigome wafanye kazi kama kawaida. Wawakilishi wa madereva watakutana na Pinda saa sita mchana.

My take kama walisha kutana na madai yao hayakutekelezwa, je kesho watakubari kufanya kazi bila kutekelezewa mahitaji Yao?
 

Attachments

  • 1430677115334.jpg
    1430677115334.jpg
    60.9 KB · Views: 325
Nipo mtaa wa Kihonda hapa Morogoro, kesho asubuhi na damka kwenda Bigwa. Bajet yangu ni 1600 kwa nauli, kama mkigoma ntapga mguu Asante JKT sina wasiwasi
 
safi sana madereva,maana kuna mijitu inafikiri yenyewe ni mungu mtu
 
Mbona kama ume_type mwenyewe na kui_print!, maana haioneshi kama imeandikwa na nani hata kuweka sahihi kuaminisha jamii kweli ni official announcement.
 
naomba wagome tu yaani kesho wagome mpaka wa maguta.
 
Wabongo ndio wamezoea kupeana taarifa kwa staili hiyo huo ujumbe umesambaa sana kwenye whaatsap na mtaani wanasema kesho hakuna usafiri kuanzia bodaboda. Tuombe mungu tu kama utatokea uwe wa amani
 
Mbona kama ume_type mwenyewe na kui_print!, maana haioneshi kama imeandikwa na nani hata kuweka sahihi kuaminisha jamii kweli ni official announcement.

Wanaogopa segerea, kutolewa meno, nk.
 
Mbona kama ume_type mwenyewe na kui_print!, maana haioneshi kama imeandikwa na nani hata kuweka sahihi kuaminisha jamii kweli ni official announcement.

Sahihi huko huko kwenu sisi tunataka tangazo tu na limeelewekA kwa uzuri kabisa,wee unayesubir sahihi endelea kusubir
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom