Kero ya Vodacom na SMS za kamata mpunga

Kero ya Vodacom na SMS za kamata mpunga

Nimeiblock hiyo namba yao...kwa hiyo kila nkiona notification ya 'Content blocked' Sina haja ya kuifungua kwa hyo mambo ni mwemwere mwemwere
 
siyapendi haya ma sms ni usumbufu sana na kero kubwa
 
Vodacom wahuni maana baada wanakuuliza maswali ya kitoto mfano Rais wa Tanzania anaitwa nani ili uendelee kuliwa. Tatizo TCRA na FCC wamewaachia hawa jamaa wa makampuni ya simu tunawaomba wawafuatilie kwa karibu
 
mimi line ya voda ipo kapuni aisee.... jamaa wezi wa vifurushi hatari.... tangu nianze kutumia Halotel naona msongo wa mawazo sina tena
 
mimi hata network yao inazingua kuwasiliana na ndugu zangu na ikipatikana zinaingia sms za kamata mpunga halafu inazingua tena.

vodacom mpo hovyooooo.
 
Mimi juzi niliwapigia Huduma kwa wateja na kuwauliza kulikoni kutuma tuma sms zao zisizo na maana? Wakadai,wazo langu wanalifanyia kazi. Kuanzia siku hiyo sijazipata tena. Nilimkoromea jamaa mpaka mwenyewe akaona sitanii na sitaki ujinga.
Kama mtu hataki ni hataki tu.
Wanaudhi sana hawa majamaa
Aisee ngoja na mi niwapigie
 
Una block vipi mkuu? maana mimi ni kero kwangu sana
Unatumia feature fone au Smartphone?? Kama ni smartfone tafuta app ya Call App
Una block vipi mkuu? maana mimi ni kero kwangu sana
Unatumia feature fone au Smartphone?? Kama ni smartfone tafuta app ya Call App au true caller..tafuta option ya call blocking and Sms filter ( Harassment filter)..nenda hapo then weka hiyo namba ya vodacom inayokutumia Message..Message zao zinakuja kimyakimya na hutakuwa ukiona notification..ukitaka kuziona hizo message zao mpaka ufungue hiyo App...
 
inakera sana. sometimes nafungua kwa hamu nikidhani ni Halima au wateja wa hoho nakutana na 15444!
 
Unatumia feature fone au Smartphone?? Kama ni smartfone tafuta app ya Call App

Unatumia feature fone au Smartphone?? Kama ni smartfone tafuta app ya Call App au true caller..tafuta option ya call blocking and Sms filter ( Harassment filter)..nenda hapo then weka hiyo namba ya vodacom inayokutumia Message..Message zao zinakuja kimyakimya na hutakuwa ukiona notification..ukitaka kuziona hizo message zao mpaka ufungue hiyo App...

Asante ndugu, na miye ni muhanga wa haya mameseji. Kwa kweli yanaboa sana
 
UJUMBE MUHIMU KWA NAMBA 767xxxxxxxx: Tuma neno GO kwenda 15544 SASA na ushiriki kwenye droo ya TZS 100,000,000 LEO! Vodacom KAMATA MPUNGA!


Hiyo kitu inakera mno kila baada ya muda naona SMS imeingia unakuta ndio hiyo ya kamata mpunga hawa wabadilishe utaratibu wao hii ni kerooooo au tuhamie mitandao mingine
Kitambo sana nimeshasepa huko.
 
Alafu kibaya zaidi ndo uwe umepanga appointment ya mgegedo na manzi wako, mara inaingia msg kuicheki kwa mzuka kumbe ni ya Vodacom aaaaaaaagh
 
UJUMBE MUHIMU KWA NAMBA 767xxxxxxxx: Tuma neno GO kwenda 15544 SASA na ushiriki kwenye droo ya TZS 100,000,000 LEO! Vodacom KAMATA MPUNGA!


Hiyo kitu inakera mno kila baada ya muda naona SMS imeingia unakuta ndio hiyo ya kamata mpunga hawa wabadilishe utaratibu wao hii ni kerooooo au tuhamie mitandao mingine
Pole sana mkuu. Sio wewe tu unayekerwa na hizo sms...sote zinatukera. Halafu huwa wanatuma asubuhi sana...mtu unakatiza usingizi wako unakimbia mbio mbio kufungua simu ukidhani ni ujumbe wa maana kumbe ni ujumbe wa kipuuzy na kitapeli. Wanakera sana hawa makaburu.
 
Back
Top Bottom