Kenyan media sector VS Tanzania media sector

luangalila

JF-Expert Member
Jan 12, 2014
6,325
6,871
Hellow Guys, Habari yenu waungwana toka ktk jumuia yetu ya Afrika Mashariki, binafsi nawasilisha UZI leo siku ya Jpili, nimebahatika kutazama television kadhaa za Kenya nimeona hawa jamaa wanafanya investment kubwa sana ktk media houses zao tofauti kabisa na Tanzania, hata ukitazama vipindi vya Tv vya Kenya unaona umakini wa hali ya JUU mnoo kuanzia uandaaji wa habari mpaka makala wanazo tengeneza tofauti na Tanzania ni muda mrefu sanaa ktk Teleision zetu nyingi waandishi wetu wa habari wanashindwa kuandaa makala au habari za utafiti zilizo ktk kiwango kizuri na zenye content. Nikijaribu ku tolea mfano ktk vituo kadhaa vya kenya citizen tv leo Jpili wanaleta makala ya vijana wanaokwenda kujiunga na al shabaab hii kitu POA sanaa na sio mara yao ya kwanza kuleta makala kama izo hapa TZ makala za utafiti kama izi niliwahi kushuhudia kipindi kile cha sakata la watoto yatima pale MAKETE na HIV kule mkoa mpya wa Njombe alikuwepo dada mmoja toka channel Ten alikuwa anaitwa Bahati mndetele Nyembe alileta ile makala ilimpa sifa sanaa kuanzia hapo makala kama zile zimeadimika TZ achana na zile habari za uchunguzi za akina DC JM
 
Don't feel so bad... Hapa Kenya pia ni jokers tu. Some try, a lot of times they do good.. but they are just as clueless. I personally believe , because of the importance of the media to a society, journalists need training in more than presentation and the like. They need to learn law, psychology, political science, economics and be taken through a class on patriotism.
 
Kenya wanatuzidi sana kwenye upande wa Media

Vipindi unaona kweli vimepikwa..

Nanaa
 
Media zetu huwa na ujasiri unaoanika uovu, sio kama Tanzania ambapo kuandika chochote lazima ufunge kwa maombi....

Nimeshangaa sana deni la taifa la Tanzania limeongezeka kiasi hiki na hakuna aliyesema, media zao bado huandika eti nchi inatumia hela ya ndani...

 
Media za kenya ni very tribal..Kuna Tv na radio za wakikuyu wakalejin wajaluo n.k
Zinazo baki ni za wanasiasa na agenda yao ni kupigia debe mwanasiasa mmiliki..
Hakuna media inayo egemea mahitaji ya mwananchi wa kawaida.
Kenya hakuna media freedom, kuna tribal freedom..Makabila yapo huru kuchochea migawanyiko ya kikabila kupitia media
 
Media za kenya ni very tribal..Kuna Tv na radio za wakikuyu wakalejin wajaluo n.k
Zinazo baki ni za wanasiasa na agenda yao ni kupigia debe mwanasiasa mmiliki..
Hakuna media inayo egemea mahitaji ya mwananchi wa kawaida.
Kenya hakuna media freedom, kuna tribal freedom..Makabila yapo huru kuchochea migawanyiko ya kikabila kupitia media
Hizo Tv. station na radio zinazotumia lugha za asili zinamilikiwa na media zinazomiliki Tv. na radio station kubwa za kitaifa ambazo zinarusha matangazo kwa lugha rasmi za kiswahili na kiingereza. Lengo lao kuu ni kufikisha huduma zao mashinani kwa lugha zinazoeleweka zaidi. Kwa mfano RMS inayomiliki Citizen Tv na radio ina Tv. na radio station za kikuyu, kijaluo, kiluhya nk. na 'content' na habari zinawasilishwa kwa njia moja kwenye stesheni zake zote, tofauti tu ni kwenye lugha zinazotumika. Swali langu, ni nini kinazuia media za Tz ambazo zinatumia lugha moja ya kiswahili kutimiza wajibu wao ipasavyo?
 
Hizo Tv. station na radio zinazotumia lugha za asili zinamilikiwa na media zinazomiliki Tv. na radio station kubwa za kitaifa ambazo zinarusha matangazo kwa lugha rasmi za kiswahili na kiingereza. Lengo lao kuu ni kufikisha huduma zao mashinani kwa lugha zinazoeleweka zaidi. Kwa mfano RMS inayomiliki Citizen Tv na radio ina Tv. na radio station za kikuyu, kijaluo, kiluhya nk. na 'content' na habari zinawasilishwa kwa njia moja kwenye stesheni zake zote, tofauti tu ni kwenye lugha zinazotumika. Swali langu, ni nini kinazuia media za Tz ambazo zinatumia lugha moja ya kiswahili kutimiza wajibu wao ipasavyo?
Wacha kukurupuka hovyo. Lugha gani kenya inaeleweka sana isopokuwa Kiswahili na kiingereza ambazo watoto hufunzwa kutoka darasa la kwanza?..Mimi mwenyewe kuandika na kusoma kukiyu ni changamoto kubwa licha ya kuwa mzawa wa ukikuyuni na nikasoma kikuyu kama somo darasani hadi darasa la tatu enzi za Maziwa ya nyayo..
Hakuna jambo la umuhimu wowote wa media za lugha ya asili sababu kizazi hiki hakuna anaye ongea lugha ya asili kwa ufasaha kuliko kiingereza na sheng.
Tanzania hamna media za asili na matunda yake ni umoja wa makabila
 
Wacha kukurupuka hovyo. Lugha gani kenya inaeleweka sana isopokuwa Kiswahili na kiingereza ambazo watoto hufunzwa kutoka darasa la kwanza?..Mimi mwenyewe kuandika na kusoma kukiyu ni changamoto kubwa licha ya kuwa mzawa wa ukikuyuni na nikasoma kikuyu kama somo darasani hadi darasa la tatu enzi za Maziwa ya nyayo..
Hakuna jambo la umuhimu wowote wa media za lugha ya asili sababu kizazi hiki hakuna anaye ongea lugha ya asili kwa ufasaha kuliko kiingereza na sheng.
Tanzania hamna media za asili na matunda yake ni umoja wa makabila
Unaumwa, lugha za mama au lugha za asili ndio lugha ambazo huwa zinatumika kufikisha ujumbe wowote nyeti virahisi kule mashinani. Sasa tuseme wewe hapo ambaye huna weledi wowote kwenye lugha yako ya asili, na bado huwa unachemsha hapa jukwaani kwenye lugha zote za kiingereza na kiswahili ni mbumbumbu wa kutupwa au? Alafu pia hujajibu swali langu, kinachozuia media za Tz. kufanya kazi zao kwa weledi ni nini?
 
Unaumwa, lugha za mama au lugha za asili ndio lugha ambazo huwa zinatumika kufikisha ujumbe wowote nyeti virahisi kule mashinani. Sasa tuseme wewe hapo ambaye huna weledi wowote kwenye lugha yako ya asili, na bado huwa unachemsha hapa jukwaani kwenye lugha zote za kiingereza na kiswahili ni mbumbumbu wa kutupwa au? Alafu pia hujajibu swali langu, kinachozuia media za Tz. kufanya kazi zao kwa weledi ni nini?
I am able to communicate effectively even to complete idiots thats why you understand and quote me.
I wonder where in kenya you come from where Tribal languages are used as the language of instruction to students. Stop being dishonest
The reason why Tz has no Tribal Media stations is because Mwalimu nyerere understood that language difference can severly fan tribal hatred. The media in TZ is patriotic, yes they can make extra money by targeting spefic markets with tribal radio stations but they understand that the country is bigger than a few coins
 
Back
Top Bottom