Kenya yapata upenyo: Tanzania yajisalimisha tena mikononi mwa Kenya

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Sep 4, 2019
1,395
3,901
TANZANIA YAJISALIMISHA TENA MIKONONI MWA KENYA

Kwa miaka takribani mitano Tanzania imekuwa "mwana mpotevu" baada ya Hayati Rais Magufuli kustukia "faulo" za kibiashara yaani biashara zisizokuwa na mizania sawa baina ya majirani hawa wawili. Ikumbukwe kuwa Kenya ndilo taifa la kiafrika linaloongoza kwa uwekezaji nchini Tanzania. Kwa lugha nyingine, Tanzania imekuwa "koloni mamboleo" la Kenya kwa miongo kadhaa.

Hayati Rais Magufuli hakutaka Tanzania iendelee na utumwa, akaratibu mipango ya kuinasua Tanzania kutoka kwa "mkoloni mweusi". Hatua hii ya Magufuli iliikera sana Kenya na tangu hapo uhusiano wa kibiashara ukayumba.

Ikumbukwe pia kuwa Kenya ni kitovu kikubwa cha mabeberu katika ukanda wa Afrika Mashariki. Makampuni mengi ya Kenya ambayo yamewekeza hapa nchini hayamilikiwi na wakenya ama yanamilikiwa na wakenya wenye asili ya kizungu (walowezi).

Kenya ambayo ilishirikiana na mabeberu wa Israel kufanikisha "Operesheni Entebbe" mwaka 1976 haiwezi kuwa mshirika wa kuaminiwa na mwenye uchungu na mtu mweusi.

Tutarajie

👉 Kenya kuongoza tena katika mauzo ya madini ya Tanzanite.
👉 Watalii kurejea Kenya
👉 Mlima Kilimanjaro sasa kuwa rasmi mlima wa Kenya
👉 Hujuma katika Shirika letu la Ndege (ATCL) ili kuikuza tena Kenya Airways
👉 Hujuma katika mashirika yetu ya simu ili kuikuza Safaricom
👉 na kadhalika.

Suala muhimu siyo "KAZI IENDELEE" bali "KAZI GANI IENDELEE"!
 
..at least hao walitokana na uchaguzi.

..unaweza kusema walikuwa wanachukiwa na walioshindwa uchaguzi.

..sasa huyu mama kosa lake ni nini? Je ni kwasababu ya kabila lake, dini yake, jinsia yake,..tatizo ni nini?
sasa uchaguzi na kuchukowa kuna mahusiano gani. wewe ulitegemea watu wote mil 60 wampende. hamna cha dini, jinsia wala kabila. nature ndio ipo hivyo. amechukiwa Gaddafi ambae kila kitu alitoa bure kwenye nchi yake sembuse Samia mkuu.
 
Mleta mada ni wa JPM- tena kindakindaki ...anata mama ssh aendeleze mambo yale Yale maana jpm na ssh ni kitu kimoja...kwa sasa inavyooneka ssh anafanyia kazi madongo ya Lissu- kuwa na ujirani mwema sio tu na wakenya Bali beyond akina Nkulunzinza...next stop Rwanda au Zimbabwe na Malawia...kazi anayo kwa kweli...
 
KUNAWAKATI HADI NATAMANI KUMUULIZA MTOA MADA KAMA AKO NA UFAHAMU WOWOTE KUHUSU MASWALA YA KIUCHUMI .

By then wacha nimuulize vimaswali vichache tu:-

1 Kwa hoja zake ni kama alitaka kutuambia kuwa Tanzania ilipaswa kuendea na misimamo ya viongozi watangulizi (ya kuifanya Tanzania iendelee kuwawekea uso wa mbuzi majirani hata kama misimamo hiyo haikuwa na tija kwa Taifa ?

2 Kwani Mama Samia amekwenda Kenya kufanya ufunguzi wa Bomba la Gas au wamekwenda kuweka mipango tu sawa?

3 Kunadhambi gani kwa Wakenya kuzitumia fursa ambazo sisi tumeshindwa kuzitumia ?

mfano :-

Kama hadi wanaweza kuwaambia watu huko Duniani kuwa Mlima Kilimanjanjaro upo kwao hatulioni hili kue ni tusi la wazi kabisa kwetu ?

Ulitaka tugombane nao kwasababu hizo na siyo sisi kuwashukuru kwa kutuamsha?

4 Issue ya wao kuwekeza kwetu (iwe ni wao au hata mabeberu kwani inatupunguzia nini sisi ikiwa watafuata sheria za inji sambamba na kulipa kodi kwa mujibu wa sheria ?

Kwani sisi tumekatazwa kwenda kuwekeza kwao?

Ziko inji hadi wakimbizi wanaruhusiwa kumiliki mali na kufanya Biashara kwa upana wake hilo nalo hulijui?

Tusidumaze akili issue ya uimarishaji wa na usisimuaji uchumi zinatutaka tuwe active sana and not as we think locally .
 
... mimi sina jipya sana ila kamshangao kidogo:
... hivi inakuwaje mtu anakabidhiwa dhamana ya 'maisha ya watu' halafu aanze na kunuizia kuwa ati watu watakimbia Dar?
... matokeo wanakimbia waliozoea 'KUSHIBA MILO MITATU' na sio jorowe wa town, aka wala urojo, walioishajipiga chanjo za 'chips dume kushushia maji'!

1620174081947.png
 
tatizo hicho kinchi chenu kina mashauzi Sana.wakati hata njaa mmeshindwa kuidhibiti
 
Back
Top Bottom