Kenya: Rais Magufuli anatukomoa kisiasa

Kenya: Rais Magufuli anatukomoa kisiasa

Aisee, tusitiane pressure bhana!! Kwenye sakata la bomba la mafuta kutoka Uganda nilishawaonya watendaji wetu kwamba, guys, trust me, Kenyatta hatakaa apumzike hadi siku anaona mabomba yanatandazwa ardhini na kwamba safari ya kuja Tanzania imeanza otherwise, ataendelea ku-lobby hadi siku ya mwisho! Nadhani haikupita hata wiki moja tangu nitamke vizuri mara nasikia Kenyatta kenda Ufaransa kuonana na wenye TOTAL yao na sio huyu Mwakilishi wa TOTAL East Africa... aliamua ku-lobby na mwenye mbwa na sio mbwa mwenyewe! That's Kenyatta!!! Na endapo tutadhani tumeshamaliza kazi, tutakuja kuachwa kwenye mataa kwenye dakika za majeruhi with no time to fight back!! Mbaya zaidi, hata ku-fight back kwenyewe hatuwezi... bomba kuja Tanga ilikuwa ni issue ya kuokota embe dodo kwenye mbuyu but we didn't do anything serious kuipata ile opportunity!
Kenya haikufika pele kwa bahati mbaya, wale ni strategists na hutafuta maarifa popote pale yanapopatikana. Wanachokifanya hivi sasa ni kutuaminisha kuwa tunawamudu ili tubweteke. Sipati picha hali ingekuwaje kama nchi yetu ndiyo ingekua inapata zile mishe mishe za alshabaab. Lakini pamoja misukosuko jamaa wameendelea kustawi zaidi na zaidi, huku zoezi la UKUTA peke yake utasikia litakavyoyumbisha uchumi wa nchi kwa gharama zilizotumika kulipa per diems za askari, kuviweka vikosi katika hali ya tahadhari pia kutoa silaha kutoka zinakutunzwa na kutembezwa mitaani.
Kenya wapo tayari kwenda kufanya lobbying kwa watakwimu wa kiuchumi wa world bank watoe takwimu zinazoonyesha kuwa Uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi huku wa Kenya ukisuasua kwa lengo la kutubwetesha tu.
 
Kenyatta ni msema ukweli, namheshimu sana, kwa maoni yangu kenyatta ndiye Raisi bora kabisa afrika mashariki
 
Kumbe wakenya hawamtambui mzee wa Piko kuwa aliwakilisha nchi maana hakuwa na mchango wala msimamo kama nchi! Alienda kuitikia uwep tu sio kuchangia! Ila kwa uelewa wa PM na JPM hawajui hayo mambo na kuyajadili hapo hapo na kueleza msimamo wa nchi lazima wamuombe Mzee Mahiga awepo na lazima awepo asaidie hapo! Namuona siku hizi Mahiga anapiga picha na ma Rais mara zote! Kawaida huwa ma Rais wanapiga wao tu! Ila sasa namuona ana hadhi sawa.....!!
 
Hapo kwenye mkataba wa EPA hao jamaa watashangaa zaidi hasa baada ya kikao cha juzi cha EAC, kukubaliana/azimia kuwa usanishwaji wa EPA ukafikiriwe tena (this Magufuli's/Tanzania's power/ influence).


Nimecheka sana eti Mseveni anamchukulia Kenyatta kama mwanae/ mtoto tu na si Rais , hivyo Kenyatta anagwaya kumface mzee M7.
Juzi nilimsikia Kagame akisema atakayekwamisha kuweka sahihi ya EPA ataftiwe adhabu, then kafika kwa magufuri amekubali kuwa hakuna isisainiwe haraka. Siasa hizi noma sana
 
Hivi tz na kenya nani ana viwanda zaidi ya mwenzake.
Maana nilimsikia jpm akisema wanataka kulinda viwanda vya ndani zaidi.
 
Kwa marais wa East Africa kinyatta ndo kiongozi nayemkubali
 
Wawe busy na nchi yao waachane na JPM kwa watanzania, kama wanataka jingine waseme
 
In unafiki mtupu lakini tusiyachukulie kama maoni ya nchi maana hao ni wachambuzi wa kawaida hata Mimi naweza itwa ITV nichambue kama walivyofanya sansana ni Uhuru wa maoni
 
Trust me, namchukia sana Uhuru Kenyatta... namchukia Kenyatta si kwa sababu ni mtu anayestahili kuchukiwa bali namchukia kv mimi ni Mtanzania ninayeipenda nchi yangu and I'll always be there for my country. Namchukia Kenyatta kwa sababu mimi si Mkenya na Kenyatta is very smart for Kenyan interests.

Labda usahihi nilipaswa kuwa na wivu lakini kwa ujeuri na hinda inabidi tu nimchukie kv Kenyatta ndie Rais ambae Africa ya leo ndie inamuhitaji. Kenyatta ni mroho tena mroho kweli kweli! Lakini tofauti na uroho wa wenzake kama vile Museven na Kagame ambao ni waroho wa madaraka; uroho wa Kenyatta ni wa kiuchumi...

uroho wa kutaka kuifanya Kenya kuwa economic giant now and always! Hapa ndipo ninapomchukia Kenyatta cuz' he can do whatever he can to stand atop of others. The guy is smart, trust me... lile ni bebari la kuzaliwa na kurithi kwahiyo linafahamu hila zote zinazohitajika kwenye dunia ya leo!!!

Haya mambo kwamba "hao watalii wakitaka waje, wasipotaka wasije...!" kamwe hayawezi kutoka mdomoni mwa bepari zohefu na lililokubuhu kama Kenyatta... sana sana si ajabu anakesha akiomba tuzidi kukaza ili "tukasanye kodi nyingi zaidi..!"

Kenyatta sikupata kumuogopa wakati wa JK kv nilifahamu JK anafahamu namna ya ku-deal na watu aina ya Kenyatta... ndo maana wakati ule anaruka ruka na akina PK na Ushoroba wa Kaskazini wao JK alikuwa anawacheka tu; kombora moja tu... wakaanza kutafutana wenyewe!!!

Mheshimiwa Uhuru Kenyatta, popote ulipo fahamu kwamba nakuchukia... lakini nakuchukia kwa sababu tu nafsi yangu imejawa husuda!! Huwa nazidi kukuchukia kila inaponipitia taswira ya Silicon Valley au kitu kinachofanana na Silicon Valley ndani ya Nairobi endapo utapewa fursa ya kuendelea kuongoza Kenya! Hivi katika mazingira hayo, nikupende kwa lipi?!
Acha kujikomba.
 
At the time mnagongesha glass mkidhani mmemshinda Kenyatta, yeye huwaacha muendelee kusherehekea, baada ya muda na matukio Fulani ndipo mnakuja kugundua kuwa hamkumshinda bali ni kinyume chake na tayari ameshawaacha hundreds of miles.
I real like the guy..


Mkuu, inaelekea huyu Jamaa alirithi traits za Babake, hata akiwa na wenzake unamuona katulia tulii akiwasoma wenzake, ngoja atoke hapo sasa - atamkuta amekwisha leap frog wenzake kiaina - jamaa huyu si mchezo hata kidogo.

Nilipo kuja kumshtukia ni pale kwenye ushindani wa ujenzi wa bomba la mafuta - mtu ungefikiri angeheshimu maamuzi ya Rais wa Uganda mambo yakaishia hapo - lakini wapi bwana? katafuta/lipa ma lobbists huko Ulaya wajaribu kizishurutisha kampuni ya Total wabadirishe maamuzi yao, bado akaona hilo halitosha - yeye na wapambe wake wakapanda ndege kwenda Ufaransa na Ujerumani kuendeleza vita yao ya ujenzi wa bomba, nafikiri Rais wa Ufaransa alimtolea nje, kwa Merkel ndiyo kabisaaa alimtolea uvivu kwa kumwambia kwamba Wajerumani wamechoshwa kuombwa ombwa misaada kutoka Serikali ya Kijerumani, Kenya wakipewa misaada inaishia kwenye mifuko ya Viongozi wao badala ya kusaidia wananchi wanyonge - Merkel alimdhalilisha jamaa kweli kweli, we sema UJK hakati tamaa.

Tukija kwa Serikali ya Uchina hiyo amekwisha tekwa nyara na Kenya, Wachina wanamchukulia Kenyatta seriously mpaka mtu unashangaa, ungetegemea kutokana na historia walao Wachina wangeifanya Tanzania kama HUB ya kila kitu - lakini wapi bwana!!! Wachina wamekwisha sahau mchango wetu wa kufanikisha Taifa hilo likubaliwe kujiunga na Umoja wa Mataifa, yaani Wachina wanawekeza zaidi Kenya kuliko Tanzania.
 
Wakenya wapo vizuri- Odinga aki shinda Mtamuona Magufuli daily -
 
Asante sana Dr. Rweyendera kwa video ya mjadala huu ni very informative! .
Kuna sehemu wametusema vibaya, kuna sehemu wamemsema Magufuli vibaya! , na kuna sehemu wametusema vizuri na kiukweli nimejisikia raha sana Mwalimu Nyerere alipozungumzwa kwa msimamo hivyo kufananishwa na Magufuli! .

Kitu ambacho Sijakipenda kabisa katika mjadala huu ni kitendo cha kumsakama sana rais Magufuli kutohudhuria mkutano wao without any mention ya uwepo Makamo wa rais wa Tanzania aliyemwakilisha rais Magufuli! . Hawa wa Kenya wanamaanisha Mhe. Samia Suluhu Hassan is nobody worth mentioned! . Angekuwa ni male angetajwa!. Wabaguzi wakubwa hawa! .

Pasco
Yes hapo bwana pasco ulichoongea nimekielewa
 
Aisee, tusitiane pressure bhana!! Kwenye sakata la bomba la mafuta kutoka Uganda nilishawaonya watendaji wetu kwamba, guys, trust me, Kenyatta hatakaa apumzike hadi siku anaona mabomba yanatandazwa ardhini na kwamba safari ya kuja Tanzania imeanza otherwise, ataendelea ku-lobby hadi siku ya mwisho! Nadhani haikupita hata wiki moja tangu nitamke vizuri mara nasikia Kenyatta kenda Ufaransa kuonana na wenye TOTAL yao na sio huyu Mwakilishi wa TOTAL East Africa... aliamua ku-lobby na mwenye mbwa na sio mbwa mwenyewe! That's Kenyatta!!! Na endapo tutadhani tumeshamaliza kazi, tutakuja kuachwa kwenye mataa kwenye dakika za majeruhi with no time to fight back!! Mbaya zaidi, hata ku-fight back kwenyewe hatuwezi... bomba kuja Tanga ilikuwa ni issue ya kuokota embe dodo kwenye mbuyu but we didn't do anything serious kuipata ile opportunity!

Kama una viongozi waliochaguliwa kwasababu ya kushindwa uchaguzi na wanamiliki kadi ya CCM unategemea nini?

Tatizo tunachagua viongozi wasio smart na ndo wanatusababisha tuwe kama tupo leo.
 
You're being too emotional over nothing

IPTL inalipa miionib499 per day na serikali na magu ameuchuna

Tunatakiwa kuwa mpango wa kuendeleza infrastructure na namna ya kuihusisha sekta binafsi na kwa kwa nini Magufuli hataki kuihusisha sekta binafsi

Those are the real issues ma sio kuwa emotional over what Kenyans think of us


Kwani Mada husika inahusu nini? Kwa nini ninyi watu huwa hamna akili lakini? Huyo uliyemnukuu kasikiliza mada iliyoletwa kajibu kulingana na jinsi alivyoisikia nakuilewa, wewe unakuja na yako, how stupid can you get man!
 
Kenya wapo tayari kwenda kufanya lobbying kwa watakwimu wa kiuchumi wa world bank watoe takwimu zinazoonyesha kuwa Uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi huku wa Kenya ukisuasua kwa lengo la kutubwetesha tu.



Duh! Hii yote inasababishwa na nini mpaka unaongea kwa hasira na uongo wote huo? Ni chuki tu uliyonayo kwa mtu mmoja yaani Raisi Magufuli? Pole sana ndugu, vuta pumzi ndefu kwa sekunde kadhaa halafu kunywa maji labda itakusaidia!
 
Back
Top Bottom