Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Ndege moja humu nchini iliyokuwa imebeba watu kumi Jumanne jioni imetoweka ikiwa angani kilomita 60 kutoka jijini Nairobi, Kamanda wa Polisi katika Kaunti ya Trans Nzola Samson Ole Kine alithibitisha, ilikuwa inatoka mjini Kitale ikielekea Nairobi.
Ndege hiyo aina ya Cesna C208 yenye namba za usajili 5YCAC inamilikiwa na Kampuni ya Fly Sax nchini humu, na inakisiwa kutoweka kwenye mawimbi ya udhibiti wa safari za ndege, rada, katika eneo la msitu wa mlima Aberdares.
Shirika la Mamlaka ya Usimamizi wa Safari za Ndege nchini (KCAA) lilithibitisha habari hizo kupitia akaunti yake ya Twitter Jumanne usiku.
"Tunathibitisha ripoti ya ndege iliyokuwa ikitoka Kitale kuelekea Nairobi kutoweka angani. Ilionekana mara ya mwisho kwenye mawimbi ya rada saa nane na dakika mbili mchana maili 40 kutoka jijini Nairobi ikipaa juu kwa urefu wa futi 11,000", umesema ujumbe huo.
Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Huduma kwa Wanyamapori (KWS), anayesimamia maeneo ya milima, Simon Gitau Jumanne usiku alisema Shughuli za kuitafuta ndege hiyo zimeanza katika milima ya Aberdares.
"Utafutaji kwa njia ya angani hauwezekani kwa sasa kutokana na hali ya hewa lakini utafanyika Jumatano asubuhi", alisema.
UPDATES:
Utafutaji wa Ndege aina ya Cesna C208 yenye namba za usajili 5YCAC iliyopotea Juni 05, 2018 ukiendelea ambapo leo baada ya takribani saa 48 mabaki ya ndege hiyo yameonekana huko Njabini, katika eneo la msitu wa mlima Aberdares
Mabaki hayo yameonekana kwa kutumia utafutaji wa kutumia ndege, hivyo timu ya uokoaji ya watu waliopo ardhini pamoja na timu ya madaktari wanelekea katika eneo hilo
UPDATES:
Abiria wote 10 waliokuwemo kwenye ndege iliyopata ajali baada ya kupotea angani na kuanguka katika eneo la Njabini, Aberdares wamefariki dunia
Taarifa hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kampuni ya Fly Sax inayomiliki ndege hiyo.
Ndege hiyo aina ya Cesna C208 yenye namba za usajili 5YCAC inamilikiwa na Kampuni ya Fly Sax nchini humu, na inakisiwa kutoweka kwenye mawimbi ya udhibiti wa safari za ndege, rada, katika eneo la msitu wa mlima Aberdares.
Shirika la Mamlaka ya Usimamizi wa Safari za Ndege nchini (KCAA) lilithibitisha habari hizo kupitia akaunti yake ya Twitter Jumanne usiku.
"Tunathibitisha ripoti ya ndege iliyokuwa ikitoka Kitale kuelekea Nairobi kutoweka angani. Ilionekana mara ya mwisho kwenye mawimbi ya rada saa nane na dakika mbili mchana maili 40 kutoka jijini Nairobi ikipaa juu kwa urefu wa futi 11,000", umesema ujumbe huo.
Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Huduma kwa Wanyamapori (KWS), anayesimamia maeneo ya milima, Simon Gitau Jumanne usiku alisema Shughuli za kuitafuta ndege hiyo zimeanza katika milima ya Aberdares.
"Utafutaji kwa njia ya angani hauwezekani kwa sasa kutokana na hali ya hewa lakini utafanyika Jumatano asubuhi", alisema.
Utafutaji wa Ndege aina ya Cesna C208 yenye namba za usajili 5YCAC iliyopotea Juni 05, 2018 ukiendelea ambapo leo baada ya takribani saa 48 mabaki ya ndege hiyo yameonekana huko Njabini, katika eneo la msitu wa mlima Aberdares
Mabaki hayo yameonekana kwa kutumia utafutaji wa kutumia ndege, hivyo timu ya uokoaji ya watu waliopo ardhini pamoja na timu ya madaktari wanelekea katika eneo hilo
UPDATES:
Abiria wote 10 waliokuwemo kwenye ndege iliyopata ajali baada ya kupotea angani na kuanguka katika eneo la Njabini, Aberdares wamefariki dunia
Taarifa hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kampuni ya Fly Sax inayomiliki ndege hiyo.