Siasa za Zitto zenyewe za kishamba tu, tangu akiwa Chadema amekuwa na siasa za kujikombakomba, kujionesha onesha, kusalitisaliti tu, hizi ni siasa za kishamba sana.
Katika kujifanya mzalendo, Zitto amekuwa mshambamshamba tu, amekuwa mtu wa kuzitishiatishia Taasisi za Umma ili zimhonge asianike maovu, amediriki hata kutetea ukiukwaji wa maadili ya nchi yetu na kuwa kibaraka wa Wazungu wanaotaka kutupa misaada kwa masharti ya kukubali Ushoga. Huu ni ushamba wa Hali ya juu.
Bata huliwa na wastaabu. Zitto hata mahusiano yake yamekuwa ya kishamba tu, ndiye mwenye historia ya kuoa wake wawili ndani ya Wiki moja.
Ulimbukeni ni kitu kibaya sana. Limbukeni anaweza kufanya mambo ya ajabu bila ya kuona aibu ila wanaomzunguka wakaona aibu kwa niaba yake. Kitu kibaya sana.
Zitto washawishi Watanzania kwa kitu kingine wakuelewe washawishike kukuona unafaa kuwa Rais, hili la kula bata, sifa hiyo huna kwa sababu mpaka hapo ulipo na zaidi ya miaka 40 huna historia ya kila Bata, Unataka kula Bata ukiwa Rais? Uzeeni? Kwanza nani alikwambia Watanzania wanamtaka Rais mla Bata? Unakumbuka 2015 kuna Mgombea alipata tabu sana kwa sababu tu ya kawaida yake ya kunyoa Unga? Itakuwaje Wewe unaetaka kula Bata ambayo huna hitoria nayo bali kwa sababu tu wewe ni Rais .
Urais ni ngazi ya juu kabisa katika nchi yetu, msiwe mnaropoka ropoka tu kama mtu anayeutaka urais wa Wasaf au Team Kiba. Au unautaka urais wa Leka Dutigite ile Taasisi ulioianzisha kwa Fedha za Walipa kodi ulizohongwa na Mifuko ya Hifadhi ya Jami wakati ulipokuwa Mwenyekiti wa PAC?