Kawe leo hii kuanzia Saa 1 hadi Saa 3 Usiku kulitokea nini hadi MP wa JWTZ Kufurika, Kukamata Watu, Kutembeza Kichapo na Kuzua taharuki?

Soma CPA kasome defensive factors ambazo zinaweza kukulinda usiwe liable.Utaelewa.
 
Mkuu mambo ya kisu au bisibisi ni yiming hata uwe vandame mtu akikutime anakuua
Boda boda na bajaji wengi wana bisibisi tena zile ndefu kabisa.

Ukiwa unabishana nae ukae kwa tahadhali.
Mara nyingi huwa wanatrmbea nazo kwa ajili ya kujitetea na majambazi ya pikipiki,

Huyo afande alifikiri cheo chake ndio kila kitu. Watu wamevurugwa kukuwahisha mbinguni hawaoni shida.

Ndio maana mimi siku zote hata mtoto mdogo anichokoze vipi sipigani nae maana najua linaweza kutokea lolote. Ni heri ionekane bwege mbele ya watu kuliko kujifanya kidume uishie kufa au jela
 
Shida sio hekima shida ni chuki, I'm telling you I know what I'm telling you raia punguzeni chuki na Jeshi lenu,
Huku kudharauliwa na kuchukiwa mmekutaka wenyewe.

Kwanini siku hizi mnapiga raia sana??
Utakuta jambo dogo tu la kutumia busara, nyie mnapiga. Zamani mlipendwa na kuheshimika....angalieni mlipokosea mrekebishe.
 
Wanajeshi mjifunze huyo kashaenda harudi tena. Haikua na ulazima wa kumzaba kofi amgemgombeza tu aachane nae. Raia wengine unaweza kuwachukulia poa ila ikachukua dakika kukuondoa duniani, huyo ana bisibisi mwingine ukute ana panga kaweka sehem akuzamishie la kichwa. Badilikeni
 
Kama kakutukana ndio una haki ya kumpiga?
Huko jeshini ndivyo mnavyofundishwa?
Sasa muwapige wanyonge, ukikutana na mwamba au mtu wa silaha madhara yake ndio hayo.
 
Punguza chuki za kijinga, form 4 failure ndio mlivyokaririshwa kua kila Askari ni form 4 failure? Acha kua mjinga chagua kua mwerevu,
Askari mwenye shule havimbi hovyo. Nasikitika kanari alishindwa kucontrol hasira.
Mimi pale Lugalo nafika sana na nafanya nao mambo mengi sana.
Nafahamu vikosi vingi tu na wakuu wake.....kwenye barracks hadi ofisini.
Wakubwa wana heshima sana, sasa hawa ndugu zetu form 4 dah dah......walinzi wa magetini dah ndo wanavimba.
Mkome.
 
Tatizo ni kwamba kuna watu baadhi wakiwa na nyadhifa flani serikalini wanafikiri ndio wana title deed ya hii nchi kwamba they can do you whatever they want, na wala huwawezi Fanya chochote, sasa ona sasa, Mungu atujalie hekima na busara katika kufanya maamuzi.
 
Mkuu The Underdog X umejitahidi sana kutetea askari. Wewe ukiwa kama kiongozi huko uliko, fikishieni taarifa wenzenu kuwa siku hizi mambo yamebadilika. Zamani ni polisi na ninyi tu ndio mlikua mnatembea na silaha (ukiacha viongozi wakubwa wakubwa).

Siku hizi kuna raia kibao wanatembea na silaha kihalali na haramu pia. Watu wamevurugwa na mambo mengi, ukiwatibua wanafanya lolote. Majuto huja baadae both sides.

Lakini pia, jeshini mjitafakari. Kwanini wananchi hawaliheshimu jeshi, wanalichukia jeshi si kama zamani?

Kimebadilika nini?

Nakumbuka zamani ukiwa porini huko remote ukiona gari ya jeshi unasimamisha unaomba lift wanakubeba. Siku hizi mtu akiliona gari huko analipisha mbali, kwanini?

Ilikua mtu anasimamisha gari vijijini na kuwazawadia mazao mikungu ya ndizi, n.k, why not today?

Mmebadilika mno, mnaonea raia wakati mwingine bila sababu za maana. Mtu kakosea njia porini huko kaingia eneo la jeshi, msaidieni aondoke. Ninyi mnaanza kumuadhibu....raia watakosa kujenga chuki?

Badilikeni au tuendelee kushuhudia vita mitaani.
 
Ujinga plus kigogo ni nani mbele ya Jeshi yaan kigogo umtume bodaboda akaue mwanajeshi alafu unavimba kua akiguswa utaua wewe nani useme akiguswa utaua mamlaka hayo unayatoa wapi?
Afike apa kambini atoe maelezo vizuri tumsikie ili tuone tunajadili vipi kifamilia
 
Magari yamepita asubuhi Mzee wewe umelala yamepita malori kibao yamebeba wanajeshi yanatoka Lugalo, endelea kulala wao hawalali wanakulinda wewe na mipaka ya Nchi yako
Mbona watu wengine ni washamba sana? Wanafanya kazi bure? Si ni kazi waliyoichagua na wanalipwa? Hujui kuna mgawanyo wa kazi? Unajua watu wanaokulisha wewe? Unajua watu wanaokutibu? Unajua watu wanaosafisha takataka? Una maana kwa vile mtu analinda ndiyo apige raia bila kufuata sheria?
 
Duuh Kanali ni mtu mkubwa sana jeshini kwann alifanya kitu Cha kijinga namna hii? SI Bora angepiga simu kikosini awaite vijana wake kuliko alichokifanya au alikuwa amelewa?
 
Na pengine hata huyo bajaji ukute alikuwa hajui kama Marehemu ni mwanajeshi, ila Cha kujifunza huku barabaran sio sehemu Nzuri kuvimbiana Bora uwe mpole tu hasa ukiwa kapuku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…