Kauli ya sina mtaji wa biashara ni dhana potofu

Kauli ya sina mtaji wa biashara ni dhana potofu

Ili kijana aweze kufanikiwa maishani, kuna mambo kadhaa muhimu anapaswa kuyazingatia. Haya hapa ni baadhi ya mambo ya msingi:

1. Kuwa na malengo maalum

Elewa unachokitaka maishani, weka malengo ya muda mfupi na ya muda mrefu, kisha yafanyie kazi kila siku.


2. Elimu na maarifa

Jitahidi kujifunza kila siku – iwe ni kupitia shule, vitabu, mitandao au watu wengine. Maarifa ni nguvu.


3. Kujituma na kufanya kazi kwa bidii

Hakuna mafanikio ya kweli bila juhudi. Fanya kazi kwa bidii na kwa nidhamu hata kama hakuna anayekuona.


4. Kujitambua na kujiamini

Fahamu uwezo wako, udhaifu wako na amini kuwa unaweza kufanikisha mambo makubwa. Kujiamini kunavunja vizuizi vingi.


5. Kujiepusha na matumizi mabaya ya muda

Epuka kupoteza muda kwenye mambo yasiyo na tija kama uvivu, starehe kupita kiasi, au marafiki wabaya.


6. Kujenga mtandao wa watu wenye maono

Zungukwa na watu wanaokuinua kiakili, kimaadili na kitaaluma. Marafiki wa kweli huchangia mafanikio yako.


7. Uvumilivu na kutokata tamaa

Njia ya mafanikio haikosi changamoto. Jifunze kutoka kwa kushindwa, simama tena na endelea kupambana.


8. Kuwa mbunifu na jasiri kuchukua hatua

Wazo zuri lisipofanyiwa kazi halina maana. Fikiria tofauti, chukua hatua, na usiogope kujaribu.
Naaam
 
Ni ajabu hakuna aliyeongelea ishu ya UAMINIFU km moja ya mtaji mkubwa sana kwenye mambo ya biashara. icho ni kitu kikubwa sana ambacho wengi wanakikosa.

UAMINIFU umekuwa mdogo sana hasa miaka hii. watu wanafanya magumashi (dhuluma) kwa wateja au wanabiashara wengine kwa short tim gain mwishowe wanakujikuta hawana wateja na connection wamepoteza.

bila UAMINIFU hata kama utaupata uo utajiri utakwama tu uko mbeleni. nazani hii ni spiritual pia. mungu anakulaani na vizazi wewe vyako kwa dhuluma zako kwa wengine.
 
Kuna wengi sana hawafanyi Biashara kwa sababu wanadhani kwamba tatizo lao ni kwamba hawana MTAJI. Utamsikia mtu anasema nikipata Mil 10, Au nikipata Mil 100 au nikipata laki 5 nitabadilisha maisha yangu oabisa. Huko ni kutokujua.

Hakuna kitu kama hicho. Hatuhitaji MTAJI mkubwa Bali UNAHITAJI mambo mawili yaani ufahamu kidogo na utayari.

Ifahamu kiasi kidogo unachotaka kufanya.

Pili, uwe na moyo wenye utayari wa kuanza na usiokata tamaa haraka.
kila kitu lazima kianze chini. Mtu anaanza kama mtotot, mti unaanza chini, mnyama hata tembo alikuwa mtoto.

Mbuyu ulikuwa mbegu kwanza.

Kwenye Biashara UNAHITAJI moyo ulio tayari na MTAJI WA 10,000. Wataalam wanasema kama huwezi kubadilisha 10,000 kuwa 100,000 maana yake huwezi kubadilisha milioni mia Moja kuwa kuwa milioni mia mbili.

Kwenye vitabu vitakatifu Kuna mfalme Sulemani aliandika kwenye Mithali 13. 11 kwamba Mali iliyopatikana haraka haraka hupungua, Bali Mali iliyopatikana kidogo kidogo huongezeka. Hii ina maanisha kwamba Kila mtu anatakiwa kuanza chini na siyo juu tena kidogo kidogo.

Uingereza walifanya utafiti wa watu waliopata Bingo ya mabilioni miaka ya nyuma na utafiti ukathibitisha Andiko la Sulemani la kwenye Mithali 13.11.

Ule utafiti uliwafuatilia watu waliopata au kushinda bahati na sibu au Bingo. Baada ya kufanya utafiti walipata matokeo haya 96+3+1=100.

YAANI kati ya watu 100 waliopata fedha za bahati nasibu au Bingo, watu 96 walirudia kwenye umaskini wao baada ya miaka mitatu hadi mitano. Watu watatu wakawa matajiri wa kawaida na Moja akawa tajiri mkubwa sana.

Huu utafiti unathibitisha kwamba Andiko La Sulemani kwenye Mithali 13. 11 na unathibitisha kwamba Changamoto yako siyo MTAJI Bali ufahamu mdogo na Utayari au moyo usiokata tamaa. Lazima uwe na moyo wenye utayari wa kuanza na kuanguka na kuanza na kuanguka na kuanza na kuanguka mpaka ufanikiwe. Haijalishi kama utachukua miezi sita au miaka mitatu.

Wachache sana wako tayari kuingia kwenye hiyo gharama ya kujifunza kidogo na kuwa na moyo usiokata tamaa ndo maana maana matajiri ni wachache. Wengine wanatafuta Hela nyingi bila kujua kwamba Hela nyingi ukipewa Leo ni sawa na kumpeleka mwanafunzi wa darasa la pili wa Shule ya Msingi, akajiunge Chuo kikuu. Ni sawa na kumimina maji ya ndo ya Lita 20 kwenye kikombe Cha chai. Mengi yatamwagika chini. Wakati unaanza chini ufahamu wako pia unaongezeka taratibu kadiri fedha inavyoongezeka. Hiyo ndo siri. Ndo maana Elimu ya darasani siyo kigezo Cha kuwa tajiri.

Leo hii Watanzania wote wakipewa MTAJI wa mil 10, nchi hii itabadilika kwa miaka mitatu tu. Baada ya hapo 96% watarudia kwenye Hali yao. Na Tanzania itarudia kwenye umaskini wake. Yaani huwezi kutangaza mimba Leo na mtoto akazaliwa Leo. UNAHITAJI utayari, ufahamu kidogo na moyo wenye uvumilivu na siyo MTAJI WA Milioni Moja. Hilo halina mjadala.

Hitimisho. Huhitaji MTAJI WA mabilioni Bali UNAHITAJI ufahamu kidogo na moyo wenye utayari na unaovumilia mimba ifikishe miezi 9 au unaovumilia kipindi Cha mpoto ambacho kinaweza kuwa miaka wakati mwingine.
Nakutakia mafanikio mema

Mikael Aweda
0719386100
Ulipotelea wapi Ndugu yangu? Habari za Siku nyingi sana? Asante Sana kwa andiko zuri.
 
Kuna wengi sana hawafanyi Biashara kwa sababu wanadhani kwamba tatizo lao ni kwamba hawana MTAJI. Utamsikia mtu anasema nikipata Mil 10, Au nikipata Mil 100 au nikipata laki 5 nitabadilisha maisha yangu oabisa. Huko ni kutokujua.

Hakuna kitu kama hicho. Hatuhitaji MTAJI mkubwa Bali UNAHITAJI mambo mawili yaani ufahamu kidogo na utayari.

Ifahamu kiasi kidogo unachotaka kufanya.

Pili, uwe na moyo wenye utayari wa kuanza na usiokata tamaa haraka.
kila kitu lazima kianze chini. Mtu anaanza kama mtotot, mti unaanza chini, mnyama hata tembo alikuwa mtoto.

Mbuyu ulikuwa mbegu kwanza.

Kwenye Biashara UNAHITAJI moyo ulio tayari na MTAJI WA 10,000. Wataalam wanasema kama huwezi kubadilisha 10,000 kuwa 100,000 maana yake huwezi kubadilisha milioni mia Moja kuwa kuwa milioni mia mbili.

Kwenye vitabu vitakatifu Kuna mfalme Sulemani aliandika kwenye Mithali 13. 11 kwamba Mali iliyopatikana haraka haraka hupungua, Bali Mali iliyopatikana kidogo kidogo huongezeka. Hii ina maanisha kwamba Kila mtu anatakiwa kuanza chini na siyo juu tena kidogo kidogo.

Uingereza walifanya utafiti wa watu waliopata Bingo ya mabilioni miaka ya nyuma na utafiti ukathibitisha Andiko la Sulemani la kwenye Mithali 13.11.

Ule utafiti uliwafuatilia watu waliopata au kushinda bahati na sibu au Bingo. Baada ya kufanya utafiti walipata matokeo haya 96+3+1=100.

YAANI kati ya watu 100 waliopata fedha za bahati nasibu au Bingo, watu 96 walirudia kwenye umaskini wao baada ya miaka mitatu hadi mitano. Watu watatu wakawa matajiri wa kawaida na Moja akawa tajiri mkubwa sana.

Huu utafiti unathibitisha kwamba Andiko La Sulemani kwenye Mithali 13. 11 na unathibitisha kwamba Changamoto yako siyo MTAJI Bali ufahamu mdogo na Utayari au moyo usiokata tamaa. Lazima uwe na moyo wenye utayari wa kuanza na kuanguka na kuanza na kuanguka na kuanza na kuanguka mpaka ufanikiwe. Haijalishi kama utachukua miezi sita au miaka mitatu.

Wachache sana wako tayari kuingia kwenye hiyo gharama ya kujifunza kidogo na kuwa na moyo usiokata tamaa ndo maana maana matajiri ni wachache. Wengine wanatafuta Hela nyingi bila kujua kwamba Hela nyingi ukipewa Leo ni sawa na kumpeleka mwanafunzi wa darasa la pili wa Shule ya Msingi, akajiunge Chuo kikuu. Ni sawa na kumimina maji ya ndo ya Lita 20 kwenye kikombe Cha chai. Mengi yatamwagika chini. Wakati unaanza chini ufahamu wako pia unaongezeka taratibu kadiri fedha inavyoongezeka. Hiyo ndo siri. Ndo maana Elimu ya darasani siyo kigezo Cha kuwa tajiri.

Leo hii Watanzania wote wakipewa MTAJI wa mil 10, nchi hii itabadilika kwa miaka mitatu tu. Baada ya hapo 96% watarudia kwenye Hali yao. Na Tanzania itarudia kwenye umaskini wake. Yaani huwezi kutangaza mimba Leo na mtoto akazaliwa Leo. UNAHITAJI utayari, ufahamu kidogo na moyo wenye uvumilivu na siyo MTAJI WA Milioni Moja. Hilo halina mjadala.

Hitimisho. Huhitaji MTAJI WA mabilioni Bali UNAHITAJI ufahamu kidogo na moyo wenye utayari na unaovumilia mimba ifikishe miezi 9 au unaovumilia kipindi Cha mpoto ambacho kinaweza kuwa miaka wakati mwingine.
Nakutakia mafanikio mema

Mikael Aweda
0719386100
Siri ya fedha kwa mtazamo wa kiroho na kimwili ni mchanganyiko wa imani, nidhamu na hekima. Hapa ni muhtasari wa siri hizo kwa ngazi zote mbili:


🌿 Kiroho – Fedha kama Baraka
1. Amini wewe unastahili ustawi Woga na hofu huzuia mzunguko wa pesa.
2. Toa kwa nia safi Kupanda huzaa mavuno (sadaka, kusaidia wengine).
3. Omba baraka na maono sahihi Maombi huongoza akili kupata fursa sahihi.
4. Usiwe mtumwa wa fedha Pesa ni chombo, si lengo la maisha.
5. Shukuru kwa kidogo – Shukrani huongeza.

🧠 Kimwili – Nidhamu ya Kifedha
1. Fanya kazi kwa bidii na maarifa Fedha huja kwa juhudi zenye mpango.
2. Tumia chini ya kipato chako Usikimbize maisha ya watu wengine.
3. Wekeza hata kidogo Kilimo, biashara, elimu, au hata akiba.
4. Epuka madeni yasiyo ya lazima Yanavuta roho ya ukata.
5. Jifunze kuhusu fedha kila wakati Maarifa yanazalisha pesa.

⚖️ Muunganiko wa Mwili na Roho
  • Mwili wenye afya hufanya kazi bora fedha huja.
  • Roho yenye amani hufanya maamuzi mazuri fedha hubaki.
  • Akili iliyo huru kutoka hofu huona fursa fedha huongezeka.

Elewa
Fedha huja kwa yule anayeheshimu pesa kwa vitendo, na kuamini kuwa ni zawadi ya utumishi si lengo la maisha.

@*Boss Glala*
🙏🙏,kuna cha kujifunza
Siri ya fedha kwa mtazamo wa kiroho na kimwili ni mchanganyiko wa imani, nidhamu na hekima. Hapa ni muhtasari wa siri hizo kwa ngazi zote mbili:


🌿 Kiroho – Fedha kama Baraka
1. Amini wewe unastahili ustawi Woga na hofu huzuia mzunguko wa pesa.
2. Toa kwa nia safi Kupanda huzaa mavuno (sadaka, kusaidia wengine).
3. Omba baraka na maono sahihi Maombi huongoza akili kupata fursa sahihi.
4. Usiwe mtumwa wa fedha Pesa ni chombo, si lengo la maisha.
5. Shukuru kwa kidogo – Shukrani huongeza.

🧠 Kimwili – Nidhamu ya Kifedha
1. Fanya kazi kwa bidii na maarifa Fedha huja kwa juhudi zenye mpango.
2. Tumia chini ya kipato chako Usikimbize maisha ya watu wengine.
3. Wekeza hata kidogo Kilimo, biashara, elimu, au hata akiba.
4. Epuka madeni yasiyo ya lazima Yanavuta roho ya ukata.
5. Jifunze kuhusu fedha kila wakati Maarifa yanazalisha pesa.

⚖️ Muunganiko wa Mwili na Roho
  • Mwili wenye afya hufanya kazi bora fedha huja.
  • Roho yenye amani hufanya maamuzi mazuri fedha hubaki.
  • Akili iliyo huru kutoka hofu huona fursa fedha huongezeka.

Elewa
Fedha huja kwa yule anayeheshimu pesa kwa vitendo, na kuamini kuwa ni zawadi ya utumishi si lengo la maisha.

@*Boss Glala*
 
Back
Top Bottom